Friday, June 19, 2009

MAMBO YA JEANS ZA KIJAPAN HAYA HAPA

Japanese Jeans. Bringing Sexy Back(A)

Japan has come out with yet another sexy, wild, and edgy fashion trend with these Bikini Jeans, that act as both underwear and jeans.

Sandra Tanimura, a Sanna designer, created these jeans after customers mentioned they had a hard time keeping their low cut jeans up.

“We specialize in making low-rise trousers and our customers wanted them to get even lower.

It was very difficult meeting these demands without the trousers falling down. I came up with the idea of using the bikini strings to let the trousers hang really low without falling,� she added.

Below are some shots of the jeans on a popular Japanese television show:


You can purchase these Bikini Jeans for about $88.
Like all trends, not everyone can pull it off quite the same.

WAZIRI WA USALAMA WA NDANI SOMALIA AUAWA

WAZIRI wa usalama wa ndani wa Somalia Omar Hashi Aden ameuwawa kwenye shambulio la kujitoa muhanga la bomu lililotegwa kwenye gari kaskazini mwa mji mkuu wa Mogadishu.

Watu wengine zaidi ya 20 wameuwawa kwenye mlipuko huo katika Hoteli ya Beledweyne, kaskazini mwa mji mkuu wa Mogadishu.

Miongoni mwa waliouwawa ni maafisa kadhaa wa Kidiplomasia wa Somalia.

Rais wa Somalia Sheikh Sharif Sheikh Ahmed amelaumu kundi la wapiganaji wa Kiislamu la Al-Shabaab , ambalo pia baadaye lilikiri kufanya shambulio hilo.

Kundi hilo linaaminika kuwa na uhusiano na mtandao wa kigaidi wa Al -Qaeda.
Siku ya jumaatano watu 10 walikufa wakati kombora liliporushwa kwenye msikiti mjini Mogadishu.

Katika shambulizi la Alhamisi , walioshuhudia walisema mlipuaji wa kujitoa muhanga alilipua gari lililojaa mabomu kwenye hoteli ya Medina , mjini Beledweyne, yapata Kilomita 400 kaskazini mwa Mogadishu.

Abdulkarim Ibrahim Lakanyo, balozi wa zamani wa Somalia nchini Ethiopia pia ameripotiwa kuwa miongoni mwa waliouwawa.

Mwandishi wa BBC Will Ross anasema bwana Aden alihamia mjini Beledweyne hivi majuzi, mji ulioko karibu na mpaka wa Ethiopia, katika jitihada za kukomesha wanamgambo wa Kiislamu wasiendelee kuthibiti maeneo mengi zaidi.

Rais Ahmed ameambia mkutano wa waandishi wa habari mjini Mogadishu kwamba Somalia imevamiwa na magaidi wasiotaka kuona benderea ya nchi hiyo, wala amani .

Amesema kundi hilo la Al- shabaab linajificha kwenye Uislamu kuendesha ukatili wao.

Somalia haijawa na serikali dhabiti tangu mwaka wa 1991 , na zaidi ya watu milioni nne , ambao ni asilimia 75 ya raia wa nchi hiyo wanahitaji msaada wa chakula.

Kundi la Al- Shabaab ni mshirika katika muungano wa wanamgambo wa kiislamu wenye msimamo mkali ambao wamekuwa wakijaribu kuiangusha serikali ya mpito ya Somalia inayoungwa mkono na umoja wa mataifa.

Rais Ahmed , ambaye mwenyewe ni muislamu mwenye msimamo wa wastani alichukua khatamu nchini Somalia mwezi Januari , lakini hata baada ya kuanzisha utawala wa kuzingatia sheria za kiislamu , hatua hiyo bado haijawaridhisha wapiganaji hao.

Jumaatano , kamanda mkuu wa Polisi mjini Mogadishu aliuwawa kwenye mashambulizi dhidi ya ngome za wanamgambo.

Mwakilishi wa shirika la umoja wa mataifa linaloshughulikia wakimbizi UNHCR nchini Somalia amesema umwagikaji damu wa hivi karibuni nchini Somalia ndio mbaya zaidi kuikumba nchi hiyo kwa muda wa karibu miaka 20.

MTIKISIKO WA YUCHUMI DUNIANI

KATIKA hatua muhimu ya kudhibiti huduma za benki nchini Marekani, Rais Barack Obama ametangaza sera mpya zenye lengo la kuhakikisha msukosuko wa kifedha ulioikumba nchi hiyo hautokei tena.

Kufuatia mabadiliko hayo, benki zilizostawi zitahitajika kukuza hazina ambayo itatumiwa kukabiliana na hasara zozote.

Pia kutabuniwa shirika maalum la kutetea haki za wateja ikiwa ni pamoja na kusimamia mfumo wa rehani na mikopo.

Rais Obama aliyataja mabadiliko hayo kuwa ndiyo muhimu zaidi kuwahi kubuniwa katika mfumo wa fedha nchini Marekani tangu miaka ya 1930.

Benki kuu itasimamia utekelezaji wa mabadiliko na imepewa mamlaka ya kuchunguza mienendo ya taasisi za kifedha na benki.

Rais Obama alisema makampuni mengi pamoja na wateja wamepata hasara kubwa kutokana na kutokuwepo na sera mufti za kusimamia benki.

"Tunafanya kila tuwezalo kujenga msingi thabiti wa kukuza uchumi kwa njia endelevu. Hili halitakuwa jambo rahisi" alisema Rais Obama.

RUBANI AFA NDEGE IKIWA ANGANI

ABIRIA 247 wameponea chupuchupu katika kisa ambacho wengi watadhani ni muujiza!!!Abiria 247 waliokuwa wakisafiri na ndege ya kampuni ya Continental kutoka Ubelgiji hadi Marekani waliponea chupuchupu wakati nahodha wa ndege yao alipofariki dunia.

Msemaji wa Halmashauri inayosimamia usafiri wa ndege Marekani, Arlene Salac alisema kulikuwa na marubani wengine wawili ambao waliidhibiti ndege hiyo aina ya Boeing 777 hadi uwanja wa ndege wa Newark Liberty ambako ilitua kwa dharura.

Mtaalamu mmoja wa usafiri wa ndege, Jim Ferguson alisema si jambo la kawaida rubani kufariki dunia akiwa angani.

Kwa kawaida ndege hiyo huendeshwa na marubani wawili. Lakini kwa bahati nzuri wakati huu, kulikuwa na mwingine wa ziada.

Bwana Ferguson alisema ingekuwa vigumu kwa rubani mmoja kuidhibiti ndege hiyo kutua.
Abiria hawakuambiwa lolote kuhusu mkasa huo.

Miongoni mwao alikuwa daktari mmoja wa maswala ya moyo, Dr. Julien Struyven ambaye aliitikia tangazo daktari yeyote kwenye ndege hiyo kujitokeza.

Abiria hawakujua kwamba mwito ulitolewa kwa ajili ya kumuokoa rubani wa ndege hiyo.
Dr Struyven alipomfikia rubani huyo alikuta kama tayari ameaga dunia.
“Hakukuwa na uwezekano wowote wa kumwokoa,” alisema Dr Struyven.

Alisema huenda rubani huyo mwenye umri wa miaka 60 na ambaye amehudumia kampuni hiyo kwa zaidi ya miaka 20 alifariki dunia kutokana na matatizo ya moyo

RUBANI AFA NDEGE IKIWA ANGANI

Rubani afa ndege ikiwa angani Abiria 247 waponea chupuchupu Katika kisa ambacho wengi watadhani ni muujiza, abiria 247 waliokuwa wakisafiri na ndege ya kampuni ya Continental kutoka Ubelgiji hadi Marekani waliponea chupuchupu wakati nahodha wa ndege yao alipofariki dunia.

Msemaji wa Halmashauri inayosimamia usafiri wa ndege Marekani, Arlene Salac alisema kulikuwa na marubani wengine wawili ambao waliidhibiti ndege hiyo aina ya Boeing 777 hadi uwanja wa ndege wa Newark Liberty ambako ilitua kwa dharura.

Mtaalamu mmoja wa usafiri wa ndege, Jim Ferguson alisema si jambo la kawaida rubani kufariki dunia akiwa angani.

Kwa kawaida ndege hiyo huendeshwa na marubani wawili. Lakini kwa bahati nzuri wakati huu, kulikuwa na mwingine wa ziada.

Bwana Ferguson alisema ingekuwa vigumu kwa rubani mmoja kuidhibiti ndege hiyo kutua.
Abiria hawakuambiwa lolote kuhusu mkasa huo.

Miongoni mwao alikuwa daktari mmoja wa maswala ya moyo, Dr. Julien Struyven ambaye aliitikia tangazo daktari yeyote kwenye ndege hiyo kujitokeza.

Abiria hawakujua kwamba mwito ulitolewa kwa ajili ya kumuokoa rubani wa ndege hiyo.
Dr Struyven alipomfikia rubani huyo alikuta kama tayari ameaga dunia.
“Hakukuwa na uwezekano wowote wa kumwokoa,” alisema Dr Struyven.

Alisema huenda rubani huyo mwenye umri wa miaka 60 na ambaye amehudumia kampuni hiyo kwa zaidi ya miaka 20 alifariki dunia kutokana na matatizo ya moyo

Tuesday, June 16, 2009

WAETHIOPIA 98 WATIWA MBARONI MKOANI MBEYA.

HAWA ni raia 98 kutoka nchini Ethiopia waliotiwa mbaroni kijiji cha Ulenje, wilaya ya Mbeya vijijini kwa kuingia nchini kinyume cha sheria wakiwa safarini kuelekea nchini Malawi ambako walidai kuwa walikuwa wanaenda kuomba Ukimbizi.Hapa walikuwa wakitolewa ofisi za Uhamiaji mkoa kupelekwa mahabusu kituo kikuu cha polisi.

MIST YAPANIA KUONGEZA UDAHILI KWA WANAWAKE

TAASISI ya Sayansi na Teknolojia Mbeya (MIST), imeanza kutekeleza agizo la Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Profesa Peter Msolla, la kuhakikisha kuwa wanaongeza udahili wa wanafunzi wa kike kujiunga chuoni hapo.

Hadi sasa walimu wa taasisi hiyo wamezitembelea shule za sekondari 21 mkoani hapa, ili kutoa elimu kwa wanafunzi wa kike kupenda kusoma masomo ya sayansi,Hisabati na ufundi.

Profesa Msolla alitoa agizo hilo hivi karibuni wakati akizindua shahada katika fani za biashara na uhandisi katika fani za ujenzi, umeme, Mitambo na Usanifu wa Majengo, katika taasisi hiyo.

Mkuu wa MIST Profesa Joseph Msambichaka, aliyasema hayo jana, wakati akielezea kuhusu hatua ya taasisi hiyo kuandaa semina ya siku tatu kwa kushirikiana na asasi ya Peace Corps Tanzania ya nchini Marekani, kwa ajili ya kumuwezesha mtoto wa kike kuyapenda masomo hayo.

Semina hiyo inashirikisha wanafunzi wa kike 80, wa shule za msingi na sekondari kutoka wilaya wilaya zote za mkoa wa Mbeya, na wanafundishwa na wataalam saba wa kujitolea, kutoka Peace Corps Tanzania.

Profesa Msambichaka alisema kuwa tatizo kubwa lililopo ni kuwa wanafunzi wa kike wamekuwa na tabia ya kuyakimbia masomo ya sayansi na kuwaachia watoto wa kikume madai kuwa masomo hayo ni magumu kitu ambacho siyo kweli.

Alisema kuwa hivi sasa MIST inao utaratibu wa kutoa mafunzo maalumu kwa ajili ya somo la Hisabati kwa watoto wa kike wanaokuwa wamemaliza elimu ya sekondari.

"Wale wanaokuwa wamefaulu vizuri huwa serikali inaingia gharama ya kuwasomesha kwa muda wote wanaokuwepo hapa taasisi lengo likiwa ni kuwahamasisha kuyapenda masomo ya sayansi" alisema Msambichaka.

Profesa Msambichaka alisema kuwa mwaka 2008, wanafunzi wa kike 13 walifanya masomo hayo maalumu, ambapo kwa mwaka jana waliojitokeza walikuwa ni zaidi ya 50.

Nao washiriki wa semina hiyo, wakizungumza kwa nyakati tofauti na Uhuru, walisema kuwa wanashukuru kwa kupata semina hiyo kwani ni ukweli kuwa watoto wa kike wapo nyuma.

Walisema kuwa wazazi wengi huwa wanawaona watoto wa kiume kuwa ndio wanaopaswa kusoma na wao kupenda kufanyishwa kazi za nyumbani hivyo huwa na muda kidogo wa kujisomea tofauti na wenzao wanaume.

"Tunataka kuiambia jamii kuwa tulikuwa nyuma kutokana na mfumo dume uliojenga kwa muda mrefu...watoto wa kike tulikuwa tunaonekana kwamba hatuwezi kusoma kwani mzazi aliyekuwa anamsomsemesha mtoto wa kike alikuwa akionekana anapoteza muda" walisema.

WHO YAISAIDIA TANZANIA FRIJI KUMI ZA KUHIFADHIA DAMU SALAMA

SHIRIKA la Afya Duniani (WHO),limetoa msaada wa friji kumi za kuhifadhia damu kwa Tanzania, kutokana na mafanikio makubwa yaliyoyafikiwa kwa muda mfupi tangu mpango wa damu salama uanzishwe mwaka 2005.

Imeelezwa kuwa hatua hiyo ya WHO ni kuichangia mpango wa damu salama nchini.

Hayo yamo katika salamu za Mkurugenzi wa shirika hilo,barani Afrika Dk.Luis Gomes Sambo, zilizotolewa katika kilele cha maadhimisho ya siku ya kuchangia damu duniani, ambapo kitaifa ilifanyika katika viwanja vya Ruanda Nzovwe jijini mbeya.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo yaliyotanguliwa na maandamano kutoka kituo cha mafuta Oil Com kilichopo Soweto hadi katika viwanja hivyo, alikuwa ni Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Profesa David Mwakyusa.

Sambo alisema kuwa tunaposherehekea na kuwatambua wachangia damu kwa hiyari, kwa ‘zawadi ya uhai’ ni muhimu kukumbuka kuwa ongezeko la wachangiaji damu hao mara kwa mara ndio njia pekee ya kuhakikisha upatikanaji wa damu salama kwa kila mgonjwa.Mkurugenzi huyo wa WHO barani afrika alisema:

”Mahitaji ya damu barani Afrika yanaongozwa na tatizo la vifo vya kina mama hadi kufikia elfu moja ambapo kwa watoto laki moja wanaozaliwa hai, zaidi ya asilimia 40 ya vifo vyao husababishwa na kutokwa damu”.

Aliongeza kuwa inakadiriwa kuwa asilimia 90 ya vifo milioni moja kila mwaka duniani kote, kutokana na ugonjwa wa maralia hutokea katika bara la afrika wakati kwa sehemu nyingine vifo hivyo vinavyotokana na maralia kali na ukosefu wa damu hufikia hadi asilimia saba na nusu.Dk.

Sambo alisema WHO limeunda mkakati wa damu salama mnamo mwaka 2001 nia ikiwa ni kulenga utoshelevu pamoja na usalama wa damu na tangu wakati huo kumekuwa na maendeleo mazuri katika kukusanya na kupima damu pia kuzuia magonjwa yanayoenea kwa damu.

“Lengo mojawapo katika mkakati huu ni kila nchi iweze kuchangia kwa hiari sio chini ya asilimia 80 ya mahitaji yake ya damu ifikapo mwaka 2012” alisema Dk.Sambo.

Aliongeza kuwa zaidi ya asilimia 50 ya nchi wanachama wamefikia lengo hilo ambapo nchi kumi na mbili kati ya 46 hukusanya damu yote inayohitajika kutoka kwa wachangia damu kwa hiari.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo, zaidi ya lita milioni 3.2 ya damu inakusanywa barani humu ila hata hivyo kuna upungufu kutokana na mahitaji ya lita milioni nane kwa mwaka hivyo juhudi zaidi zinahitajika ili kufikia lengo hilo.

Naye Meneja wa Mpango wa Damu salama nchini, Efespar Nkya,alisema hapo awali kulikuwa hakuna mfumo uliokuwa ukisimamia na kuratibu huduma za upatikanaji na upimaji damu uliokuwa ukizingatia ubora wa viwango.

Nkya alisema mfumo huu unategemea wachangiaji ndugu,marafiki na wakati mwingine watu wanaolipwa na kuwa mfumo huo una kiwango kiwango kikubwa cha maambukizi ya magonjwa kupitia kwenye damu, upungufu wa damu mara kwa mara na kukosekana.

MBEYA YATAWALIWA NA MAUJI MFULULIZO.

>WENGINE WAWILI WAUAWA NDANI YA NYUMBA KISHA KUCHOMWA MOTO.

MWANAMKE mmoja wa kijiji cha Mwaoga-Makongorosi, amekufa papo hapo baada ya kukatwa katwa mapanga na mwanaume ambaye naye alikamatwa na wananchi wenye hasira kali na kuuawa.

Tukio hilo la aina yake linalodaiwa chanzo ni wivu wa kimapenzi, limetokea jana saa 7:40 mchana, katika kijiji hicho kilichopo wilayani Chunya mkoani Mbeya.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kaimu Kamanda wa polisi mkoani hapa, Monica Madembwe, alisema kuwa marehemu wote wawili hawajaweza kufahamika majina ya.

Monica alisema kuwa mwanamke huyo mwenye umri kati ya miaka 30-35, akiwa katika barabara ya Mkwajuni kwenda Makongorosi, alishambuliwa na mwanaume huyo mwenye umri kati ya miaka 20-25 kwa kukatwa katwa mapanga na kufariki papo hapo.

Kaimu Kamanda Monica alisema baada ya kufanya mauaji hayo, wananchi wenye hasira kali walimkamata na kumshambulia kwa mawe, fimbo na marungu hadi na yeye kufariki.

Aliongeza kuwa hakuna mtu ama watu waliokamatwa kuhusiana na tukio hilo, ambalo chake chake inasadikiwa ni wivu wa kimapenzi.Uchunguzi zaidi unaendelea.

Katika tukio lingine lilitokea kijiji cha Itimba-Utengule wilaya ya Mbeya vijijini, watu wawili wameuawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani wakiwa ndani ya nyumba yao.

Monica aliwataja marehemu hao kuwa ni Merry Mpenzu (50) na William Mpenzu (30).

Akielezea zaidi tukio hilo, alisema marehemu hao wawili wakiwa ndani ya nyumba walivamiwa na watu wasiofahamika na kupigwa na kitu kizito vichwani, kufungiwa mlango na baadaye nyumba hiyo kuwashwa moto.

"Nyumba yao ilikuwa imeeezekwa kwa nyasi, hivyo baada ya marehemu hao kuuawa, wauaji hao waliezua paa la nyumba hiyo na kulitumia kuchoma moto nyumba hiyo huku marehemu hao wakiwa ndani" alisema Monica.

Uchunguzi zaidi kujua chanzo cha mauaji hayo pamoja na kuwasaka watuhumiwa unaendelea kufanywa.Wakati huo huo mkazi wa kijiji cha Hatelele, wilayani Mbozi ameuawa kwa kukatwa na kitu chenye ncha kikali kichwani.

Marehemu ametajwa kuwa ni Evance Halele (29), ambaye mwili wake ulikutwa umetupwa kwenye mtaro wa barabara.

Imedaiwa kuwa marehemu alikuwa anajishughulisha na matukio ya wizi na hakuna mtu aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo.

Wednesday, June 3, 2009

WAPATA HATI SAFI YA UKAGUZI WA HESABU

HALMASHAURI ya wilaya ya Chunya mkoani Mbeya, ni miongoni mwa halmashauri 54 nchini, zilizofanikiwa kupata hati safi ya ukaguzi wa hesabu kwa mwaka wa fedha 2007/2008.

Hilo limetokana na halmashauri kuwa na watumishi wenye uwezo na pia kitengo cha ukaguzi wa ndani kufanya ukaguzi wa mara kwa mara katika idara za halmashauri hiyo.

Mkaguzi wa ndani wa halmashauri hiyo, Saimon Minja, aliyasema hayo jana alipokuwa akizungumzia kuhusu jitihada zinazofanywa na kitengo hicho muhimu katika kuhakikisha halmashauri hiyo inasonga mbele.

Minja alisema kwa kitengo hicho kufanya ukaguzi wa mara kwa mara, huwa inasaidia wahusika kurekebisha makosa yao na hivyo anapokuja mkaguzi wa nje, huwa anakuta matatizo yote yameisharekebishwa.

"Pia kitu kingine kilichotusaidia kupata hati safi ni ushirikiano mkubwa uliopo kati ya kitengo cha ukaguzi wa ukaguzi wa ndani na Mkurugenzi Maurice Sapanjo, hali ambayo inafanya mazingira ya kazi kuwa rahisi" alisema Minja.

Aliongeza kuwa Mkurugenzi Sapanjo amekuwa anatumia taarifa za kitengo hicho kuwakemea na pia kuwashauri wakuu wa idara kutokana na taarifa anazokuwa amefikishwa mezani pake.

Alisema Changamoto waliyonayo hivi sasa ni ukubwa wa wilaya hiyo hivyo kuwa kikwazo kwao kuweza kufika maeneo yote ya wilaya hiyo kwa ajili ya kufanya ukaguzi wa ndani wa hesabu.

Ofisa huyo wa wilaya alisema vile vile kitengo hicho cha ukaguzi wa ndani hakina usafiri hali inayowalazimu kuomba magari kutoka idara nyigine, na inapotokea magari hayo kuwa na kazi hulazimika kusubiri ili kwenda kutekeleza majukumu yao.

Minja alisema:"Kuna dhana potofu iliyopo wilayani hapa kwa baadhi ya watu wakiwemo wana-siasa kuwa Mkaguzi wa ndani anatakiwa kuwakamata watu wanaobainika kufuja fedha za halmashauri, kitu ambacho siyo sahihi".

Alifafanua zaidi kauli yake hiyo kuwa wao wanachokifanya mara baada ya kubaini ubadhirifu wa fedha ndani ya idara yoyote huwa wanazifikishga taarifa kwa Mkurugenzi kwa hatua zaidi na wao huwa hawana uwezo wa kuwa polisi wa kuwakamata wabadhirifu hao.

Minja aliongeza kuwa pia kitengo hicho kinakabiriwa na upungufu wa watumishi kwani kinao wawili tu na mmoja hivi sasa yupo masomoni, hali inayofanya utendaji wa kazi kuwa mgumu hasa ukizingatia kuwa wilaya ina eneo kubwa kuliko wilaya nyigine zote mkoani hapa.

CHUNYA WAKAMATA MAKOKORO YENYE THAMANI YA ZAIDI YA SH.MILIONI 20

MAKOKORO 103 yenye thamani ya zaidi ya shilingi 20,600,000, yamekamatwa katika maeneo ya Isanzu na Udinde yaliyopo pembezoni mwa Ziwa Rukwa, wilayani Chunya.

Imeelezwa kuwa wamiliki wa makokoro hayo hawakuweza kutiwa mbaroni baada ya kuwahi kukimbia na kuyatelekeza makokoro hayo.

Akizungumza Ofisa Uvuvi wa wilaya hiyo, Christina Potta, alisema kuwa operesheni ya kuyakamata makokoro hayo ilifanyika kati ya Mei 3, na hadi 14, mwaka huu katika maeneo hayo yaliyopo Ziwa Rukwa, upande wa wilaya ya Chunya.

Christina alisema kuwa matumizi ya makokoro huwa yanapelekea upungufu wa samaki kwani nyavu za aina hiyo (makokoro), kutokana na kuwa na macho madogo zinapovutwa huharibu viota, mayai, vifaranga vya samaki na hivyo kuua vizazi vya samaki.

Aliongeza kuwa katika zoezi hilo, wilaya hiyo ilishirikiana na kikosi cha doria cha uvuvi cha Kanda ya Kasanga, kilichopo mkoani Rukwa.

"Kazi ya kutupa makokoro ziwa Rukwa huwa inafanywa nyakati za usiku, hivyo hutuwia vigumu kuwatia mbaroni watuhumiwa na huwa tukienda mchana huwa ntunafanikiwa kuyakukuta makokoro lakini wamiliki wake huwa wanafanikiwa kukimbia" alisema Christina.

Ofisa Uvuvi huyo wa wilaya alisema ili kukabiriana na wavuvi ambao wamekuwa watumiaji wakubwa wa makokoro, wilaya imekuwa inajitahidi kutoa elimu kwa wananchi juu athari za makokoro.Christina alisema:

"Tunaendelea kushirikiana na viongozi wa vijiji katika utoaji elimu hali iliyopelekea baadhi ya wavuvi kwa hiyari yao wenyewe, kuamua kuanza kusalimisha makokoro waliyokuwa wanayatumia".

Aliongeza kuwa changamoto kubwa wanayokutana nayo ni kuwa watumiaji wa makokoro hayo kwa kutumia simu za kiganjani, wamekuwa wanapeana taarifa kila unapofanyika msako hali inayowawia vigumu kuwatia mbaroni watuhumiwa ili kuwafikisha mbele ya sheria.

Alisema wilaya katika kukabiriana na tatizo hilo, imefanikiwa kukamilisha matengenzo ya Boti ya doria ambayo tayari imetumbukizwa kwenye Ziwa Rukwa, ambayo itasaidia sana kukabiriana na wavuvi wanaotumia makokoro katika shughuli zao za uvuvi.

TAMISEMI WAPOKEA MALUMBANO KATI YA KAPUNGA NA ELIZABETH

WAZIRI wa Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI),Selina Kombani, amesema kuwa ofisi yake imepokea taarifa za kuwepo malumbano kati ya watendaji na viongozi wa siasa jijini Mbeya.

Alisema lakini serikali haiwezi kuzifanyia kazi hizo za malalamiko bila ya kuzifanyia utafiti, hivyo kuwataka waliopeleka taarifa hizo kuvuta subira.

“Nawaomba wale walioniletea taarifa hizi ofisini kwangu kuwa na subira ili niweze kuniwezesha kufanya utafiti kwa nia ya kutoa majibu yaliyo sahihi” alisema Selina.

Hayo aliyasema jana mjini hapa, mara baada ya kufungua semina ya madiwani wanawake mkoani hapa,katika ukumbi wa Benjamini Mkapa yenye nia ya kuwawezesha kuwa na ujasiri katika kugombea nafasi za uongozi.

Waziri wa TAMISEMI alisema ofisi yake ilishapokea taarifa za kuwepo malumbano kati ya watendaji na viongozi wa kisiasa wa halmashauri ya jiji la Mbeya.

Aliongeza kuwa hatua za awali zilizochukuliwa ni kufanya utafiti wa chanzo cha malumbano hayo, ambapo baada ya kubainika chanzo cha tatizo hilo ndipo utatolewa uamuzi utakaokuwa na nia ya kuutendea haki kila upande.Selina alisema:

”Lengo la TAMISEMI kukaa kimya muda mrefu bila ya kutoa maamuzi ya malalamiko hayo (hakutaja kundi lililopeleka kwakwe), ni kuhakikisha uamuzi unaotolewa hauumizi upande mmoja au kuwagawa wahusika”.

Waziri huyo alikiri kuwa ni kweli ofisi ama sehemu yoyote inayokuwa na malumbano, shughuli za utendaji hushuka lakini hilo haliwezi kuifanya serikali ikatoa maamuzi yasiyofanyiwa utafiti wa kina hivyo kuwataka wananchi kuwa wavumilivu.

“Nakubaliana nanyi kuwa sehemu kunapokuwa na malumbano ya namna hii kazi nyingi zinafanyika kwa kiwango cha chini…lakini kwa kuwa hazijasimama kabisa,niwaombe wananchi wa Mbeya na taifa kwa ujumla kuvuta subira ili uamuzi utakaotolewa uwe na manufaa kwa wote” alisema Selina.

Alisema utaratibu uliopo TAMISEMI ni kuwa wanafanyia kazi maelezo yaliyotolewa na pande zote mbili kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na maofisa wake na kwamba vikao vitaketi na kupitia taarifa hiyo ili kufikia uamuzi.

Malumbano yaliyofikishwa TAMISEMI ni kati ya mkurugenzi wa jiji la Mbeya, Elibeth Munuo na Meya wake Athanas Kapunga, ambapo kwa nyakati tofauti kila mmoja amekuwa akimlaumu mwenzake kuwa ni chanzo cha matatizo mbalimbali katika halmashauri hiyo.