Saturday, May 30, 2009
WASAHINDI WATATU WA MISS MBEYA 2009
MARY KAGALI MISS MBEYA 2009
MARY Kagali (19), ameshinda taji la Miss Mbeya 2009, baada ya kuwashinda warembo wengine kumi na mmoja waliojitokeza kuwania taji hilo na kujinyakulia zawadi ya sh.800,000.
Shindano hilo, liliingia dosari baada ya kiongozi wa majaji,Tasha Jim kumtangaza mrembo, Raulensia Laurency kuwa mshindi namba mbili, hali iliyopelekea ukumbi mzima kuzomea kupinga matokeo hayo.
Mamia ya mashabiki lukuki waliohudhuria shindano hilo, lililofanyikia katika ukumbi wa Benjamin Mkapa, walifikia hatua hiyo baada ya Raulensia kushindwa kuonyesha uwezo katika kutembea pia kwenye kujibu swali ili kumpima ufahamu wake.
Kwa kushinda nafasi hiyo, mrembo huyo alijinyakulia zawadi ya shilingi 400,000 huku nafasi ya tatu ikitwalia na Agnes Mpona, aliyezawadiwa shilingi 200,000.
Warembo hao watatu wataungana na mrembo aliyeshika ya nne, Jacqueline Magayane kuingia katika shindano la kumsaka mrembo wa kanda ya nyanda za juu kusini.
Awali warembo hao kumi na wawili walipita jukwaani na kuonyesha mavazi ya ubunifu, ufukweni na baadaye kumaliza na vazi la kutokea jioni, ambapo walichujwa na kupatikana tano bora.
Waliofanikiwa kuingia tano ni Jacqueline Magayane, Neema Mushi, Agnes Sasawata, Raulensia Laurency na Mary Kagali ambaye kila alipokuwa akipita jukwaani ukumbi mzima ulikuwa unalipuka kwa kofi na mayowe kumshangilia.
Mashabiki wa shindano hilo, walimtupia lawama jaji mkuu, Tasha Jim, kwa kuharibu shindano hilo kufuatia kumtangaza Raulensia kuwa mshindi wa pili ambaye wengi waliona kuwa hakustahili kutwaa nafasi hiyo.
Shindano hilo, lilipambwa na burudani kutoka kikundi cha muziki wa taarabu cha Victoria Modern kutoka Dar es Salaam lenye wasani wa kike watupu pamoja na kundi la muziki kutoka jijini Mbeya lililo chini ya msanii Robby Matunda.
Shindano hilo, liliingia dosari baada ya kiongozi wa majaji,Tasha Jim kumtangaza mrembo, Raulensia Laurency kuwa mshindi namba mbili, hali iliyopelekea ukumbi mzima kuzomea kupinga matokeo hayo.
Mamia ya mashabiki lukuki waliohudhuria shindano hilo, lililofanyikia katika ukumbi wa Benjamin Mkapa, walifikia hatua hiyo baada ya Raulensia kushindwa kuonyesha uwezo katika kutembea pia kwenye kujibu swali ili kumpima ufahamu wake.
Kwa kushinda nafasi hiyo, mrembo huyo alijinyakulia zawadi ya shilingi 400,000 huku nafasi ya tatu ikitwalia na Agnes Mpona, aliyezawadiwa shilingi 200,000.
Warembo hao watatu wataungana na mrembo aliyeshika ya nne, Jacqueline Magayane kuingia katika shindano la kumsaka mrembo wa kanda ya nyanda za juu kusini.
Awali warembo hao kumi na wawili walipita jukwaani na kuonyesha mavazi ya ubunifu, ufukweni na baadaye kumaliza na vazi la kutokea jioni, ambapo walichujwa na kupatikana tano bora.
Waliofanikiwa kuingia tano ni Jacqueline Magayane, Neema Mushi, Agnes Sasawata, Raulensia Laurency na Mary Kagali ambaye kila alipokuwa akipita jukwaani ukumbi mzima ulikuwa unalipuka kwa kofi na mayowe kumshangilia.
Mashabiki wa shindano hilo, walimtupia lawama jaji mkuu, Tasha Jim, kwa kuharibu shindano hilo kufuatia kumtangaza Raulensia kuwa mshindi wa pili ambaye wengi waliona kuwa hakustahili kutwaa nafasi hiyo.
Shindano hilo, lilipambwa na burudani kutoka kikundi cha muziki wa taarabu cha Victoria Modern kutoka Dar es Salaam lenye wasani wa kike watupu pamoja na kundi la muziki kutoka jijini Mbeya lililo chini ya msanii Robby Matunda.
MHANDISI MSHAURI WA MAJENGO MKOA WA MBEYA AMCHEFUA RC.
MKUU wa mkoa wa Mbeya, John Mwakipesile, amemuagiza Katibu Tawala, Beatha Swai, kumuondoa Mhandisi mshauri wa majengo, Aidan Ngwada, kufuatia kuboronga katika utendaji wake wa kazi.
Hatua hiyo imefikiwa kufuatia malalamiko mengi kutolewa kuhusu idara ya Uhandisi mkoani hapa, hali inayopelekea miradi mingi inayofanyika kuwa chini ya kiwango cha ubora.
Mwakipesile alifikia hatua hiyo jana katika kikao cha Kamati ya Ushauri ya mkoa (RCC), kilichofanyika jana katika ukumbi wa Dk.Ali Shein, baada ya wakuu wa wilaya watatu, kumnyoshea kidole Ngwada, kuwa kazi anazosimamia hazina kiwango.
Alisema kuwa idara hiyo ni mbovu ambapo fedha nyingi zinazotolewa na serikali kuu kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali zimekuwa zinatumika isivyo huku miradi hiyo ikiwa haina ubora wowote.
"Tumechoka na kazi mbovu za Uandisi katika serikali ya mkoa wa Mbeya na hatuwezi kuendelea kukaa kimya wakatri fedha za serikali zinatumika vibaya huku miradi ikiwa haina ubora unaotakiwa" alisema Mwakipesile.
Aliongeza kuwa hataki kuwa sehemu ya wizi huo unaofanyika katika idara hiyo na awali alishawahi kumtaka aliyekuwa Katibu Tawala mkoani hapa Assumpta Ndimbo, kumuondoa Mhandisi huyo lakini haelewi ni vipi anaendelea kushikilia wadhifa huo hadi leo.
Mkuu wa mkoa alisema:"Sitaki kuwa sehemu ya wizi huu, inawezekana wewe ni injinia mbovu, huna cheti na iwapo hivi vyote unavyo basi ni wazi unashirikiana na wengine katika wizi".
Alisema kuwa serikali imeajiri wahandisi kwa kila wilaya, lakini wamekuwa wanalipwa tu mishahara bila ya kufanya kazi zozote kutokana na ukiritimba unaofanywa na Ngwada wa kwenda kufanya kazi hizo badala ya kuziachia wilaya husika.
Akizungumza kwa hasira, Mwakipesile alisema hawezi kukubali yeye aonekane ni sehemu ya ubovu katika mkoa wa Mbeya, kwani kila siku amekuwa akipokea malamiko ya ujenzi mbovu wa barabara hasi nyumba za wakuu wa wilaya na makatibu Tawala wa wilaya.
"Hivyo nawaomba wajumbe tusiendelee kuchangia katika hili, kwani kwa kuwa Katibu Tawala Beatha yupo, amesikia na atalifanyia kazi...tumuachie hili mikononi mwake" alisema Mwakipesile.
Kufuatia hali ya hewa kuchafuka, mara baada ya Mkuu wa mkoa kumaliza kuitolea ufafabnuzi hoja hiyo iliyokuwa imeibuliwa na Wakuu wa wilaya za Chunya, Kyela na Mbeya, mnamo saa 7:20 mchana Ngwada alisimama na kutoka nje ya ukumbi na hakurejea tena hadi kikao hicho kinafungwa saa 9:00 alasiri.
Waandishi walipotoka nje ili kumuomba Ngwada atoe ufafanuzi kuhusu kilichotokea, aliwaomba wamuache kwani hajisikii vizuri na kuwa mapigo ya moyo (BP), hayapo salama.
Hatua hiyo imefikiwa kufuatia malalamiko mengi kutolewa kuhusu idara ya Uhandisi mkoani hapa, hali inayopelekea miradi mingi inayofanyika kuwa chini ya kiwango cha ubora.
Mwakipesile alifikia hatua hiyo jana katika kikao cha Kamati ya Ushauri ya mkoa (RCC), kilichofanyika jana katika ukumbi wa Dk.Ali Shein, baada ya wakuu wa wilaya watatu, kumnyoshea kidole Ngwada, kuwa kazi anazosimamia hazina kiwango.
Alisema kuwa idara hiyo ni mbovu ambapo fedha nyingi zinazotolewa na serikali kuu kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali zimekuwa zinatumika isivyo huku miradi hiyo ikiwa haina ubora wowote.
"Tumechoka na kazi mbovu za Uandisi katika serikali ya mkoa wa Mbeya na hatuwezi kuendelea kukaa kimya wakatri fedha za serikali zinatumika vibaya huku miradi ikiwa haina ubora unaotakiwa" alisema Mwakipesile.
Aliongeza kuwa hataki kuwa sehemu ya wizi huo unaofanyika katika idara hiyo na awali alishawahi kumtaka aliyekuwa Katibu Tawala mkoani hapa Assumpta Ndimbo, kumuondoa Mhandisi huyo lakini haelewi ni vipi anaendelea kushikilia wadhifa huo hadi leo.
Mkuu wa mkoa alisema:"Sitaki kuwa sehemu ya wizi huu, inawezekana wewe ni injinia mbovu, huna cheti na iwapo hivi vyote unavyo basi ni wazi unashirikiana na wengine katika wizi".
Alisema kuwa serikali imeajiri wahandisi kwa kila wilaya, lakini wamekuwa wanalipwa tu mishahara bila ya kufanya kazi zozote kutokana na ukiritimba unaofanywa na Ngwada wa kwenda kufanya kazi hizo badala ya kuziachia wilaya husika.
Akizungumza kwa hasira, Mwakipesile alisema hawezi kukubali yeye aonekane ni sehemu ya ubovu katika mkoa wa Mbeya, kwani kila siku amekuwa akipokea malamiko ya ujenzi mbovu wa barabara hasi nyumba za wakuu wa wilaya na makatibu Tawala wa wilaya.
"Hivyo nawaomba wajumbe tusiendelee kuchangia katika hili, kwani kwa kuwa Katibu Tawala Beatha yupo, amesikia na atalifanyia kazi...tumuachie hili mikononi mwake" alisema Mwakipesile.
Kufuatia hali ya hewa kuchafuka, mara baada ya Mkuu wa mkoa kumaliza kuitolea ufafabnuzi hoja hiyo iliyokuwa imeibuliwa na Wakuu wa wilaya za Chunya, Kyela na Mbeya, mnamo saa 7:20 mchana Ngwada alisimama na kutoka nje ya ukumbi na hakurejea tena hadi kikao hicho kinafungwa saa 9:00 alasiri.
Waandishi walipotoka nje ili kumuomba Ngwada atoe ufafanuzi kuhusu kilichotokea, aliwaomba wamuache kwani hajisikii vizuri na kuwa mapigo ya moyo (BP), hayapo salama.
Friday, May 29, 2009
TANROADS MBEYA WATAKIWA KUWASILISHA BAJETI
WAJUMBE wa kikao cha Bodi ya barabara mkoa wa Mbeya, wamemuagiza Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), mkoa kuhakikisha kuwa bajeti ya barabara inayotakiwa kupitishwa inapitiwa kwanza na kikao hicho.
Imeelezwa kuwa TANROADS wamekuwa wanapitisha bajeti hiyo na kuamua wao barabara za kuzitengeneza badala ya zile zinazotakiwa na wananchi wa wilaya husika.
Wakichangia katika kikao cha Bodi ya Barabara kilichofanyika jana.chini ya Uenyekiti wa Mkuu wa mkoa wa Mbeya,wajumbe hao walisema kuwa barabara zinazotengenezwa na TANROADS zinatakiwa kujibu kero za wananchi na siyo nje ya hapo.
Walisema kuwa hivyo kuanzia bajeti ijayo ni lazima kabla ya kupitishwa iwe inaletwa kwenye kikao hicho kujadiriwa ili barabara zitakazotengenezwa ziwe ni zile zinazopewa kipaumbele na wananchi na siyo wakala huyo wa barabara.
“Ni vyema hili lifanyiwe kazi ili barabara zile zinazotakiwa na wananchi kutokana na umuhimu wake ndizo zipewe kipaumbele cha kwanza na siyo zile ambazo TANROADS mmekuwa mnaziamua na kuzipangia bajeti bila ya kutushirikisha” walisema.
Imeelezwa kuwa TANROADS wamekuwa wanapitisha bajeti hiyo na kuamua wao barabara za kuzitengeneza badala ya zile zinazotakiwa na wananchi wa wilaya husika.
Wakichangia katika kikao cha Bodi ya Barabara kilichofanyika jana.chini ya Uenyekiti wa Mkuu wa mkoa wa Mbeya,wajumbe hao walisema kuwa barabara zinazotengenezwa na TANROADS zinatakiwa kujibu kero za wananchi na siyo nje ya hapo.
Walisema kuwa hivyo kuanzia bajeti ijayo ni lazima kabla ya kupitishwa iwe inaletwa kwenye kikao hicho kujadiriwa ili barabara zitakazotengenezwa ziwe ni zile zinazopewa kipaumbele na wananchi na siyo wakala huyo wa barabara.
“Ni vyema hili lifanyiwe kazi ili barabara zile zinazotakiwa na wananchi kutokana na umuhimu wake ndizo zipewe kipaumbele cha kwanza na siyo zile ambazo TANROADS mmekuwa mnaziamua na kuzipangia bajeti bila ya kutushirikisha” walisema.
MKANDARASI ABORONGA UJENZI WA BARABARA JIJINI MBEYA
SERIKALI mkoa wa Mbeya, imeuagiza uongozi wa halmashauri ya jiji la Mbeya, kutomkamilisha malipo mkandarasi aliyejenga barabara inayoanzia benki ya Stanbic, kuelekea Ikulu ndogo kwani imejengwa chini ya kiwango.Imeelezwa kuwa hadi sasa halmashauri tayari imemlipa Mkandarasi huyo shilingi milioni 43 kati ya milioni 132 anazotakiwa kulipwa kwa kazi hiyo.
Agizo hilo limetolewa jana na Mkuu wa mkoa wa Mbeya,John Mwakipesile, kufuatia malalamiko yaliyofikishwa ofisini kwake na wananchi wa eneo la Uzunguni,inapopita barabara hiyo kufuatia adha ya vumbi wanayoipata wakati barabara hiyo inajengwa kwa kiwango cha lami.
Mwakipesile alisema kuwa hata yeye kiwango cha utengenezaji wa barabara hiyo kilimtia mashaka,hali iliyopelekea kumuagiza mtaalamu kutoka Wakala wa barabara nchini (TANROADS), mkoa wa Mbeya kwenda kuifanyia ukaguzi ili kuona kama imejengwa kwa kiwango.
"Mtaalam niliyemtuma kutoka TANROADS aliikagua barabara hiyo na kubaini kuwa imejengwa chini ya kiwango kinachotakiwa...hivyo naagiza kuwa mkandarasi huyo asilipwe fedha zilizobaki hadi tujiridhishe na kazi iliyofanyika" alisema Mwakipesile.
Aliongeza kuwa wakazi wa eneo la Uzunguni wamekuwa wanampelelekea malalamiko kutokana na adha ya vumbi linalotimka katika barabara hiyo ambayo ilitakiwa kujengwa kwa kiwango cha lami.
Agizo hilo limetolewa jana na Mkuu wa mkoa wa Mbeya,John Mwakipesile, kufuatia malalamiko yaliyofikishwa ofisini kwake na wananchi wa eneo la Uzunguni,inapopita barabara hiyo kufuatia adha ya vumbi wanayoipata wakati barabara hiyo inajengwa kwa kiwango cha lami.
Mwakipesile alisema kuwa hata yeye kiwango cha utengenezaji wa barabara hiyo kilimtia mashaka,hali iliyopelekea kumuagiza mtaalamu kutoka Wakala wa barabara nchini (TANROADS), mkoa wa Mbeya kwenda kuifanyia ukaguzi ili kuona kama imejengwa kwa kiwango.
"Mtaalam niliyemtuma kutoka TANROADS aliikagua barabara hiyo na kubaini kuwa imejengwa chini ya kiwango kinachotakiwa...hivyo naagiza kuwa mkandarasi huyo asilipwe fedha zilizobaki hadi tujiridhishe na kazi iliyofanyika" alisema Mwakipesile.
Aliongeza kuwa wakazi wa eneo la Uzunguni wamekuwa wanampelelekea malalamiko kutokana na adha ya vumbi linalotimka katika barabara hiyo ambayo ilitakiwa kujengwa kwa kiwango cha lami.
TANROADS MBEYA WAWEKWA KITI MOTO.
WAJUMBE wa kikao cha Bodi ya barabara mkoa wa Mbeya, wamemuagiza Wakala wa Barabara nchini (TANROADS),mkoa kuhakikisha kuwa bajeti ya barabara inayotakiwa kupitishwa inapitiwa kwanza na kikao hicho.
Imeelezwa kuwa TANROADS wamekuwa wanapitisha bajeti hiyo na kuamua wao barabara za kuzitengeneza badala ya zile zinazotakiwa na wananchi wa wilaya husika.
Wakichangia katika kikao cha Bodi ya Barabara kilichofanyika jana.chini ya Uenyekiti wa Mkuu wa mkoa wa Mbeya,wajumbe hao walisema kuwa barabara zinazotengenezwa na TANROADS zinatakiwa kujibu kero za wananchi na siyo nje ya hapo.
Walisema kuwa hivyo kuanzia bajeti ijayo ni lazima kabla ya kupitishwa iwe inaletwa kwenye kikao hicho kujadiriwa ili barabara zitakazotengenezwa ziwe ni zile zinazopewa kipaumbele na wananchi na siyo wakala huyo wa barabara.
“Ni vyema hili lifanyiwe kazi ili barabara zile zinazotakiwa na wananchi kutokana na umuhimu wake ndizo zipewe kipaumbele cha kwanza na siyo zile ambazo TANROADS mmekuwa mnaziamua na kuzipangia bajeti bila ya kutushirikisha” walisema.
Waliongeza kuwa mabadiliko hayo yasipofanyika ni wazi hadi tunaingia kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2010,barabara nyingi zitakuwa zimetengenezwa lakini zitakuwa hazijibu utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2005-2010.
Walisema haiwezekani TANROADS wawe wanaamua barabara zipi za kutengenezwa, kupanga bajeti na kisha kuileta kwenye kikao cha Bodi ya Barabara kwa ajili ya kuwasomea tu wajumbe,hali ambayo inakuwa haisadii.
“Tuachane na utaratibu huu uliopo hivi sasa kwani barabara hizi ni zetu na nyie TANROADS ni wakala tu wa kuzisimamia….kwani wananchi ndio wanaoamua barabara ipi itengenezwe kutokana na umuhimu wake na siyo nyie ndio muwe mnawaamulia” walisema.
Kufuatia hali hiyo,Mkuu wa mkoa Mwakipesile alikubaliana na hoja hizo za wajumbe na kuwa kuanzia sasa bajeti hiyo iwe inaletwa kwenye kikao hicho,kujadiriwa kabla ya kuanza kutekelezwa ili barabara zenye umuhimu kwa wananchi ndizo zipewe kipaumbele kikubwa cha kutengenezwa.
Imeelezwa kuwa TANROADS wamekuwa wanapitisha bajeti hiyo na kuamua wao barabara za kuzitengeneza badala ya zile zinazotakiwa na wananchi wa wilaya husika.
Wakichangia katika kikao cha Bodi ya Barabara kilichofanyika jana.chini ya Uenyekiti wa Mkuu wa mkoa wa Mbeya,wajumbe hao walisema kuwa barabara zinazotengenezwa na TANROADS zinatakiwa kujibu kero za wananchi na siyo nje ya hapo.
Walisema kuwa hivyo kuanzia bajeti ijayo ni lazima kabla ya kupitishwa iwe inaletwa kwenye kikao hicho kujadiriwa ili barabara zitakazotengenezwa ziwe ni zile zinazopewa kipaumbele na wananchi na siyo wakala huyo wa barabara.
“Ni vyema hili lifanyiwe kazi ili barabara zile zinazotakiwa na wananchi kutokana na umuhimu wake ndizo zipewe kipaumbele cha kwanza na siyo zile ambazo TANROADS mmekuwa mnaziamua na kuzipangia bajeti bila ya kutushirikisha” walisema.
Waliongeza kuwa mabadiliko hayo yasipofanyika ni wazi hadi tunaingia kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2010,barabara nyingi zitakuwa zimetengenezwa lakini zitakuwa hazijibu utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2005-2010.
Walisema haiwezekani TANROADS wawe wanaamua barabara zipi za kutengenezwa, kupanga bajeti na kisha kuileta kwenye kikao cha Bodi ya Barabara kwa ajili ya kuwasomea tu wajumbe,hali ambayo inakuwa haisadii.
“Tuachane na utaratibu huu uliopo hivi sasa kwani barabara hizi ni zetu na nyie TANROADS ni wakala tu wa kuzisimamia….kwani wananchi ndio wanaoamua barabara ipi itengenezwe kutokana na umuhimu wake na siyo nyie ndio muwe mnawaamulia” walisema.
Kufuatia hali hiyo,Mkuu wa mkoa Mwakipesile alikubaliana na hoja hizo za wajumbe na kuwa kuanzia sasa bajeti hiyo iwe inaletwa kwenye kikao hicho,kujadiriwa kabla ya kuanza kutekelezwa ili barabara zenye umuhimu kwa wananchi ndizo zipewe kipaumbele kikubwa cha kutengenezwa.
Thursday, May 28, 2009
ASKARI WA TANAPA AUAWA NA MWILI WAKE KUTUPWA MFEREJINI.
ASKARI wa Hifadhi ya Taifa (TANAPA), kambi ya Nyota wilayani Mbarali, mwenye cheo cha Staff Sajenti, Brighton Ng’umbi (57), ameuawa na watu wasiojulikana na maiti yake kutupwa katika mfereji wa maji.
Mwili wa marehemu Ng’umbi ambaye alipotea tangu Mei 23,mwaka huu saa 5:00 usiku, akitokea katika baa ya Oasis iliyopo Rujewa, ulikutwa katika mfereji huo unaosafirisha maji kwenye mashamba ya mpunga ya kampuni ya Highland Estate Ltd.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya, Zelothe Stephen, alisema mwili huo uliokotwa jana saa 2:00 asuubuhi ukiwa umetupwa katika mfereji huo.
Stephen alisema uchunguzi uliofanywa kwenye mwili wa marehemu Ng’umbi umeonyesha majeraha kwenye paji lake la uso na mdomoni.
“Polisi inamshikilia Rebecca Emmanuel (39), maarufu zaidi kwa jina la Mwakyami, mkazi wa kijiji cha Ihango, kwa tuhuma za kuhusika na kifo hicho” alisema Stephen.
Alifafanua kuwa mtuhumiwa Rebecca ametiwa mbaroni kwani ndiye alikuwa na marehemu siku ya mwisho kabla ya kutoweka wakiwa wanakunywa vinywaji katika baa hiyo ya Oasis, hivyo anaisadia polisi.
Alisema uchunguzi zaidi ili kuwabaini watuhumiwa waliohusika na mauaji ya askari huyo wa doria wa TANAPA (Park Ranger), unaendelea kufanywa na polisi.
Mwili wa marehemu Ng’umbi ambaye alipotea tangu Mei 23,mwaka huu saa 5:00 usiku, akitokea katika baa ya Oasis iliyopo Rujewa, ulikutwa katika mfereji huo unaosafirisha maji kwenye mashamba ya mpunga ya kampuni ya Highland Estate Ltd.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya, Zelothe Stephen, alisema mwili huo uliokotwa jana saa 2:00 asuubuhi ukiwa umetupwa katika mfereji huo.
Stephen alisema uchunguzi uliofanywa kwenye mwili wa marehemu Ng’umbi umeonyesha majeraha kwenye paji lake la uso na mdomoni.
“Polisi inamshikilia Rebecca Emmanuel (39), maarufu zaidi kwa jina la Mwakyami, mkazi wa kijiji cha Ihango, kwa tuhuma za kuhusika na kifo hicho” alisema Stephen.
Alifafanua kuwa mtuhumiwa Rebecca ametiwa mbaroni kwani ndiye alikuwa na marehemu siku ya mwisho kabla ya kutoweka wakiwa wanakunywa vinywaji katika baa hiyo ya Oasis, hivyo anaisadia polisi.
Alisema uchunguzi zaidi ili kuwabaini watuhumiwa waliohusika na mauaji ya askari huyo wa doria wa TANAPA (Park Ranger), unaendelea kufanywa na polisi.
Wednesday, May 27, 2009
MAUAJI MFYULULIZO YA WANAWAKE YATINGISHA MJI WA MABATINI, JIJINI MBEYA
WIMBI la mauaji ya kinyama ya wanawake, katika eneo la Mabatini jijini Mbeya, linaelekea kuota mizizi, kufuatia mwanamke mwingine kuuawa kikatili kwa kupigwa na kitu kizito kichwani.
Katika tukio hilo, wanawake wengine wawili ambao ni ndugu wa marehemu walijeruhiwa vibaya maeneo ya kichwani na wanaendelea kupata matibabu hospitali ya Rufani Mbeya.
Marehemu ametajwa kuwa ni Vena Kasokela (25), wakati waliojeruhiwa wakitajwa kuwa Emmy (46) na Lydia John (58).
Hivi karibuni mwanamke mjamzito, Jacquliene Mwasunga (18), aliuawa kikatili eneo hilo hilo huku mtoto wa dada ake, ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha pili sekondari ya Legico, Upendo Mwasunga (16), akijeruhiwa kichwani na kukatwa sikio lake kushoto.
Akithibitisha kutokea kwa tukio la kinyama, Kamanda wa polisi mkoani Mbeya, Zelothe Stephen, alisema lilitokea juzi saa 12:00 asubuhi, baada ya watu wasiofahamika kuivamia nyumba hiyo.
Akifafanua, Stephen alisema kuwa marehemu Vena na majeruhi Emmy, walikuwa ni wageni waliokuwa wamefikia kwa mwenyeji wao Lydia ambaye ni mfanyabiashara wa pombe za kienyeji katika klabu moja iliyopo eneo hilo.
"Mara baada ya kuvamiwa, wanawake wote watatu walianza kupigwa maeneo ya kichwani na kitu kizito, na kusababisha majeraha ambapo wote walikimbizwa hospitali ya Rufani Mbeya kwa matibabu" alisema Stephen.
Aliongeza kuwa ilipofika saa 4:00 asubuhi, zilipatikana taarifa kuwa mmoja wa majeruhi, Vena Kasokela, amefariki dunia wakati akiendelea kupatiwa matibabu ili kuokoa maisha yake.
Stephen alisema:"Taarifa za awali kuhusu chanzo cha mauaji haya, zinaonyesha kuwa huenda tukio hili ni la ulipizaji kisasi, kwani majeruhi Emmy alikuwa ameolewa na ameachika hivi karibuni".
Alisema kuwa polisi wanachukulia mauaji hayo kama ni ya kulipiza kisasi, kwani watuhumiwa wa mauaji hao hawakuchukua kitu chochote kutoka nyumba hiyo, hali ambayo ingeashiria kuwa walikuwa ni majambazi wa kawaida.
Aliongeza kuwa kikosi cha upelelezi cha jeshi hilo, kimepelekwa eneo la Mabatini kwa ajili ya kuendelea na uchunguzi zaidi kuhusu tukio hilo la kinyama.
Alisema hivyo polisi wanaendelea na uchunguzi wa matukio yote mawili,aliyoyata kuwa ni kujeruhi na mauaji kwani wana uhakika kuwa wakifanikiwa kuwakamata watuhumiwa basi ni wazi ndio watakuwa wameshiriki katika matukio yote mawili.
Lakini wananchi wa eneo la Mabatini waliozungumza na gazeti hili, kwa nyakati tofauti, wamelitupia lawama jeshi la polisi mkoa kwani hadi leo halijafanikiwa kuwatia mbaroni watuhumiwa wa mauaji ya mwanamke mjamzito, Jacquliene.
Waliongeza kuwa hali ya usalama iliyopo hivi sasa maeneo hayo, hasa kwa wanawake inawatia hofu kwani matukio yote mawili ya mauaji hayo ya mfululizo, yamekuwa yakitokea saa za asubuhi.
"Tunaomba jeshi la polisi lifanye kazi zake kwa ufanisi ili kuweza kuwatia mbaroni watuhumiwa hawa wa mauaji yanayotokea mfululizo... kwa kweli hivi sasa tunaishi kwa maashaka hatujui kesho itakuwa zamu ya nani" walisema.
Katika tukio hilo, wanawake wengine wawili ambao ni ndugu wa marehemu walijeruhiwa vibaya maeneo ya kichwani na wanaendelea kupata matibabu hospitali ya Rufani Mbeya.
Marehemu ametajwa kuwa ni Vena Kasokela (25), wakati waliojeruhiwa wakitajwa kuwa Emmy (46) na Lydia John (58).
Hivi karibuni mwanamke mjamzito, Jacquliene Mwasunga (18), aliuawa kikatili eneo hilo hilo huku mtoto wa dada ake, ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha pili sekondari ya Legico, Upendo Mwasunga (16), akijeruhiwa kichwani na kukatwa sikio lake kushoto.
Akithibitisha kutokea kwa tukio la kinyama, Kamanda wa polisi mkoani Mbeya, Zelothe Stephen, alisema lilitokea juzi saa 12:00 asubuhi, baada ya watu wasiofahamika kuivamia nyumba hiyo.
Akifafanua, Stephen alisema kuwa marehemu Vena na majeruhi Emmy, walikuwa ni wageni waliokuwa wamefikia kwa mwenyeji wao Lydia ambaye ni mfanyabiashara wa pombe za kienyeji katika klabu moja iliyopo eneo hilo.
"Mara baada ya kuvamiwa, wanawake wote watatu walianza kupigwa maeneo ya kichwani na kitu kizito, na kusababisha majeraha ambapo wote walikimbizwa hospitali ya Rufani Mbeya kwa matibabu" alisema Stephen.
Aliongeza kuwa ilipofika saa 4:00 asubuhi, zilipatikana taarifa kuwa mmoja wa majeruhi, Vena Kasokela, amefariki dunia wakati akiendelea kupatiwa matibabu ili kuokoa maisha yake.
Stephen alisema:"Taarifa za awali kuhusu chanzo cha mauaji haya, zinaonyesha kuwa huenda tukio hili ni la ulipizaji kisasi, kwani majeruhi Emmy alikuwa ameolewa na ameachika hivi karibuni".
Alisema kuwa polisi wanachukulia mauaji hayo kama ni ya kulipiza kisasi, kwani watuhumiwa wa mauaji hao hawakuchukua kitu chochote kutoka nyumba hiyo, hali ambayo ingeashiria kuwa walikuwa ni majambazi wa kawaida.
Aliongeza kuwa kikosi cha upelelezi cha jeshi hilo, kimepelekwa eneo la Mabatini kwa ajili ya kuendelea na uchunguzi zaidi kuhusu tukio hilo la kinyama.
Alisema hivyo polisi wanaendelea na uchunguzi wa matukio yote mawili,aliyoyata kuwa ni kujeruhi na mauaji kwani wana uhakika kuwa wakifanikiwa kuwakamata watuhumiwa basi ni wazi ndio watakuwa wameshiriki katika matukio yote mawili.
Lakini wananchi wa eneo la Mabatini waliozungumza na gazeti hili, kwa nyakati tofauti, wamelitupia lawama jeshi la polisi mkoa kwani hadi leo halijafanikiwa kuwatia mbaroni watuhumiwa wa mauaji ya mwanamke mjamzito, Jacquliene.
Waliongeza kuwa hali ya usalama iliyopo hivi sasa maeneo hayo, hasa kwa wanawake inawatia hofu kwani matukio yote mawili ya mauaji hayo ya mfululizo, yamekuwa yakitokea saa za asubuhi.
"Tunaomba jeshi la polisi lifanye kazi zake kwa ufanisi ili kuweza kuwatia mbaroni watuhumiwa hawa wa mauaji yanayotokea mfululizo... kwa kweli hivi sasa tunaishi kwa maashaka hatujui kesho itakuwa zamu ya nani" walisema.
Tuesday, May 26, 2009
VIMBWANGA MICHEZONI
UTAFITI ZIWA NGOSI.
MBEYA NA UTALII- ZIARA YA ZIWA NGOSI
MBUNGE MPESYA AMSHUKIA MKURUGENZI WA JIJI LA MBEYA.
MBUNGE wa jimbo la Mbeya mjini (CCM), Benson Mpesya, amesema kuwa maazimio yanayotolewa na baraza la madiwani yasiposimamiwa na kutekelezwa, anayepaswa kuwajibika ni Mkurugenzi na siyo vinginevyo.
Alisema kuwa Mkurugenzi wa halmashauri ya jiji la Mbeya,Elizabeth Munuo, ndiye anatakiwa awapange watendaji wake na kuwaelekeza kitu gani kinatakiwa kifanywe ndani ya jiji na siyo madiwani.
Mpesya aliyasema hayo wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari, waliotaka kupata ufafanuzi wa masuala mbalimbali, likiwemo suala la kukithiri kwa uchafu ndani ya jiji la Mbeya.
"Kazi ya madiwani ni kusimamia yale maazimio ili yatekelezwe...sasa maazimio yanapotolewa na baraza la madiwani yasipotekelezwa, mwenye matatizo hapo kwa mujibu wa kanuni na taratibu zetu ni yule anayetakiwa kuyasimamia maazimio" alisema Mpesya.
Aliongeza kuwa kazi ya madiwani ni kuamua, na kuadhimia kuwa kuanzia sasa wanataka takataka za mahali fulani ziondolewe, ama yanunuliwe magari kwa ajili ya kuzoa takataka, na mtekelezaji mkuu ni kiongozi wa kiserikali ambaye ni Mkurugenzi.
Mbunge huyo alisema hivyo ni vyema waandishi wa habari, wangekuwa wanahoji iwapo yale maazimo yanayoamuliwa na baraza la madiwani yanatekelezwa, ama la na ndipo wangejua ni nani wa kumkamata ili atoe ufafanuzi sahihi.
Mpesya alisema:"Na nyinyi ndugu zangu waandishi wa habari, ni figa la nne licha ya kuwa halipo ndani ya katiba...mimi ni miongoni mwa wabunge ambao nawakiri kabisa kuwa kazi yenu ya kuielimisha jamii ni nzuri".
Aliongeza kuwa hivyo waandishi wa habari wanatakiwa kujenga na kuwafanya viongozi wawe wamoja badala ya kuwabomoa, kwani wao ni figa halali lakini wakati mwingine hawaifanyi kazi hiyo kwani wanawasukuma mno wanasiasa katika kutekeleza majukumu.
Alisema ni vyema kukiwa na tatizo, basi kitafutwe kiini cha tatizo,na sityo kurusha rusha tu mambo bali wajue tatizo lipo wapi.
Katika hatua nyingine, Mpesya alithibitisha kuwa atakuwa ni mmoja wa wana-CCM watakaojitokeza kuwania nafasi hiyo ya ubunge katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2010.
Alisema zipo habari zinazoenezwa mitaani kuwa hatagombea ubunge mwakani, na aliwachekesha waandishi aliposema kuwa yeye atapata wapi nafasi ya kusema kuwa atatetea nafasi hiyo kama siyo kupitia vyombo vya habari.
"Na mimi natoa mapema azimio langu kuwa nitajitokeza tena katika uchaguzi mkuu ujao ili kutetea nafasi ya ubunge wa jimbo hili, hivyo wale wengine wenye nia nao wajipime ubavu...kwa kazi nilizozifanya katika kuteleleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM, ninao uhakika kuwa nitapata kura nyingi" alisema Mpesya.
Alisema kuwa Mkurugenzi wa halmashauri ya jiji la Mbeya,Elizabeth Munuo, ndiye anatakiwa awapange watendaji wake na kuwaelekeza kitu gani kinatakiwa kifanywe ndani ya jiji na siyo madiwani.
Mpesya aliyasema hayo wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari, waliotaka kupata ufafanuzi wa masuala mbalimbali, likiwemo suala la kukithiri kwa uchafu ndani ya jiji la Mbeya.
"Kazi ya madiwani ni kusimamia yale maazimio ili yatekelezwe...sasa maazimio yanapotolewa na baraza la madiwani yasipotekelezwa, mwenye matatizo hapo kwa mujibu wa kanuni na taratibu zetu ni yule anayetakiwa kuyasimamia maazimio" alisema Mpesya.
Aliongeza kuwa kazi ya madiwani ni kuamua, na kuadhimia kuwa kuanzia sasa wanataka takataka za mahali fulani ziondolewe, ama yanunuliwe magari kwa ajili ya kuzoa takataka, na mtekelezaji mkuu ni kiongozi wa kiserikali ambaye ni Mkurugenzi.
Mbunge huyo alisema hivyo ni vyema waandishi wa habari, wangekuwa wanahoji iwapo yale maazimo yanayoamuliwa na baraza la madiwani yanatekelezwa, ama la na ndipo wangejua ni nani wa kumkamata ili atoe ufafanuzi sahihi.
Mpesya alisema:"Na nyinyi ndugu zangu waandishi wa habari, ni figa la nne licha ya kuwa halipo ndani ya katiba...mimi ni miongoni mwa wabunge ambao nawakiri kabisa kuwa kazi yenu ya kuielimisha jamii ni nzuri".
Aliongeza kuwa hivyo waandishi wa habari wanatakiwa kujenga na kuwafanya viongozi wawe wamoja badala ya kuwabomoa, kwani wao ni figa halali lakini wakati mwingine hawaifanyi kazi hiyo kwani wanawasukuma mno wanasiasa katika kutekeleza majukumu.
Alisema ni vyema kukiwa na tatizo, basi kitafutwe kiini cha tatizo,na sityo kurusha rusha tu mambo bali wajue tatizo lipo wapi.
Katika hatua nyingine, Mpesya alithibitisha kuwa atakuwa ni mmoja wa wana-CCM watakaojitokeza kuwania nafasi hiyo ya ubunge katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2010.
Alisema zipo habari zinazoenezwa mitaani kuwa hatagombea ubunge mwakani, na aliwachekesha waandishi aliposema kuwa yeye atapata wapi nafasi ya kusema kuwa atatetea nafasi hiyo kama siyo kupitia vyombo vya habari.
"Na mimi natoa mapema azimio langu kuwa nitajitokeza tena katika uchaguzi mkuu ujao ili kutetea nafasi ya ubunge wa jimbo hili, hivyo wale wengine wenye nia nao wajipime ubavu...kwa kazi nilizozifanya katika kuteleleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM, ninao uhakika kuwa nitapata kura nyingi" alisema Mpesya.
BENKI YA DUNIA YASAIDIA SH.BILIONI 21 UJENZI WA BARABARA JIJI LA MBEYA
BARABARA zenye urefu wa kilometa 30, zinatarajiwa kujengwa kwa kiwango cha lami, katika halmashauri ya jiji la Mbeya, baada ya jiji hilo kuingizwa katika mpango wa Benki ya Dunia (WB), wa kuboresha miundombinu.
Sambamba na hilo, benki ya Dunia kupitia mradi huo ilikubaliana na jiji la Mbeya, kuiongezea uwezo wa kukusanya mapato yake yenyewe.Gharama za mradi wote zinatarajiwa kuwa shilingi bilioni 21.
Kaimu Mhandisi wa jiji la Mbeya, Masalu Bashiganye, akizungumza na mwandishi wa habari hizi, alisema kuwa mwishoni mwa mwaka uliopita, jiji lilibahatika kuingizwa kwenye mpango wa benki ya Dunia wa kuboresha miuondombinu yake.
Alisema kuwa mradi huo utahusisha ujenzi wa barabara, kwa kiwango cha lami katika stendi ya Nanenane na pia kuboresha usafi, kwa kununua magari kwa ajili ya kuzolea takataka.
"Utekelezaji wa mradi huu utachukua muda wa miaka mitatu na utafanyika katika awamu mbili tofauti kuanzia mwezi Machi,mwakani" alisema Bashiganye.
Aliongeza kuwa hivi sasa jiji la Mbeya, linaendelea na michakatoi mbalimbali kwa kushirikiana na Wizara ya TAMISEMI na Benki ya Dunia, ili kuwapata Makandarasi washauri.
Bashiganye alisema Makandarasi hao ndio watakuwa na kazi ya kubuni ama kussanifu miundombinu hiyo na kutengeneza nyaraka za zabuni ambazo ndizo zitatumika kuwapata makandarasi wa kujenga miundombinu hiyo.
Kaimu Mhandisi alisema mchakato huo unaendelea na unatarajia kukamilika mapema mwakani na halmashauri katika mradi huo itachangia wataalamu wa usimamizi katika ujenzi kwa maeneo mbalimbali.
Aliwataja wataalamu hao kuwa ni kutoka idara mbalimbali zikiwemo ya Ujenzi, Afya, Utumishi, Fedha na uthamini wa mali na ile ya Maendeleo ya Jamii.
Pia Kitengo cha Uthamini kitashirikishwa katika kuthamini nyumba mbalimbali za jiji la Mbeya, ambazo bado hazijafanyiwa uthamini ili zianze kulipiwa kodi ya majengo.
Sambamba na hilo, benki ya Dunia kupitia mradi huo ilikubaliana na jiji la Mbeya, kuiongezea uwezo wa kukusanya mapato yake yenyewe.Gharama za mradi wote zinatarajiwa kuwa shilingi bilioni 21.
Kaimu Mhandisi wa jiji la Mbeya, Masalu Bashiganye, akizungumza na mwandishi wa habari hizi, alisema kuwa mwishoni mwa mwaka uliopita, jiji lilibahatika kuingizwa kwenye mpango wa benki ya Dunia wa kuboresha miuondombinu yake.
Alisema kuwa mradi huo utahusisha ujenzi wa barabara, kwa kiwango cha lami katika stendi ya Nanenane na pia kuboresha usafi, kwa kununua magari kwa ajili ya kuzolea takataka.
"Utekelezaji wa mradi huu utachukua muda wa miaka mitatu na utafanyika katika awamu mbili tofauti kuanzia mwezi Machi,mwakani" alisema Bashiganye.
Aliongeza kuwa hivi sasa jiji la Mbeya, linaendelea na michakatoi mbalimbali kwa kushirikiana na Wizara ya TAMISEMI na Benki ya Dunia, ili kuwapata Makandarasi washauri.
Bashiganye alisema Makandarasi hao ndio watakuwa na kazi ya kubuni ama kussanifu miundombinu hiyo na kutengeneza nyaraka za zabuni ambazo ndizo zitatumika kuwapata makandarasi wa kujenga miundombinu hiyo.
Kaimu Mhandisi alisema mchakato huo unaendelea na unatarajia kukamilika mapema mwakani na halmashauri katika mradi huo itachangia wataalamu wa usimamizi katika ujenzi kwa maeneo mbalimbali.
Aliwataja wataalamu hao kuwa ni kutoka idara mbalimbali zikiwemo ya Ujenzi, Afya, Utumishi, Fedha na uthamini wa mali na ile ya Maendeleo ya Jamii.
Pia Kitengo cha Uthamini kitashirikishwa katika kuthamini nyumba mbalimbali za jiji la Mbeya, ambazo bado hazijafanyiwa uthamini ili zianze kulipiwa kodi ya majengo.
KAMISHNA WA TUME YA HAKI ZA BINADAMU
wa sekondari kutoka mkoani Kigoma, aliyeuawa hivi karibuni wilayani Mbarali mkoa wa Mbeya.
KAPUNGA AKITANGAZWA MSHINDI.
JAJI MKUU MSTAAFU BARNABAS SAMATTA
MEYA WA JIJI LA MBEYA ACHAGULIWA KUWA KATIBU MUENEZI CCM
MEYA wa halmashauri ya jiji la Mbeya, Athanas Kapunga, amechaguliwa kwa kishindo kuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi, wilaya ya Mbeya mjini baada ya kuwabwaga wagombea wengine wawili walijitokeza.
Kapunga alishinda nafasi hiyo kwa kupata kura 122 na kuwashinda wapinzani wake, Sure Mwasanguti aliyepata kura 60 huku Mwajuma Tindwa, ambaye alikuwepo nje ya ukumbi na kuingia 'mitini' dakika za mwisho akiambulia kura 3.
Katika uchaguzi huo uliofanyika katika ukumbi wa shule ya sekondari iliyo chini ya Jumuia ya Wazazi ya CCM, Sangu iliyopo mjini hapa,ulihudhuriwa na wajumbe 187 wa halmashauri Kuu ya CCM wilaya hiyo.
Msimamizi mkuu wa uchaguzi huo, Ernest Machunda, alipowataka wajumbe kufanya zoezi kla kuhakiki> wajumbe halali wa mkutano huo.
Katika hali ya kushangaza, wajumbe kutoka kata ya Mwasanga, walilazimika kupitishwa mbele ili kuhakikiwa ambapo ilibainika mjumbe mmoja, Amani Salone, ambaye alijitambulisha kama Kaimu Mwenyekiti wa CCM Kata hiyo, kubainika kuwa siyo mjumbe.
Machunda alilazimika kumtoa nje Salone na ndipo wagombea walipoanza kujieleza akianza Kapunga, Mwasanaguti na Katibu wa CCM wilaya, Bahati Makalanzi, alilazimika kusimama na kumuombea kura Mwajuma.
Akiomba kura Kapunga aliwaomba wajumbe kumchagua kushika nafasi hiyo kwani anao uzoefu na nafasi hiyo ambayo alisema aliwahi kuiongoza katika vuipindi tofauti.
"Nimeifanya kazi hii ya Uenezi katika kvipindi viwili tofauti na nilifanikiwa kwa kushirikiana na wana-CCM wilaya hii, kuweza kulirudisha jimbo hili ambalo lilikuwa linashikiliwa na Polisya Mwaisyeje wa chama cha upinzani cha> NCCR-Mageuzi.
Mara baada ya matokeo kutangazwa na Kapunga, kupatikana mshindi, ukumbi ulilipuka kwa shangwe na kuimba nyimbo za Chama, hali iliyoashiria kuwa wajumbe waliridhika na matokeo hayo.
Kwa upande wake Mwasanguti aliwashukuru wajumbe wa kikao hicho kwa kupata kura 60, na kuongeza kuwa hizo si haba kwani hiyo ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuomba kura kwa wajumbe wa kikao hicho.
Awali Mwasanguti alikuwa ni Mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya Mbeya mjini, na alistaafu baada ya umri wake kutomruhusu kugombea tena kwa kipindi kingine cha miaka mitano.
0000
Kapunga alishinda nafasi hiyo kwa kupata kura 122 na kuwashinda wapinzani wake, Sure Mwasanguti aliyepata kura 60 huku Mwajuma Tindwa, ambaye alikuwepo nje ya ukumbi na kuingia 'mitini' dakika za mwisho akiambulia kura 3.
Katika uchaguzi huo uliofanyika katika ukumbi wa shule ya sekondari iliyo chini ya Jumuia ya Wazazi ya CCM, Sangu iliyopo mjini hapa,ulihudhuriwa na wajumbe 187 wa halmashauri Kuu ya CCM wilaya hiyo.
Msimamizi mkuu wa uchaguzi huo, Ernest Machunda, alipowataka wajumbe kufanya zoezi kla kuhakiki> wajumbe halali wa mkutano huo.
Katika hali ya kushangaza, wajumbe kutoka kata ya Mwasanga, walilazimika kupitishwa mbele ili kuhakikiwa ambapo ilibainika mjumbe mmoja, Amani Salone, ambaye alijitambulisha kama Kaimu Mwenyekiti wa CCM Kata hiyo, kubainika kuwa siyo mjumbe.
Machunda alilazimika kumtoa nje Salone na ndipo wagombea walipoanza kujieleza akianza Kapunga, Mwasanaguti na Katibu wa CCM wilaya, Bahati Makalanzi, alilazimika kusimama na kumuombea kura Mwajuma.
Akiomba kura Kapunga aliwaomba wajumbe kumchagua kushika nafasi hiyo kwani anao uzoefu na nafasi hiyo ambayo alisema aliwahi kuiongoza katika vuipindi tofauti.
"Nimeifanya kazi hii ya Uenezi katika kvipindi viwili tofauti na nilifanikiwa kwa kushirikiana na wana-CCM wilaya hii, kuweza kulirudisha jimbo hili ambalo lilikuwa linashikiliwa na Polisya Mwaisyeje wa chama cha upinzani cha> NCCR-Mageuzi.
Mara baada ya matokeo kutangazwa na Kapunga, kupatikana mshindi, ukumbi ulilipuka kwa shangwe na kuimba nyimbo za Chama, hali iliyoashiria kuwa wajumbe waliridhika na matokeo hayo.
Kwa upande wake Mwasanguti aliwashukuru wajumbe wa kikao hicho kwa kupata kura 60, na kuongeza kuwa hizo si haba kwani hiyo ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuomba kura kwa wajumbe wa kikao hicho.
Awali Mwasanguti alikuwa ni Mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya Mbeya mjini, na alistaafu baada ya umri wake kutomruhusu kugombea tena kwa kipindi kingine cha miaka mitano.
0000
TUME YA HAKI ZA BINADAMU YAPONDA HUKUMU...
TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, imesema kuwa kuachiwa huru kwa watuhumiwa watatu, raia wenye asili ya kiasia waliokuwa wanatuhumiwa kwa mauaji ya mwanafunzi Swaibu Omary, kumegubikwa na harufu ya rushwa.
Kamishna wa Tume hiyo, Bernadeta Gambishi, aliyasema hayo katika mkutano wa hadhara wakati akizungumza na wananchi wa eneo la Mwanjelwa, jijini Mbeya kuelezea kazi ya Tume hiyo kwa wananchi.Alikuwa akijibu swali la mmoja wa wananchiu aliyetaka kujua Tume hiyo ina mtazamo gani kuhusu hukumu hiyo.
Tume hiyo ipo mkoani hapa akitokea mkoa jirani wa Iringa, kwa ajili ya kukagua hali za magereza nchini baada ya kufanya ziara mnamo mwaka 2006/07, hivyo inatembelea tena kuona kama kile walishoishauri serikali kuhusu hali za magereza kimetekelezwa.
"Haiwezekani watuhumiwa hao watatu waachiwe baada ya kusota jela kwa muda wa mwezi mmoja...kuachiwa huku kunaonyesha kuna mazingira makubwa ya rushwa.Tukifanikiwa kukutana na ndugu wa marehemu tutawashauri ili wakate rufaa kwa ajili ya kufungua upya kesi hii ili haki itendeke" alisema Bernadeta.
Watuhumiwa hao ndugu kutoka familia moja ni Samir Muzrai, Faizy Abdulrasul na Hassan Abdul.
Kuachiwa kwa wapakistani hao kwa kipindi kifupi ambao walikamatwa April 6, mwaka huu kumezua maswali mengi kutoka kwa wananchi wa wilaya ya Mbarali ambao wanahoji kwa nini kesi nyingine za mauji watuhumiwa wamekuwa wakiwekwa mahabusu kwa muda mrefu wa zaidi ya miaka miwili bila kesi zao kuanza kusikilizwa.
Wananchi wamelitupia lawama jeshi la polisi mkoani hapa, kuwa linajenga matabaka katika kupeleleza kesi za mauaji kutokana na watu wenye kipato kikubwa upelelezi wao kufanyika haraka huku maskini wakisota kwa muda mrefu mahabusu.
Naye Wakili wa Serikali Mkoa wa Mbeya, Ayoub Mwenda, akizungumza na waandishi wa habari, alithibitisha kuachiwa hutu kwa watuhumiwa hao baada ya ofisi yake kujiridhisha na maelezo ya upelelezi uliofanywa na polisi pamoja na vipimo vya daktari aliyeufanyia uchunguzi mwili wa marehemu.
Mwenda alisema kwa mujibu wa upelelezi uliofanywa na polisi kutokana na tukio hilo ni kwamba mwanafunzi huyo alifariki dunia kwa kuumia baada ya kuruka kutoka juu ya gari na hivyo kusababisha kuumia vibaya kichwani.
Aliongeza kuwa daktari aliyeufanyia uchunguzi mwili wa marehemu alieleza kuwa mwanafunzi huyo alifariki kwa kuumia na siyo kwa kipigo kama ilivyodaiwa awali hivyo kutokana na maelezo ya polisi na daktari, serikali imeamua kuwafutia shitaka baada ya kubaini kuwa watuhumiwa hawakuhusika na mauji ya mwanafunzi huyo.
"Pamoja na watuhumiwa hao kuachiwa huru iwapo watajitokeza watu wengine wakatoa ushahidi wa kudhibitisha kuwa raia hao wa Pakistani walimuua mwanafunzi huyo watuhumiwa hao wanaweza wakakamatwa tena na shauri lao likaanza kupitiwa upya" alisema Mwenda.
Kwa upande wake Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Mbarali, Mustaphir Siyani, alisema watuhimiwa hao wameachiwa huru Mei 18 mwaka huu baada ya kubainika kuwa hakuna ushahidi wa kutosha wa kesi hiyo kutokana na upelelezi uliofanywa na polisi na kuupeleka kwa wakili wa serikali.
Alisema hata hivyo iwapo kutapatikana ushahidi wa kutosha jamuhuri ina uwezo wa kuwakamata watuhumiwa na kuwafunguliwa upya shitaka kutokana na kifungu cha 91 cha sheria ya makosa ya mauaji.
Awali jeshi la polisi Mkoani Mbeya lilieleza kuwa watuhumiwa hao walikamatwa kwa kutuhumiwa kuumua mwanafunzi wa shule ya sekondari ya mkoani Kigoma baada ya kumkuta akiiba matunda aina ya mapera shambani mwao April 6 mwaka huu.
0000
Kamishna wa Tume hiyo, Bernadeta Gambishi, aliyasema hayo katika mkutano wa hadhara wakati akizungumza na wananchi wa eneo la Mwanjelwa, jijini Mbeya kuelezea kazi ya Tume hiyo kwa wananchi.Alikuwa akijibu swali la mmoja wa wananchiu aliyetaka kujua Tume hiyo ina mtazamo gani kuhusu hukumu hiyo.
Tume hiyo ipo mkoani hapa akitokea mkoa jirani wa Iringa, kwa ajili ya kukagua hali za magereza nchini baada ya kufanya ziara mnamo mwaka 2006/07, hivyo inatembelea tena kuona kama kile walishoishauri serikali kuhusu hali za magereza kimetekelezwa.
"Haiwezekani watuhumiwa hao watatu waachiwe baada ya kusota jela kwa muda wa mwezi mmoja...kuachiwa huku kunaonyesha kuna mazingira makubwa ya rushwa.Tukifanikiwa kukutana na ndugu wa marehemu tutawashauri ili wakate rufaa kwa ajili ya kufungua upya kesi hii ili haki itendeke" alisema Bernadeta.
Watuhumiwa hao ndugu kutoka familia moja ni Samir Muzrai, Faizy Abdulrasul na Hassan Abdul.
Kuachiwa kwa wapakistani hao kwa kipindi kifupi ambao walikamatwa April 6, mwaka huu kumezua maswali mengi kutoka kwa wananchi wa wilaya ya Mbarali ambao wanahoji kwa nini kesi nyingine za mauji watuhumiwa wamekuwa wakiwekwa mahabusu kwa muda mrefu wa zaidi ya miaka miwili bila kesi zao kuanza kusikilizwa.
Wananchi wamelitupia lawama jeshi la polisi mkoani hapa, kuwa linajenga matabaka katika kupeleleza kesi za mauaji kutokana na watu wenye kipato kikubwa upelelezi wao kufanyika haraka huku maskini wakisota kwa muda mrefu mahabusu.
Naye Wakili wa Serikali Mkoa wa Mbeya, Ayoub Mwenda, akizungumza na waandishi wa habari, alithibitisha kuachiwa hutu kwa watuhumiwa hao baada ya ofisi yake kujiridhisha na maelezo ya upelelezi uliofanywa na polisi pamoja na vipimo vya daktari aliyeufanyia uchunguzi mwili wa marehemu.
Mwenda alisema kwa mujibu wa upelelezi uliofanywa na polisi kutokana na tukio hilo ni kwamba mwanafunzi huyo alifariki dunia kwa kuumia baada ya kuruka kutoka juu ya gari na hivyo kusababisha kuumia vibaya kichwani.
Aliongeza kuwa daktari aliyeufanyia uchunguzi mwili wa marehemu alieleza kuwa mwanafunzi huyo alifariki kwa kuumia na siyo kwa kipigo kama ilivyodaiwa awali hivyo kutokana na maelezo ya polisi na daktari, serikali imeamua kuwafutia shitaka baada ya kubaini kuwa watuhumiwa hawakuhusika na mauji ya mwanafunzi huyo.
"Pamoja na watuhumiwa hao kuachiwa huru iwapo watajitokeza watu wengine wakatoa ushahidi wa kudhibitisha kuwa raia hao wa Pakistani walimuua mwanafunzi huyo watuhumiwa hao wanaweza wakakamatwa tena na shauri lao likaanza kupitiwa upya" alisema Mwenda.
Kwa upande wake Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Mbarali, Mustaphir Siyani, alisema watuhimiwa hao wameachiwa huru Mei 18 mwaka huu baada ya kubainika kuwa hakuna ushahidi wa kutosha wa kesi hiyo kutokana na upelelezi uliofanywa na polisi na kuupeleka kwa wakili wa serikali.
Alisema hata hivyo iwapo kutapatikana ushahidi wa kutosha jamuhuri ina uwezo wa kuwakamata watuhumiwa na kuwafunguliwa upya shitaka kutokana na kifungu cha 91 cha sheria ya makosa ya mauaji.
Awali jeshi la polisi Mkoani Mbeya lilieleza kuwa watuhumiwa hao walikamatwa kwa kutuhumiwa kuumua mwanafunzi wa shule ya sekondari ya mkoani Kigoma baada ya kumkuta akiiba matunda aina ya mapera shambani mwao April 6 mwaka huu.
0000
Thursday, May 21, 2009
JAMAA AKIJIHAMI KUUMWA NA NYUKI KWA KUTIMUA VUMBI.
MBUNGE THOMAS MWANG'ONDA
MBIO ZA MWENGE WA UHURU NA SHUGHULI ZA MAENDELEO.
WAREMBO WAKIWA KATIKA POZI
JOSE CHAMELION AKIPAGAWISHA WAKAZI WA JIJI LA MBEYA - 3.
JOSE CHAMELION AKIPAGAWISHA WAKAZI WA JIJI LA MBEYA - 2.
Subscribe to:
Posts (Atom)