MTU mmoja anayetuhumiwa kuwa jambazi, ameuawa kwa kupigwa na baadaye kuchomwa moto na wananchi wenye hasira kali wa mji mdogo wa Mlowo, wilayani Mbozi.
Tukio hilo lilitokea jana saa 11;00 alfajiri baada ya jambazi huyo akiwa na mwenzake mmoja aliyefanikiwa kukimbia, kukurupushwa eneo la darajani na sungusungu waliokuwa doria.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana, wakazi wa mji huo walisema kuwa Sungusungu hao wakiwa doria waliwakuta watuhumiwa hao wawili wakiwa na nondo pamoja na mapanga, hali iliyoonyesha kuwa walikuwa wakienda kufanya uharifu.
Walisema mara baada ya kukurupushwa, mmoja alifanikiwa kukimbia na kumuacha mwenzake ambaye alipata kipigo kikali hadi kupoteza fahamu ambapo waliwaacha baadhi ya sungusungu wakimlinda na wengine kuendelea kumtafuta aliyekimbia.
“Mmoja wa watuhumiwa hao alifanikiwa kukimbia na ilidaiwa kuwa amejificha katika nyumba ya kulala wageni iitwayo Altimalta iliyopo Mlowo.Viongozi wa serikali ya mtaa walilazimika kuwaomba wananchi waliokuwa wamejitokeza kuondoka eneo hilo lakini ilishindikana” walisema.
Kufuatia hali hiyo baadhi ya raia wema walikimbilia kituo kidogo cha polisi Mlowo na kutoa taarifa ambapo walifika katika nyumba hiyo ya kulala wageni na kuwataka wananchi kuondoka lakini waliendelea kukaidi amri hali iliyowalazimisha polisi kutumia mabomu ya machozi kuwatanya.
Polisi walifanikiwa kuwakamata Paulo Dulle na mhudumu wa nyumba hiyo ya wageni,aitwaye Taida ambapo wananchi wakiwa mikono mitupu waliandamana hadi kituoni hapo na kuwataka polisi wamuachie Dulle ili wamuue pia.
Naye Meneja wa nyumba hiyo ya kulala wageni Altimalta, Furaha Mgalla alisema Julai 1,mwaka huu, aliwapokea wapangaji watatu aliowataja kuwa ni Ezekia Mbope, Paulo Dulle ambaye ni mpiga ramli, mkazi wa Tunduma na Salum.
Mgalla aliongeza kuwa jana saa 5:00 usiku, kulitokea ugomvi wa kimapenzi kati ya mhudumu wake aliyemtaja kwa jina moja la Taida na mpangaji Dulle, hali iliyopelekea aingilie kati ili kuleta suluhu.
“Baada ya kuwafuata mhudumu wangu Taida alidai kuwa Dulle alitaka kumkaba na amempora shilingi 80,000, ambapo nilipomuuliza Dulle hakutaka kuongea na badala yake alitoka nje.Mwenzake Salum alipoelezwa kilichojiri alianza kumpiga Dulle”alisema Mgalla.
Aliongeza kuwa kelele za ugomvi huo ziliwafikia Sungusungu, ambao walifika eneo hilo na kuwakamata Taida pamoja na Salum na kuwapeleka kituo kidogo cha polisi Mlowo, lakini Dulle alikataa kukamatwa.
Mgalla alisema ndipo Sungusungu hao walipotoka hapo na kuendelea na doria ambapo, waliwakuta vijana hao wawili eneo la darajani wakijianda kwenda kufanya uharifu na kuwazingira ambapo mmoja alifanikiwa kukimbia.
Taarifa zaidi zilizopatikana kwa watu walishuhudia tukio hilo, walisema mara baada ya kumuacha majeruhi huyo na kuanza kumfuata mwenzake aliyekuwa amekimbia, nyuma baadhi ya Sungusungu waliokuwa wameachwa na majeruhi huyo waliamua kutafuta majani na kuanza kumchoma moto mtuhumiwa.
Zilidai kuwa ndipo mtuhumiwa huyo alipokurupuka huku akipiga kelele, na kwenda kujitumbukiza katika mto ulio karibu na eneo hilo ili kuuzima moto uliokuwa ukiwaka mwilini mwake, na kelele hizo zilivuta kundi la watu waliofika na kumpiga na kisha kumchoma moto.
Imeelezwa kuwa Sungusungu hao walioondoka na kwenda moja kwa moja katika nyumba ya kulala wageni Altimalta kwani inadaiwa kuwa walikuwa na mashaka na kundi la watu hao watatu waliokuwa wamepanga hapo kuwa ni majambazi.
Hivyo walihisi kuwa mtuhumiwa aliyekimbia ni mmoja wa wapangaji watatu waliokuwa wakiwatilia mashaka, ambap walipofika waliizingira nyumba hiyo ya wageni ili kuhakikisha kuwa hakuna anayefanikiwa kutoroka.
Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Advocate Nyombi, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo la mauaji lakini alisema marehemu hajatambulika jina na kwamba wanawashikilia watu wawili kwa upelelezi zaidi.
Nyombi aliongeza kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa hospitali ya wilaya Vwawa.
Wednesday, August 5, 2009
UVCCM YATOA UFAFANUZI KUHUSU RIDHWANI KIKWETE
UONGOZI wa jumuia ya Umoja wa Vijana ya Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), wilaya ya Kyela, umepinga uzushi unaonezwa kuwa Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji UVCCM Taifa, Ridhwan Kikwete, alizuiwa kushiriki harambee wilayani humo.
Imeelezwa kuwa UVCCM wilaya hiyo walimuomba Kikwete kuwa mgeni rasmi katika harambee hiyo iliyofanyika Julai 31,mwaka huu kwa kuwa ni kiongozi wa kitaifa wa jumuia hiyo na si vinginevyo.
Katibu wa UVCCM wilaya ya Kyela, George Silindu, aliyasema hayo wilayani humo kufuatia habari moja iliyoandikwa na gazeti moja la kila siku (jina linahifadhiwa) kuwa Kikwete aliingia mitini baada ya kuzuiwa na kundi moja la kisiasa wilayani humo.
Silindu alisema walianza kufanya mawasiliano na Kikwete kwa njia yam domo tangu mwaka 2008, ambapo mawasiliano rasmi ikiwa ni kumuandikia barua kupitia Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa yalianza mwezi Februali mwaka huu.
“Tulimualika awe mgeni rasmi katika harambee yetu kwa ajili ya kutafuta mtaji wa UVCCM wilaya ya Kyela…Makadirio yetu yalikuwa ni kupata shilingi milioni 155 kwa awamu mbili tofauti” alisema Silindu.
Aliongeza kuwa Julai 31, mwaka huu baada ya kufanya mawasiliano na Mjumbe huyo wa Kamati ya Utekelezaji UVCCM Taifa, waliandaa mapokezi eneo la Busale, ambapo walikaa hadi saa 11:00 jioni bila ya kiongozi huyo kutokea.
Alifafanua kuwa waliamua kurudi ukumbi wa KBC uliopo Kyela mjini, ambako ndiko harambee ilikuwa ifanyike wakiwa wameongozana na viongozi wa UVCCM mkoa wa Mbeya pamoja na wawakilishi wa CCM mkoa ambao waliongozwa na Katibu wa Uchumi na fedha Keneth Ndingo.
Katibu huyo wa UVCCM wilaya alisema iliwabidi kuendesha harambee hiyo kama walivyokuwa wamepanga, lakini walishindwa kutangaza kiwango kilichopatikana kwa kuhofia kuwa Kikwete anaweza kutokea wakato wowote wakiwa ukumbini humo.
Silindu alisema Kamati maalumu ya harambee hiyo leo (jana), ilikuwa inatarajiwa kukutana kwa ajili ya kufanya tathmini nzima ya harambee hiyo na ndio itatangaza kiasi cha fedha kilichopatikana.
Aliongeza kuwa mbali ya kuendesha harambee hiyo, Kikwete pia alikuwa amepangiwa kazi ya kufungua matawi mawili ya UVCCM katika maeneo ya Ipinda na Ngyeke yaliyopo kata ya Matema na baadaye ahutubie mkutano wa hadhara katika kata hiyo.
“Tulimualika Kikwete kwa kuwa ni kiongozi wa kitaifa wa UVCCM,lakini hatukumualika kwa makusudi mengine yoyote kama inavyoenezwa…hivyo siyo sahihi kuwa alizuiwa kuja Kyela na kundi moja la kisiasa wilayani humu” alisema Silindu.
Alifafanua kuwa Kikwete asingekuwa kiongozi wa jumuia hiyo ngazi ya kitaifa, ndio ilipaswa watu wahoji kuwa ameenda wilayani humo kama nani lakini itambulike kuwa ni kiongozi wa kitaifa na ndiyo iliyoisukuma jumuia hiyo kumualika.
Silindu alisema kuwa UVCCM wilaya hiyo haiwezi kushtushwa na Kikwete kutohudhuria harambee, kwani naye ni binadamu kama walivyo wengine hivyo anaweza kupata udhuru uliopelekea ashindwe kufika wilayani Kyela.
Alibainisha kuwa wapo viongozi wengine waliowatumia kadi za mwaliko wakiwemo kutoka Dar es Salaam lakini walishindwa kufika, ila walituma michango yao waliyoahidi hivyo kutofika kwa Kikwete kusiwe nongwa.
“Kwa mtu mwenye shaka yoyote juu ysa ujio wa Kikwete ni vyema awasiliane na Mwenyekiti wa UVCCM wilayani hapa, Dk.Hunter Mwakifuna ama mimi ili tumpe ufafanuzi lakini siyo kuzusha mambo ambayo hayapo” alisema Silindu kwa msisitizo.
Imeelezwa kuwa UVCCM wilaya hiyo walimuomba Kikwete kuwa mgeni rasmi katika harambee hiyo iliyofanyika Julai 31,mwaka huu kwa kuwa ni kiongozi wa kitaifa wa jumuia hiyo na si vinginevyo.
Katibu wa UVCCM wilaya ya Kyela, George Silindu, aliyasema hayo wilayani humo kufuatia habari moja iliyoandikwa na gazeti moja la kila siku (jina linahifadhiwa) kuwa Kikwete aliingia mitini baada ya kuzuiwa na kundi moja la kisiasa wilayani humo.
Silindu alisema walianza kufanya mawasiliano na Kikwete kwa njia yam domo tangu mwaka 2008, ambapo mawasiliano rasmi ikiwa ni kumuandikia barua kupitia Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa yalianza mwezi Februali mwaka huu.
“Tulimualika awe mgeni rasmi katika harambee yetu kwa ajili ya kutafuta mtaji wa UVCCM wilaya ya Kyela…Makadirio yetu yalikuwa ni kupata shilingi milioni 155 kwa awamu mbili tofauti” alisema Silindu.
Aliongeza kuwa Julai 31, mwaka huu baada ya kufanya mawasiliano na Mjumbe huyo wa Kamati ya Utekelezaji UVCCM Taifa, waliandaa mapokezi eneo la Busale, ambapo walikaa hadi saa 11:00 jioni bila ya kiongozi huyo kutokea.
Alifafanua kuwa waliamua kurudi ukumbi wa KBC uliopo Kyela mjini, ambako ndiko harambee ilikuwa ifanyike wakiwa wameongozana na viongozi wa UVCCM mkoa wa Mbeya pamoja na wawakilishi wa CCM mkoa ambao waliongozwa na Katibu wa Uchumi na fedha Keneth Ndingo.
Katibu huyo wa UVCCM wilaya alisema iliwabidi kuendesha harambee hiyo kama walivyokuwa wamepanga, lakini walishindwa kutangaza kiwango kilichopatikana kwa kuhofia kuwa Kikwete anaweza kutokea wakato wowote wakiwa ukumbini humo.
Silindu alisema Kamati maalumu ya harambee hiyo leo (jana), ilikuwa inatarajiwa kukutana kwa ajili ya kufanya tathmini nzima ya harambee hiyo na ndio itatangaza kiasi cha fedha kilichopatikana.
Aliongeza kuwa mbali ya kuendesha harambee hiyo, Kikwete pia alikuwa amepangiwa kazi ya kufungua matawi mawili ya UVCCM katika maeneo ya Ipinda na Ngyeke yaliyopo kata ya Matema na baadaye ahutubie mkutano wa hadhara katika kata hiyo.
“Tulimualika Kikwete kwa kuwa ni kiongozi wa kitaifa wa UVCCM,lakini hatukumualika kwa makusudi mengine yoyote kama inavyoenezwa…hivyo siyo sahihi kuwa alizuiwa kuja Kyela na kundi moja la kisiasa wilayani humu” alisema Silindu.
Alifafanua kuwa Kikwete asingekuwa kiongozi wa jumuia hiyo ngazi ya kitaifa, ndio ilipaswa watu wahoji kuwa ameenda wilayani humo kama nani lakini itambulike kuwa ni kiongozi wa kitaifa na ndiyo iliyoisukuma jumuia hiyo kumualika.
Silindu alisema kuwa UVCCM wilaya hiyo haiwezi kushtushwa na Kikwete kutohudhuria harambee, kwani naye ni binadamu kama walivyo wengine hivyo anaweza kupata udhuru uliopelekea ashindwe kufika wilayani Kyela.
Alibainisha kuwa wapo viongozi wengine waliowatumia kadi za mwaliko wakiwemo kutoka Dar es Salaam lakini walishindwa kufika, ila walituma michango yao waliyoahidi hivyo kutofika kwa Kikwete kusiwe nongwa.
“Kwa mtu mwenye shaka yoyote juu ysa ujio wa Kikwete ni vyema awasiliane na Mwenyekiti wa UVCCM wilayani hapa, Dk.Hunter Mwakifuna ama mimi ili tumpe ufafanuzi lakini siyo kuzusha mambo ambayo hayapo” alisema Silindu kwa msisitizo.
HALMASHAURI WILAYA YA KYELA YASHINDWA KUTUMIA SH.MILIONI 700
MKURUGENZI wa halmashauri ya wilaya Kyela, Harold Senyagwa, amefanya ukaguzi wa ghafla na kubaini jumla ya shilingi 738,317,808 zilizokuwa zimetengwa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2008/09, hazijatumika.
Kufuatia hatua hiyo, ameunda Timu ya Ukaguzi ya watu watatu ili kufanya uchunguzi zaidi kujua sababu zilizopelekea kiasi hicho cha fedha kukaa bila kutumika hadi mwaka mwingine wa fedha unaanza.
Akithibitisha hilo kwa mwandishi wa habari hizi jana ofisini kwake, Senyagwa alisema kuwa alifanya ukaguzi huo Juni 15,mwaka huu wakati zimebakia siku kumi na tano kabla ya mwaka wa fedha kumalizika ili kujua kiasi cha fedha kilichotumika.
Mkurugenzi huyo Mtendaji alizitaja baadhi ya idara zilizobakiza fedha na kuwa ni Afya kwa upande wa ‘Busket fund’ sh.milioni 40.4, Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi (MMAM) sh.milioni 45.4, Ukimwi sh.140.8 na Kilimo na Mifugo sh.milioni 400.
“Lakini tumebaini pia kuna fedha nyingine ziliingia Juni 12,mwaka huu ambazo ni za MMAM sh.24.4 na RWSSP shilingi milioni 41.2.Hivyo ilikuwa ni vigumu kwa fedha hizo kutumika bila kufuata utaratibu uliowekwa na serikali” alisema Senyagwa.
Aliongeza kuwa aliwaandikia barua wakuu wa Idara ambao hawakutumia fedha zao walizokuwa wametengewa ambapo baadhi aliridhika na maelezo waliyoyatoa na wengine hakuridhika na maelezo yao.
Alizitaja idara alizoridhika na maelezo waliyotoa kuwa ni za MMAM, RWSSP na Kilimo ambao nao walipata fedha nyingine kiasi cha shilingi milioni 70 mwezi Machi, mwaka huu kwa ajili ya kuendeleza Kilimo.
Senyagwa alisema mbali ya kuunda timu ya kuchunguza sababu iliyopelekea fedha hizo zisitumike pia tayari ametoa taarifa hiyo kwa Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ya halmashauri hiyo juu ya suala hilo.
“Baada ya timu hii ya watu watatu kumaliza kufanya uchunguzi wao na kuniletea walichobaini itajulikana ni hatua zipi zichukuliwe” alisema Senyagwa.
Aliongeza kuwa pia hiyo ya Kamati ya Fedha imependekeza kuwa fedha hizo zaidi ya shilingi milioni 700 zifanyiwe Mpango mkakati wa kuhakikisha zinatumika ili zisiingiliane na bajeti ya mwaka huu wa fedha 2009/10.
Mkurugenzi alisema hivi sasa utekelezaji wake unaendelea lakini amewataka Wakuu wa idara ndani ya halmashauri ya Kyela, kuanza kuoredhesha na kukamilisha mahitaji mapema yakiwemo mambo ya tenda (zabuni).Senyagwa alisema:
”Kwa kufanya hivi itapelekea tusiwe na mambo kama haya ya kubakisha fedha hadi mwaka wa fedha unakwisha kwa miaka ijayo…lakini ikumbukwe kuwa mimi Mkurugenzi ndiye niliyeibua na kubaini kiasi hiki cha fedha kubaki”.
Kufuatia hatua hiyo, ameunda Timu ya Ukaguzi ya watu watatu ili kufanya uchunguzi zaidi kujua sababu zilizopelekea kiasi hicho cha fedha kukaa bila kutumika hadi mwaka mwingine wa fedha unaanza.
Akithibitisha hilo kwa mwandishi wa habari hizi jana ofisini kwake, Senyagwa alisema kuwa alifanya ukaguzi huo Juni 15,mwaka huu wakati zimebakia siku kumi na tano kabla ya mwaka wa fedha kumalizika ili kujua kiasi cha fedha kilichotumika.
Mkurugenzi huyo Mtendaji alizitaja baadhi ya idara zilizobakiza fedha na kuwa ni Afya kwa upande wa ‘Busket fund’ sh.milioni 40.4, Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi (MMAM) sh.milioni 45.4, Ukimwi sh.140.8 na Kilimo na Mifugo sh.milioni 400.
“Lakini tumebaini pia kuna fedha nyingine ziliingia Juni 12,mwaka huu ambazo ni za MMAM sh.24.4 na RWSSP shilingi milioni 41.2.Hivyo ilikuwa ni vigumu kwa fedha hizo kutumika bila kufuata utaratibu uliowekwa na serikali” alisema Senyagwa.
Aliongeza kuwa aliwaandikia barua wakuu wa Idara ambao hawakutumia fedha zao walizokuwa wametengewa ambapo baadhi aliridhika na maelezo waliyoyatoa na wengine hakuridhika na maelezo yao.
Alizitaja idara alizoridhika na maelezo waliyotoa kuwa ni za MMAM, RWSSP na Kilimo ambao nao walipata fedha nyingine kiasi cha shilingi milioni 70 mwezi Machi, mwaka huu kwa ajili ya kuendeleza Kilimo.
Senyagwa alisema mbali ya kuunda timu ya kuchunguza sababu iliyopelekea fedha hizo zisitumike pia tayari ametoa taarifa hiyo kwa Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ya halmashauri hiyo juu ya suala hilo.
“Baada ya timu hii ya watu watatu kumaliza kufanya uchunguzi wao na kuniletea walichobaini itajulikana ni hatua zipi zichukuliwe” alisema Senyagwa.
Aliongeza kuwa pia hiyo ya Kamati ya Fedha imependekeza kuwa fedha hizo zaidi ya shilingi milioni 700 zifanyiwe Mpango mkakati wa kuhakikisha zinatumika ili zisiingiliane na bajeti ya mwaka huu wa fedha 2009/10.
Mkurugenzi alisema hivi sasa utekelezaji wake unaendelea lakini amewataka Wakuu wa idara ndani ya halmashauri ya Kyela, kuanza kuoredhesha na kukamilisha mahitaji mapema yakiwemo mambo ya tenda (zabuni).Senyagwa alisema:
”Kwa kufanya hivi itapelekea tusiwe na mambo kama haya ya kubakisha fedha hadi mwaka wa fedha unakwisha kwa miaka ijayo…lakini ikumbukwe kuwa mimi Mkurugenzi ndiye niliyeibua na kubaini kiasi hiki cha fedha kubaki”.
WAGOMEA KULIPWA FIDIA KIDUCHU KUPISHA UJENZI WA SOKO JIPYA LA MWANJELWA
WAMILIKI 30 wa nyumba zinazotaka kubomolewa kata ya Ruanda, ili kupisha ujenzi wa soko jipya la kisasa la Mwanjelwa, wamepinga kiwango kidogo cha fidia wanachotaka kulipwa na halmashauri ya jiji la Mbeya.
Imeelezwa kuwa halmashauri hiyo imetenga kiasi cha shilingi Bilioni 1.1 kwa ajili ya kulipa fidia huku kiwango cha juu cha fidia kikiwa ni sh.milioni 82.3 na cha chini ni sh. milioni 9.
Soko la awali Mwanjelwa lililokuwa na wafanyabiashara zaidi ya 900, liliungua na kuteketea kwa moto Desemba mwaka 2006, na kupelekea hasara ya mamilioni ya shilingi.
Wamesema kuwa wanatarajia kuandika barua kwa Mkurugenzi wa jiji kupinga kiwango wanacjhotaka kulipwa na iwapo watapuuzwa basi watafungua kesi mahakamani kupinga nyumba zao kubomolewa.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana, walisema kuwa nyumba zao hizo zimekaa kibiashara kwani zipo katika mtaa wa soko ambapo wenzao walio umbali wa mita 50 wamekuwa wakiziuza nyumba zao kati ya shilingi milioni 400 hadi milioni 200.
Vitus Swalo mwenye nyumba namba R/049 alisema kuwa yeye licha ya kumiliki nyumba kubwa ya kibiashara anashangaa kuwa katika uthamini uliofanywa na maofisa wa kitengo cha uthamini cha jiji kilichopo chini ya Edina Mwaigomole, anatakiwa kulipwa fidia y ash.milioni 11 kitu ambacho hawezi kukubaliana nacho.
Swalo alisema wao wanakubali nyumba zao kubomolewa ili kupisha ujenzi wa soko hilo lililotengewa jumla ya shilingi Bilioni 13 kwa ajili ya ujenzi wake, lakini hakubaliana na fidia anayotaka kulipwa kwani hailingani na eneo ilipo nyumba yake.
“Fedha ya fidia tunayotaka kulipwa na halmashauri ya jiji la Mbeya ni ndogo na mbaya zaidi ni kuwa hailingani na hasdhi ya jiji bali ni ile ya halmashauri…hatukatai kupisha ujenzi lakini kiwango hatukubaliani nacho” alisema Swalo.
Naye Keneth Mbewe mwenye nyumba namba R/.004 alisema wanapinga kiwango kidogo walichotengewa kwa ajili ya fidia na wanaiomba serikali kuingilia kati ili haki iweze kutendeka na wapate fidia ya kiwango kinacholingana na eneo hilo la kibiashara zilizopo nyumba zao.
Mbewe alisema kuwa wanataka kumuandikia barua Mkurugenzi wa halmashauri ya jiji la Mbeya, Elizabeth Munuo, kupinga kiwango hicho kidogo cha fidia na iwapo ombi lao halitasikilizwa basi wapo tayari kwenda Mahakamani kusimamisha zoezi hilo la ubomoaji wa nyumba zao.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa mtaa wa Soko, zilizopo nyumba hizo, Baraka Mwakyabula, alisema uthaminishaji wa nyumba hizo hauendani na hadhi ya jiji licha ya kwamba wananchi wake wameelezwa kuwa eneo hilo linatakiwa lijengwe soko la kisasa lenye hadhi ya jiji.
Naye Diwani wa kata ya Ruanda, Ephraim Mwaitenda, alipofuatwa alikiri kuwa baadhi ya wananchi wanaomiliki nyumba zinazotakiwa kubomolewa ili kupisha ujenzi wa soko hilo jipya, wamelalamikia kiwango kidogo cha fidia wanachotaka kulipwa.
Mwaitenda alisema lakini fedha hizo wanalipwa kulingana na uthamini uliofanywa na kitengo cha Uthamini cha halmashauri ya jiji la Mbeya, kulingana na matofali yaliyotumika kujenga nyumba husika.
“Baadhi ya nyumba zimejengwa kwa matofali ya saruji, matofali ya kuchoma na nyingine zimejengwa kwa matofali mabichi…kwa mantiki hiyo ni wazi kuwa wale waliojenga kwa matofali ya saruji (Block), watalipwa fidia kubwa zaidi” alisema Mwaitenda.
Aliongeza kuwa amewataka wamiliki hao waliokuwa wanapinga kiwango hicho cha fidia kurudi majumbani mwao, kuchukua karatasi za uhakiki na kisha kuzilinganisha na thamani halisi ya nyumba zao.
Mwaitenda alisema:”Nimewataka baada ya hapo iwapo wataona kuwa hawajaridhika na kiwango cha fidia wanachotaka kulipwa wauone uongozi wa jiji la Mbeya, ili suala lao lipatiwe ufumbuzi”.
Imeelezwa kuwa halmashauri hiyo imetenga kiasi cha shilingi Bilioni 1.1 kwa ajili ya kulipa fidia huku kiwango cha juu cha fidia kikiwa ni sh.milioni 82.3 na cha chini ni sh. milioni 9.
Soko la awali Mwanjelwa lililokuwa na wafanyabiashara zaidi ya 900, liliungua na kuteketea kwa moto Desemba mwaka 2006, na kupelekea hasara ya mamilioni ya shilingi.
Wamesema kuwa wanatarajia kuandika barua kwa Mkurugenzi wa jiji kupinga kiwango wanacjhotaka kulipwa na iwapo watapuuzwa basi watafungua kesi mahakamani kupinga nyumba zao kubomolewa.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana, walisema kuwa nyumba zao hizo zimekaa kibiashara kwani zipo katika mtaa wa soko ambapo wenzao walio umbali wa mita 50 wamekuwa wakiziuza nyumba zao kati ya shilingi milioni 400 hadi milioni 200.
Vitus Swalo mwenye nyumba namba R/049 alisema kuwa yeye licha ya kumiliki nyumba kubwa ya kibiashara anashangaa kuwa katika uthamini uliofanywa na maofisa wa kitengo cha uthamini cha jiji kilichopo chini ya Edina Mwaigomole, anatakiwa kulipwa fidia y ash.milioni 11 kitu ambacho hawezi kukubaliana nacho.
Swalo alisema wao wanakubali nyumba zao kubomolewa ili kupisha ujenzi wa soko hilo lililotengewa jumla ya shilingi Bilioni 13 kwa ajili ya ujenzi wake, lakini hakubaliana na fidia anayotaka kulipwa kwani hailingani na eneo ilipo nyumba yake.
“Fedha ya fidia tunayotaka kulipwa na halmashauri ya jiji la Mbeya ni ndogo na mbaya zaidi ni kuwa hailingani na hasdhi ya jiji bali ni ile ya halmashauri…hatukatai kupisha ujenzi lakini kiwango hatukubaliani nacho” alisema Swalo.
Naye Keneth Mbewe mwenye nyumba namba R/.004 alisema wanapinga kiwango kidogo walichotengewa kwa ajili ya fidia na wanaiomba serikali kuingilia kati ili haki iweze kutendeka na wapate fidia ya kiwango kinacholingana na eneo hilo la kibiashara zilizopo nyumba zao.
Mbewe alisema kuwa wanataka kumuandikia barua Mkurugenzi wa halmashauri ya jiji la Mbeya, Elizabeth Munuo, kupinga kiwango hicho kidogo cha fidia na iwapo ombi lao halitasikilizwa basi wapo tayari kwenda Mahakamani kusimamisha zoezi hilo la ubomoaji wa nyumba zao.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa mtaa wa Soko, zilizopo nyumba hizo, Baraka Mwakyabula, alisema uthaminishaji wa nyumba hizo hauendani na hadhi ya jiji licha ya kwamba wananchi wake wameelezwa kuwa eneo hilo linatakiwa lijengwe soko la kisasa lenye hadhi ya jiji.
Naye Diwani wa kata ya Ruanda, Ephraim Mwaitenda, alipofuatwa alikiri kuwa baadhi ya wananchi wanaomiliki nyumba zinazotakiwa kubomolewa ili kupisha ujenzi wa soko hilo jipya, wamelalamikia kiwango kidogo cha fidia wanachotaka kulipwa.
Mwaitenda alisema lakini fedha hizo wanalipwa kulingana na uthamini uliofanywa na kitengo cha Uthamini cha halmashauri ya jiji la Mbeya, kulingana na matofali yaliyotumika kujenga nyumba husika.
“Baadhi ya nyumba zimejengwa kwa matofali ya saruji, matofali ya kuchoma na nyingine zimejengwa kwa matofali mabichi…kwa mantiki hiyo ni wazi kuwa wale waliojenga kwa matofali ya saruji (Block), watalipwa fidia kubwa zaidi” alisema Mwaitenda.
Aliongeza kuwa amewataka wamiliki hao waliokuwa wanapinga kiwango hicho cha fidia kurudi majumbani mwao, kuchukua karatasi za uhakiki na kisha kuzilinganisha na thamani halisi ya nyumba zao.
Mwaitenda alisema:”Nimewataka baada ya hapo iwapo wataona kuwa hawajaridhika na kiwango cha fidia wanachotaka kulipwa wauone uongozi wa jiji la Mbeya, ili suala lao lipatiwe ufumbuzi”.
Wednesday, July 29, 2009
WALIMU JIJINI MBEYA WAZUSHA TIMBWILI OFISI ZA JIJI NA BAADAYE KWA DC.
KUNDI la Walimu zaidi ya 100 wakiwa na jazba jana walivamia ofisi za Elimu na baadaye ofisi za Mkuu wa wilaya ya Mbeya, Leonidas Gama, wakilalamikia kucheleweshewa malipo yao bila chochote kulipwa tangu mwaka 2001 hadi 2007.
Kitendo hicho cha walimu kuzingira ofisi za elimu jijini hapa saa 2:00 asubuhi, kilipelekea baadhi ya watendaji kuzikimbia ofisi zao wakihofia kuwa wangeweza kupata kipigo kutoka kwa walimu hao.
Walidai kuwa wamekuwa wakifanywa wapumbavu na wanyonge ambapo wamekuwa wakitakiwa kuwasilisha kumbukumbu zao za madai ambapo mchakato umekuwa ukizidi kurefushwa.
Wakizungumza na waandishi wa habari waliofuatilia tukio hilo, walimu hao walisema kuwa waliambiwa waende ofisi hizo kati ya Julai 20 na 24 mwaka huu lakini kila mwalimu aliyefika hapo aliambiwa arudi siku nyingine huku wengine wakitakiwa kuwasilisha vielelezo vya madai yao wakati walikwisha kuviwasilisha awali.
Waandishi walifanikiwa kufika ofisi hizo za Ofisa Elimu wa jiji na kukutana na msongamano wa walimu hao waliokuwa wakidai hawawezi kuondoka ofisini hapo hadi madai yao yafanyiwe kazi.
Wakizungumza wakiwa katika makundi, walisema kuwa malimbikizo hayo ni mishahara, nauli za likizo,marekebisho ya mishahara yao kwa waliopandishwa vyeo huku waliorekebishiwa madaraja hawajawahi kupata mishahara mipya kwa muda wa miaka saba.
Naye Ofisa Elimu wa jiji la Mbeya, Aurelia Lwenza alipfuatwa alisema kuwa hajui lolote kuhusu mchakato mzima wa madai hayo ya walimu kwani mchakato mzima ulikuwa ukifanywa na idara ya utumishi kwa kushirikiana na Tume ya Utumishi wa Walimu(TSD), ofisi yake haikhusiki na madai hayo.
Aurelia aliongeza kuwa hana taarifa na uvamizi wa walimu hao isipokuwa walipofika alilazimika kumuita Ofisa Utumishi anayeshughulikia madai hayo awaondoe walimu hao kwani ofisi za TSD zipo.
Baadaye ndipo kundi hilo la walimu lilipovamia ofisi za Mkuu wa wilaya ya Mbeya, Gama ili kuwasilisha malalamiko yao, lakini hawakufanikiwa kumkuta kwani na kuelezwa kuwa yupo safarini jijini Dar es Salaam.
Kwa upande wake Ofisa Utumishi wa jiji, Lucy Timba hakuweza kuweka wazi kuhusu madai ya walimu hao na na kwamba haelewi sababu zilizowafanya wakusanyike kwenye ofisi hizo badala ya kuutumia muda huo kufundisha.
Lucy alithibitisha wito wa kuitwa kwa walimu hao uliotolewa na Katibu wa Tume ya Utumishi ya Walimu jiji la Mbeya,Fredy Lucas ambaye hakuweza kupatikana kwani yupo mkoani Morogoro kikazi.
Kitendo hicho cha walimu kuzingira ofisi za elimu jijini hapa saa 2:00 asubuhi, kilipelekea baadhi ya watendaji kuzikimbia ofisi zao wakihofia kuwa wangeweza kupata kipigo kutoka kwa walimu hao.
Walidai kuwa wamekuwa wakifanywa wapumbavu na wanyonge ambapo wamekuwa wakitakiwa kuwasilisha kumbukumbu zao za madai ambapo mchakato umekuwa ukizidi kurefushwa.
Wakizungumza na waandishi wa habari waliofuatilia tukio hilo, walimu hao walisema kuwa waliambiwa waende ofisi hizo kati ya Julai 20 na 24 mwaka huu lakini kila mwalimu aliyefika hapo aliambiwa arudi siku nyingine huku wengine wakitakiwa kuwasilisha vielelezo vya madai yao wakati walikwisha kuviwasilisha awali.
Waandishi walifanikiwa kufika ofisi hizo za Ofisa Elimu wa jiji na kukutana na msongamano wa walimu hao waliokuwa wakidai hawawezi kuondoka ofisini hapo hadi madai yao yafanyiwe kazi.
Wakizungumza wakiwa katika makundi, walisema kuwa malimbikizo hayo ni mishahara, nauli za likizo,marekebisho ya mishahara yao kwa waliopandishwa vyeo huku waliorekebishiwa madaraja hawajawahi kupata mishahara mipya kwa muda wa miaka saba.
Naye Ofisa Elimu wa jiji la Mbeya, Aurelia Lwenza alipfuatwa alisema kuwa hajui lolote kuhusu mchakato mzima wa madai hayo ya walimu kwani mchakato mzima ulikuwa ukifanywa na idara ya utumishi kwa kushirikiana na Tume ya Utumishi wa Walimu(TSD), ofisi yake haikhusiki na madai hayo.
Aurelia aliongeza kuwa hana taarifa na uvamizi wa walimu hao isipokuwa walipofika alilazimika kumuita Ofisa Utumishi anayeshughulikia madai hayo awaondoe walimu hao kwani ofisi za TSD zipo.
Baadaye ndipo kundi hilo la walimu lilipovamia ofisi za Mkuu wa wilaya ya Mbeya, Gama ili kuwasilisha malalamiko yao, lakini hawakufanikiwa kumkuta kwani na kuelezwa kuwa yupo safarini jijini Dar es Salaam.
Kwa upande wake Ofisa Utumishi wa jiji, Lucy Timba hakuweza kuweka wazi kuhusu madai ya walimu hao na na kwamba haelewi sababu zilizowafanya wakusanyike kwenye ofisi hizo badala ya kuutumia muda huo kufundisha.
Lucy alithibitisha wito wa kuitwa kwa walimu hao uliotolewa na Katibu wa Tume ya Utumishi ya Walimu jiji la Mbeya,Fredy Lucas ambaye hakuweza kupatikana kwani yupo mkoani Morogoro kikazi.
HOSPITALI YA RUFAA MBEYA WATAKIWA KUTENDA HAKI KATIKA MALIPO YA SAA ZA ZIADA.
UONGOZI wa hospitali ya Rufaa Mbeya, umetakiwa kuwalipa wafanyakazi wake malipo ya saa za ziada kwa kufuata ngazi za mshahara (TGHS), na siyo utaratibu uliopo sasa.
Imeelezwa kuwa uongozi huo umekuwa ukiwaweka maofisa katika makundi mawili, lakini wote wamekuwa wakilipwa saa za ziada kwa kima cha chini cha mshahara, hali ambayo inakuwa haiwatendei haki.
Hayo yalisemwa jana na Mwenyekiti wa Chama Cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE), hospitalini hapo, Ismail Zambi, wakati wa hafla ya kuwapa zawadi wafanyakazi bora wa Sikukuu ya Wafanyakazi duniani(Mei Mosi), mwaka huu, iliyofanyika hospitalini hapo.
Mgeni rasmi katika tukio hilo, alikuwa Rais wa Shirikisho la Vyama Vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Ayuob Omary.
Wafanyakazi saba walipewa zawadi zao akiwemo mfanyakazi bora wa hospitali hiyo kwa mwaka huu ambaye ni muuguzi mkunga, Regina Sithole, aliyezawadiwa shilingi 300,000.
Zambi alisema utaratibu huo unaofanywa na hospitali ya Rufaa Mbeya siyo sahihi kwani umekuwa unawatambua maofisa wenye elimu ya digrii kitu ambacho siyo sahihi.
"Tumekuwa tunawekwa matabaka mawili tofauti wakati kazi ni zile zile...hivyo ingekuwa vyema wangeweka utaratibu wa kuangalia TGHS kwani Utumishi unatutambua kuwa ni maofisa wakati uongozi wa hospitali unamtambua ofisa kuwa ni yule mwenye digrii" alisema Zambi.
Aliongeza kuwa pia kuna mapungufu mengine yaliyopo hospitalini hapo ikiwemo kutowapandisha vyeo wafanyakazi kwa wakati kwa mujibu wa taratibu zilizopo.
Mwenyekiti huyo wa TUGHE alisema vile vile kumekuwepo na tatizo la kutorekebishwa mishahara kwa wakati kwa wanaopandishwa vyeo, kutolipwa mapunjo ya mishahara kwa wanaopandishwa vyeo na kurekebishiwa mishahara yao.
Zambi alisema:"Tunaupongeza uongozi wa hospitali kwa kudumisha utaratibu huu wa kutoa zawadi kwa watumishi hodari wakati wa sherehe za Mei Mosi kwa kila mwaka...".
Naye Rais wa TUCTA Omary alipongeza hatua hiyo ya kuwapatia zawadi watumishi bora, lakini pia alikumbushia kuhusu umuhimu wa kufanya vikao mahali pa kazi kwa kufuata utaratibu uliopo.
Omary alisema kuwa kwa kupitia vikao hivyo uongozi na wafanyakazi wanaweza kuvitumia kuweka wazi kasoro mbalimbali zinazokuwepo na hivyo kuweza kuzipatia ufumbuzi wake.
"Kwa kuwapa zawadi watumishi wenu bora mnakuwa mnawajengea motisha zaidi ya kuwajibika zaidi" alisema Omary.
Wafanyakazi wengine waliopata zawadi zao za shilingi 150, 0000 kila mmoja ni Dk.Henry Mwakayoka, ofisa wa maabara Hilary Mchuka, ofisa muuguzi kitengo cha wajawazito na Watoto Meta, Mwanjaa Kasigwa na ofisa muuguzi kitengo cha huduma ya afya ya akili, Daina Ifwani.
Pia wamo Muuguzi mkunga wa kitengo cha kuhudumia wanaoishi na virusi vya Ukimwi, Eddah Sanjala na Ally Mbasha kutoka upande wa masijala katika sehemu ya utawala.
Imeelezwa kuwa uongozi huo umekuwa ukiwaweka maofisa katika makundi mawili, lakini wote wamekuwa wakilipwa saa za ziada kwa kima cha chini cha mshahara, hali ambayo inakuwa haiwatendei haki.
Hayo yalisemwa jana na Mwenyekiti wa Chama Cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE), hospitalini hapo, Ismail Zambi, wakati wa hafla ya kuwapa zawadi wafanyakazi bora wa Sikukuu ya Wafanyakazi duniani(Mei Mosi), mwaka huu, iliyofanyika hospitalini hapo.
Mgeni rasmi katika tukio hilo, alikuwa Rais wa Shirikisho la Vyama Vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Ayuob Omary.
Wafanyakazi saba walipewa zawadi zao akiwemo mfanyakazi bora wa hospitali hiyo kwa mwaka huu ambaye ni muuguzi mkunga, Regina Sithole, aliyezawadiwa shilingi 300,000.
Zambi alisema utaratibu huo unaofanywa na hospitali ya Rufaa Mbeya siyo sahihi kwani umekuwa unawatambua maofisa wenye elimu ya digrii kitu ambacho siyo sahihi.
"Tumekuwa tunawekwa matabaka mawili tofauti wakati kazi ni zile zile...hivyo ingekuwa vyema wangeweka utaratibu wa kuangalia TGHS kwani Utumishi unatutambua kuwa ni maofisa wakati uongozi wa hospitali unamtambua ofisa kuwa ni yule mwenye digrii" alisema Zambi.
Aliongeza kuwa pia kuna mapungufu mengine yaliyopo hospitalini hapo ikiwemo kutowapandisha vyeo wafanyakazi kwa wakati kwa mujibu wa taratibu zilizopo.
Mwenyekiti huyo wa TUGHE alisema vile vile kumekuwepo na tatizo la kutorekebishwa mishahara kwa wakati kwa wanaopandishwa vyeo, kutolipwa mapunjo ya mishahara kwa wanaopandishwa vyeo na kurekebishiwa mishahara yao.
Zambi alisema:"Tunaupongeza uongozi wa hospitali kwa kudumisha utaratibu huu wa kutoa zawadi kwa watumishi hodari wakati wa sherehe za Mei Mosi kwa kila mwaka...".
Naye Rais wa TUCTA Omary alipongeza hatua hiyo ya kuwapatia zawadi watumishi bora, lakini pia alikumbushia kuhusu umuhimu wa kufanya vikao mahali pa kazi kwa kufuata utaratibu uliopo.
Omary alisema kuwa kwa kupitia vikao hivyo uongozi na wafanyakazi wanaweza kuvitumia kuweka wazi kasoro mbalimbali zinazokuwepo na hivyo kuweza kuzipatia ufumbuzi wake.
"Kwa kuwapa zawadi watumishi wenu bora mnakuwa mnawajengea motisha zaidi ya kuwajibika zaidi" alisema Omary.
Wafanyakazi wengine waliopata zawadi zao za shilingi 150, 0000 kila mmoja ni Dk.Henry Mwakayoka, ofisa wa maabara Hilary Mchuka, ofisa muuguzi kitengo cha wajawazito na Watoto Meta, Mwanjaa Kasigwa na ofisa muuguzi kitengo cha huduma ya afya ya akili, Daina Ifwani.
Pia wamo Muuguzi mkunga wa kitengo cha kuhudumia wanaoishi na virusi vya Ukimwi, Eddah Sanjala na Ally Mbasha kutoka upande wa masijala katika sehemu ya utawala.
Monday, July 27, 2009
SUMATRA KUDHITI DALADALA ZISIZTIKETI KWA ABIRIA JIJINI MBEYA.
MAMLAKA ya Udhibiti Wa Usafiri Nchi kavu na Majini (SUMATRA), kanda ya nyanda za juu kusini, imeazimia kupambana na tatizo sugu la wamiliki wa daladala jijini Mbeya la kutopenda kutoa tiketi kwa abiria.
Imeelezwa kuwa tatizo la utoaji wa tiketi kwa abiria wa daladala jijini Mbeya, limekuwa sugu hali inayopelekea abiria wengi wanaotumia usafiri huo kuona kama ni kawaida kwa wao kutopatiwa tiketi.
Akizungumza ofisini kwake, Ofisa Mfawidhi wa SUMATARA kanda, Amani Shamaje, alisema kuwa wamedhamiria kukomesha tabia hiyo ambayo imekuwa kero kwa abiria wengi.
Shamaje alisema kuwa tatizo hilo lilikuwepo pia kwa mabasi yafanyayo safari kwenda wilayani, lakini hivi sasa limekwisha baada ya SUMATRA kuingilia kati na kuanza kuyakamata mabasi hayo na kutoza faini ya shilingi 250,000 kwa kila basi lililokuwa halitoi tiketi kwa abiria.
"Hivi sasa mabasi mengi yafanyayo safari za kwenda wilayani yamekuwa yanatoa tiketi kwa abiria...tatizo tulilonalo sasa ni utoaji wa tiketi kwa daladala zifanyazo safari hapa jijini Mbeya" alisema Shamaje.
Aliongeza kuwa waliamua kwanza kutilia mkazo suala la uvaaji wa sare kwa madereva na makondakta wa daladala na pia kupiga marufuku usimamaji kwa sehemu zisizo kuwa na vituo ambapo wameweza kufanikiwa kwa kiwango kikubwa.
Ofisa Mfawidhi huyo wa SUMATRA kanda ya nyanda za juu kusini, alisema utoaji wa tiketi kwa abiria wa daladala jijini Mbeya, limekuwa ni tatizo linalowasumbua kwa muda mrefu na wameamua kujipanga ili kuhakikisha kuwa wanalimaliza.
Alisema kuanzia sasa daladala yoyote inayofanya safari zake jijini Mbeya, ambayo itakuwa haitoi tiketi kwa abiria itakuwa inatozwa faini ya shilingi 250,000 au kifungo cha kuanzia mwaka mmoja ama kisichopungua miwili au adhabu zote kwa mpigo.
Katika hatua nyingine, Shamaje alisema kuwa wanaandaa mkakati wa kuwadhibiti madereva wa daladala zinazotoka jijini Mbeya kwenda mji mdogo wa Mbalizi, ambazo zimekuwa hazifiki mwisho wa safari na badala yake kuishia eneo la Iyunga na hivyo kupelekea usumbufu kwa abiria.
Alisema kuwa watakutana na Mkuu wa kikosi cha Usalama barabarani mkoa wa Mbeya, Ezekiel Mgeni, ili kuangalia njia sahihi za kukomesha tabia hiyo ambayo hufanywa kuanzia saa 12:00 jioni ambayo imekuwa inapelekea abiria walazimike kupanda mabasi mawili tofauti ili kukamilisha safari
."Huu ni usumbufu kwa abiria kwani unakuta gari limeandikwa kuwa linakwenda Mbalizi, lakini likifika Iyunga abiria wanaambiwa kuwa hapo ndio mwisho wa safari...hii ni usumbufu kwani huwalazimu abiria kupanda daladala lingine ili kuwawezesha kukamilisha safari" alisema Shemaje.
Imeelezwa kuwa tatizo la utoaji wa tiketi kwa abiria wa daladala jijini Mbeya, limekuwa sugu hali inayopelekea abiria wengi wanaotumia usafiri huo kuona kama ni kawaida kwa wao kutopatiwa tiketi.
Akizungumza ofisini kwake, Ofisa Mfawidhi wa SUMATARA kanda, Amani Shamaje, alisema kuwa wamedhamiria kukomesha tabia hiyo ambayo imekuwa kero kwa abiria wengi.
Shamaje alisema kuwa tatizo hilo lilikuwepo pia kwa mabasi yafanyayo safari kwenda wilayani, lakini hivi sasa limekwisha baada ya SUMATRA kuingilia kati na kuanza kuyakamata mabasi hayo na kutoza faini ya shilingi 250,000 kwa kila basi lililokuwa halitoi tiketi kwa abiria.
"Hivi sasa mabasi mengi yafanyayo safari za kwenda wilayani yamekuwa yanatoa tiketi kwa abiria...tatizo tulilonalo sasa ni utoaji wa tiketi kwa daladala zifanyazo safari hapa jijini Mbeya" alisema Shamaje.
Aliongeza kuwa waliamua kwanza kutilia mkazo suala la uvaaji wa sare kwa madereva na makondakta wa daladala na pia kupiga marufuku usimamaji kwa sehemu zisizo kuwa na vituo ambapo wameweza kufanikiwa kwa kiwango kikubwa.
Ofisa Mfawidhi huyo wa SUMATRA kanda ya nyanda za juu kusini, alisema utoaji wa tiketi kwa abiria wa daladala jijini Mbeya, limekuwa ni tatizo linalowasumbua kwa muda mrefu na wameamua kujipanga ili kuhakikisha kuwa wanalimaliza.
Alisema kuanzia sasa daladala yoyote inayofanya safari zake jijini Mbeya, ambayo itakuwa haitoi tiketi kwa abiria itakuwa inatozwa faini ya shilingi 250,000 au kifungo cha kuanzia mwaka mmoja ama kisichopungua miwili au adhabu zote kwa mpigo.
Katika hatua nyingine, Shamaje alisema kuwa wanaandaa mkakati wa kuwadhibiti madereva wa daladala zinazotoka jijini Mbeya kwenda mji mdogo wa Mbalizi, ambazo zimekuwa hazifiki mwisho wa safari na badala yake kuishia eneo la Iyunga na hivyo kupelekea usumbufu kwa abiria.
Alisema kuwa watakutana na Mkuu wa kikosi cha Usalama barabarani mkoa wa Mbeya, Ezekiel Mgeni, ili kuangalia njia sahihi za kukomesha tabia hiyo ambayo hufanywa kuanzia saa 12:00 jioni ambayo imekuwa inapelekea abiria walazimike kupanda mabasi mawili tofauti ili kukamilisha safari
."Huu ni usumbufu kwa abiria kwani unakuta gari limeandikwa kuwa linakwenda Mbalizi, lakini likifika Iyunga abiria wanaambiwa kuwa hapo ndio mwisho wa safari...hii ni usumbufu kwani huwalazimu abiria kupanda daladala lingine ili kuwawezesha kukamilisha safari" alisema Shemaje.
MARY MWANJELWA AKITOA MSAADA WA SHATI ZA CCM
Thursday, July 23, 2009
WANAWAKEW WATAKIWA KUJITOKEZA KUWANIA UONGOZI SERIKALI ZA MITAA
WANAWAKE mkoani Mbeya, wametakiwa kujitokeza kwa wingi kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi ujao wa serikali za mitaa, kupitia Chama Cha Mapinduzi, kwani uwezo wa kuongoza wanao.
Imeelezwa kuwa kitu kinachowakwamisha wanawake kushinda nafasi mbalimbali za uongozi katika chaguzi ni tabia ya kuonea wivu na kupigana majungu na kutosaidiana.
Wito huo umetolewa na Mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Mary Mwanjelwa, katika ziara zake za kutembelea wilaya zote za mkoa wa Mbeya kuwashukuru wanawake kwa kumchagua katika nafasi hiyo na pia kuangalia uhai wa jumuia na CCM kwa jumla.
Mary alisema umefika wakati wanawake wanatakiwa kujiamini kuwa wanaweza na kwa kufanya hivyo ni wazi hawataweza kushindwa kushinda katika nafasi mbalimbali watakazoomba kuwania kupitia Chama Cha Mapinduzi.
"Tujenge mahusiano mazuri baina yetu sisi wanawake ili tuweze kuasonga mbele, kwa maslahi ya Chama Cha Mapinduzi...tupo katika nafasi hizi kwa nia ya kukitumikia Chama na siyo nje ya hapo" alisema Mwanjelwa.
Aliongeza kuwa itakuwa sifa kubwa kwa CCM na wanawake mkoani hapa, iwapo wanawake wengi watashinda kwa kishindo katika uchaguzi ujao wa serikali za Mitaa.
Alisema, jumuia ya UWT mkoani hapa imekuwa inalegalega kutokana na wanawake kuendekeza majungu na kutopendana kwa sababu zisizokuwa za msingi hali ambayo haikijengi Chama bali inakibomoa.
Mjumbe huyo wa Baraza la UWT TAifa, alisema umefika wakati wanawake mkoani hapa na Tanzania kwa jumla kuachana na wale wanaowaona kuwa wamekuwa wanawachonganisha na kuendeleza majungu ndani ya jumuia na CCM Kwa jumla ili kukifanya Chama kizidi kuimarika na kukubalika kwa wananchi wengi.
Naye Katibu wa UWT mkoa wa Mbeya, Mwanaidy Mbisha, alisema uhai wa Chama na jumuia zake utaonekana pale wanawake watakapokuwa wanalipia kadi zao kwa wakati, kuingiza wanachama wengi na pia kuhakikisha kuwa wanavaa sare za Chama katika shughuli zozote za Chama.
Mwanaidy alisema pia wanawatakiwa kuhakikisha wanafanya vikao vya mara kwa mara kwa mujibu wa Katiba na kunapokuwa na tofauti baina yao basi ni vyema watumie vikao halali vya Chama kumaliza tofauti zao kwa maslahi ya CCM.
"Hamfanyi vikao vya jumuia katika ngazi zenu za matawi na kata...lakini nafikiri tatizo kubwa malokuwa nalo ni kudhani kuwa hamna ajenda za kuitisha vikao hivyo.Lakini hata suala la kuhamasisha kulipia kadi nalo mnaweza kulifanya kuwa ajenda ya kikao chenu" alisema Mwanaidy.
Katika ziara hiyo Mary amekuwa akitoa msaada wa shati za CCM, kwa wajumbe wa Baraza la UWT wa wilaya na kadi mia moja za UWT ili kuziwezesha ofisi za UWT Katika wilaya husika ziweze kutunisha mfuko na kuingiza wanawachama wengi zaidi.
Imeelezwa kuwa kitu kinachowakwamisha wanawake kushinda nafasi mbalimbali za uongozi katika chaguzi ni tabia ya kuonea wivu na kupigana majungu na kutosaidiana.
Wito huo umetolewa na Mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Mary Mwanjelwa, katika ziara zake za kutembelea wilaya zote za mkoa wa Mbeya kuwashukuru wanawake kwa kumchagua katika nafasi hiyo na pia kuangalia uhai wa jumuia na CCM kwa jumla.
Mary alisema umefika wakati wanawake wanatakiwa kujiamini kuwa wanaweza na kwa kufanya hivyo ni wazi hawataweza kushindwa kushinda katika nafasi mbalimbali watakazoomba kuwania kupitia Chama Cha Mapinduzi.
"Tujenge mahusiano mazuri baina yetu sisi wanawake ili tuweze kuasonga mbele, kwa maslahi ya Chama Cha Mapinduzi...tupo katika nafasi hizi kwa nia ya kukitumikia Chama na siyo nje ya hapo" alisema Mwanjelwa.
Aliongeza kuwa itakuwa sifa kubwa kwa CCM na wanawake mkoani hapa, iwapo wanawake wengi watashinda kwa kishindo katika uchaguzi ujao wa serikali za Mitaa.
Alisema, jumuia ya UWT mkoani hapa imekuwa inalegalega kutokana na wanawake kuendekeza majungu na kutopendana kwa sababu zisizokuwa za msingi hali ambayo haikijengi Chama bali inakibomoa.
Mjumbe huyo wa Baraza la UWT TAifa, alisema umefika wakati wanawake mkoani hapa na Tanzania kwa jumla kuachana na wale wanaowaona kuwa wamekuwa wanawachonganisha na kuendeleza majungu ndani ya jumuia na CCM Kwa jumla ili kukifanya Chama kizidi kuimarika na kukubalika kwa wananchi wengi.
Naye Katibu wa UWT mkoa wa Mbeya, Mwanaidy Mbisha, alisema uhai wa Chama na jumuia zake utaonekana pale wanawake watakapokuwa wanalipia kadi zao kwa wakati, kuingiza wanachama wengi na pia kuhakikisha kuwa wanavaa sare za Chama katika shughuli zozote za Chama.
Mwanaidy alisema pia wanawatakiwa kuhakikisha wanafanya vikao vya mara kwa mara kwa mujibu wa Katiba na kunapokuwa na tofauti baina yao basi ni vyema watumie vikao halali vya Chama kumaliza tofauti zao kwa maslahi ya CCM.
"Hamfanyi vikao vya jumuia katika ngazi zenu za matawi na kata...lakini nafikiri tatizo kubwa malokuwa nalo ni kudhani kuwa hamna ajenda za kuitisha vikao hivyo.Lakini hata suala la kuhamasisha kulipia kadi nalo mnaweza kulifanya kuwa ajenda ya kikao chenu" alisema Mwanaidy.
Katika ziara hiyo Mary amekuwa akitoa msaada wa shati za CCM, kwa wajumbe wa Baraza la UWT wa wilaya na kadi mia moja za UWT ili kuziwezesha ofisi za UWT Katika wilaya husika ziweze kutunisha mfuko na kuingiza wanawachama wengi zaidi.
MARY MWANJELWA AJITOLEA KUSOMESHA WATOTO YATIMA WANANE MBEYA
MJUMBE wa Baraza Kuu la Umoja wa Wanawake (UWT), kutoka mkoa wa Mbeya, Mary Mwanjelwa, amejitolea kusomesha watoto yatima wa kike wanane waliofaulu mtihani wa darasa la saba, kutoka wilaya zote mkoani hapa, lakini hawana uwezo wa kusomeshwa sekondari.
Hivyo amezitaka kamati za Utekelezaji za UWT za wilaya hizo, kufanya mchakato bila ya upendeleo ili kuwapata watoto hao yatima ambao yeye atawajibika kuwalipia ada na mahitaji yote muhimu katika sekondari za kata.
"Jukumu la kuwalea watoto hawa yatima ni letu sisi wanawake wote...serikali na taifa kwa jumla wameonyesha kuwajali watoto hawa hivyo imefika kipindi na sisi tuone jukumu hili ni letu" alisema Mary.
Hayo aliyasema katika ziara yake ya kushukuru kwa kuchaguliwa katika nafasi hiyo na pia kuangalia uhai wa jumuia ya UWT na Chama Cha Mapinduzi kwa jumla.
Ameongozana na Katibu wa UWT mkoa wa Mbeya, Mwanaidy Mbisha na Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji UWT mkoani hapa, Florence Mwakanyamale.
Mary alisema mwanamke ndiye uhai wa jamii yoyote ile na ndio maana hata kwenye suala la uzazi wa Mpango iwapo mwanamke atakataa kushiriki ni wazi suala hilo halitawezekana.
Aliwataka wanawake mkoani Mbeya kuwajali na kuwathamini watioto yatima waliopo katika maeneo yao ili nao waweze kujiona siyo wanyonge kwa vile tu walipoteza wazazi wao wote wawili.Mjumbe huyo wa Baraza Kuu la UWT Taifa alisema:
"Hivyo nawaombeni mfanye mchakato wa bila upendeleo wowote ili niweze kupata mtoto yatima wa kike ambaye amefaulu mtihani lakini hana kabisa uwezo wa kusomeshwa sekondari".Aliongeza kuwa ukimgusa mtoto yatima ama mjane ni wazi unakuwa umemgusa Mwenyezi Mungu.
Mary alisema aliomba nafasi hiyo ili kuwatumikia wanawake wa mkoa wa Mbeya, katika kuwaletea maendeleo lakini hilo litafanikiwa iwapo nao watatoa ushirikiano wa dhati na kujenga umoja baina yao.
"Wanawake wa mkoa wa Mbeya na sisi umefika wakati tunatakiwa tuone wivu kwa wanawake wenzetu wa mikoa ya kaskazini ambao wanazidi kupiga hatua za kimaendeleo lakini sisi tunaendelea kupigana majungu na kutopendana" alisema Mary.
Hivyo amezitaka kamati za Utekelezaji za UWT za wilaya hizo, kufanya mchakato bila ya upendeleo ili kuwapata watoto hao yatima ambao yeye atawajibika kuwalipia ada na mahitaji yote muhimu katika sekondari za kata.
"Jukumu la kuwalea watoto hawa yatima ni letu sisi wanawake wote...serikali na taifa kwa jumla wameonyesha kuwajali watoto hawa hivyo imefika kipindi na sisi tuone jukumu hili ni letu" alisema Mary.
Hayo aliyasema katika ziara yake ya kushukuru kwa kuchaguliwa katika nafasi hiyo na pia kuangalia uhai wa jumuia ya UWT na Chama Cha Mapinduzi kwa jumla.
Ameongozana na Katibu wa UWT mkoa wa Mbeya, Mwanaidy Mbisha na Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji UWT mkoani hapa, Florence Mwakanyamale.
Mary alisema mwanamke ndiye uhai wa jamii yoyote ile na ndio maana hata kwenye suala la uzazi wa Mpango iwapo mwanamke atakataa kushiriki ni wazi suala hilo halitawezekana.
Aliwataka wanawake mkoani Mbeya kuwajali na kuwathamini watioto yatima waliopo katika maeneo yao ili nao waweze kujiona siyo wanyonge kwa vile tu walipoteza wazazi wao wote wawili.Mjumbe huyo wa Baraza Kuu la UWT Taifa alisema:
"Hivyo nawaombeni mfanye mchakato wa bila upendeleo wowote ili niweze kupata mtoto yatima wa kike ambaye amefaulu mtihani lakini hana kabisa uwezo wa kusomeshwa sekondari".Aliongeza kuwa ukimgusa mtoto yatima ama mjane ni wazi unakuwa umemgusa Mwenyezi Mungu.
Mary alisema aliomba nafasi hiyo ili kuwatumikia wanawake wa mkoa wa Mbeya, katika kuwaletea maendeleo lakini hilo litafanikiwa iwapo nao watatoa ushirikiano wa dhati na kujenga umoja baina yao.
"Wanawake wa mkoa wa Mbeya na sisi umefika wakati tunatakiwa tuone wivu kwa wanawake wenzetu wa mikoa ya kaskazini ambao wanazidi kupiga hatua za kimaendeleo lakini sisi tunaendelea kupigana majungu na kutopendana" alisema Mary.
Sunday, July 19, 2009
MWANAMKE AJIUA KWA KUJIRUSHA KUTOKA GHOROFANI
MWANAMKE aliyekuwa ametoka kujifungua, Hellena Kambanga (29) amejiua baada ya kujirusha dirishani akiwa ghorofani ya tatu, hospitali ya Rufani Mbeya, kitengo cha Wazazi Meta, alikokuwa amelazwa.
Imeelezwa kuwa Hellena alijirusha kutoka wadi namba nne iliyopo ghorofani, saa 11:00 asubuhi, mara baada ya kumalizia dripu ya damu aliyokuwa ameongezewa mwilini baada kuishiwa wakati wa kujifungua.
Akithibitisha tukio hilo jana, mdogo wa marehemu ambaye ni mwanafunzi wa chuo cha IFM Dar es Salaam, akiwa mwaka wa pili aliyejitambulisha kwa jina la Shida Kambanga, alisema marehemu ameacha mtoto huyo ambaye ana umri wa wiki mbili sasa.
Shida alikuwa akitoa maelezo hayo kwa kushirikiana na mdogo wake alijitambulisha kuwa anaitwa Amina.
Shida alisema hiyo ilikuwa ni mimba ya pili, kwa dada yake huyo ambaye alikuwa anaishi eneo la Mbagala jijini Dar es Salaam na mumewe, na alikuwa amekuja mkoani Mbeya ambako ndipo alipozaliwa kusalimia ndugu na jamaa.
“Alikuwa anaumwa homa za mara kwa mara ambazo ni za kawaida kwa mwanamke mjamzito…siku za kujifungua zilipotimia alifanikiwa kujifungua salama kitengo cha Wazazi Meta, lakini alikuwa amepungukiwa damu mwilini” alisema Shida.
Aliongeza kuwa mara baada ya kuongezewa damu, marehemu Hellena alikuwa anaendelea vizuri na siku moja baada ya kumaliza dripu ya mwisho ya damu aliyokuwa amewekewa ndio aliamua kujirusha kutoka dirisha.
Kwa mujibu wa mdogo huyo wa marehemu, inaonyesha kuwa Hellena hakuwa na uangalizi wowote kutoka kwa wauguzi wa zamu siku hiyo hali iliyopelekea aweze kuamka muda huo wa alfajiri, kupanda dirishani na kujirusha hadi chini.
Alifafanua kuwa kutokana na utaratibu uliopo kitengo hicho cha Wazazi Meta, ndugu huwa hawaruhusiwi kulala na mgonjwa hivyo walipofika saa 12:00 asubuhi kumjulia hali ndipo walipopewa taarifa hizo.
Shida alisema:”Mara baada ya kujirusha kutoka juu ghorofani, dada alipata majeraha ya ndani kwa ndani mwilini na alikuwa akilalamika maumivu makali ya mgongo hali iliyopelekea ahamishiwe hospitali ya Rufani Mbeya kwa matibabu zaidi”.
Aliongeza kuwa Hellena alifariki dunia siku ya pili tangu afikishwe hospitalini hapo, na tayari amezikwa katika makaburi ya Mianzini yaliyopo eneo la Nzovwe jijini Mbeya, ambapo mtoto wake mchanga amechukuliwa na mama yao kwenda kulelewa Dar es Salaam.
Naye Mkurugenzi wa hospitali ya Rufani Mbeya, Dk. Eliuter Samky alipofuatwa ili kutoa ufafanuzi kuhusiana na tukio hilo, alisema hana taarifa zozote hivyo hawezi kuliongelea suala hilo.
“Mimi sina taarifa kuhusu kutokea kwa tukio hilo, hivyo siwezi kutoa maelezo yoyote…ningekuwa nimepewa taarifa ningesema, kifupi hakuna tukio kama hilo hospitalini hapa” alisema Dk.Samky.
Imeelezwa kuwa Hellena alijirusha kutoka wadi namba nne iliyopo ghorofani, saa 11:00 asubuhi, mara baada ya kumalizia dripu ya damu aliyokuwa ameongezewa mwilini baada kuishiwa wakati wa kujifungua.
Akithibitisha tukio hilo jana, mdogo wa marehemu ambaye ni mwanafunzi wa chuo cha IFM Dar es Salaam, akiwa mwaka wa pili aliyejitambulisha kwa jina la Shida Kambanga, alisema marehemu ameacha mtoto huyo ambaye ana umri wa wiki mbili sasa.
Shida alikuwa akitoa maelezo hayo kwa kushirikiana na mdogo wake alijitambulisha kuwa anaitwa Amina.
Shida alisema hiyo ilikuwa ni mimba ya pili, kwa dada yake huyo ambaye alikuwa anaishi eneo la Mbagala jijini Dar es Salaam na mumewe, na alikuwa amekuja mkoani Mbeya ambako ndipo alipozaliwa kusalimia ndugu na jamaa.
“Alikuwa anaumwa homa za mara kwa mara ambazo ni za kawaida kwa mwanamke mjamzito…siku za kujifungua zilipotimia alifanikiwa kujifungua salama kitengo cha Wazazi Meta, lakini alikuwa amepungukiwa damu mwilini” alisema Shida.
Aliongeza kuwa mara baada ya kuongezewa damu, marehemu Hellena alikuwa anaendelea vizuri na siku moja baada ya kumaliza dripu ya mwisho ya damu aliyokuwa amewekewa ndio aliamua kujirusha kutoka dirisha.
Kwa mujibu wa mdogo huyo wa marehemu, inaonyesha kuwa Hellena hakuwa na uangalizi wowote kutoka kwa wauguzi wa zamu siku hiyo hali iliyopelekea aweze kuamka muda huo wa alfajiri, kupanda dirishani na kujirusha hadi chini.
Alifafanua kuwa kutokana na utaratibu uliopo kitengo hicho cha Wazazi Meta, ndugu huwa hawaruhusiwi kulala na mgonjwa hivyo walipofika saa 12:00 asubuhi kumjulia hali ndipo walipopewa taarifa hizo.
Shida alisema:”Mara baada ya kujirusha kutoka juu ghorofani, dada alipata majeraha ya ndani kwa ndani mwilini na alikuwa akilalamika maumivu makali ya mgongo hali iliyopelekea ahamishiwe hospitali ya Rufani Mbeya kwa matibabu zaidi”.
Aliongeza kuwa Hellena alifariki dunia siku ya pili tangu afikishwe hospitalini hapo, na tayari amezikwa katika makaburi ya Mianzini yaliyopo eneo la Nzovwe jijini Mbeya, ambapo mtoto wake mchanga amechukuliwa na mama yao kwenda kulelewa Dar es Salaam.
Naye Mkurugenzi wa hospitali ya Rufani Mbeya, Dk. Eliuter Samky alipofuatwa ili kutoa ufafanuzi kuhusiana na tukio hilo, alisema hana taarifa zozote hivyo hawezi kuliongelea suala hilo.
“Mimi sina taarifa kuhusu kutokea kwa tukio hilo, hivyo siwezi kutoa maelezo yoyote…ningekuwa nimepewa taarifa ningesema, kifupi hakuna tukio kama hilo hospitalini hapa” alisema Dk.Samky.
RAS MKOA WA MBEYA AWATIMUA WAANDISHI WA HABARI
WAANDISHI wa habari kutoka vyombo mbalimbali, jana walishindwa kuhudhuria kikao cha Mkuu wa mkoa wa Mbeya,John Mwakipesile na Jaji Mkuu Agustino Ramadhan, baada ya Katibu Tawala wa mkoa (RAS), Beatha Swai kuwazuia mlangoni.
Tukio hilo lilitokea jana saa 3:00 asubuhi, mara baada ya waandishi wa habari kufika hapo kuitikia wito uliotolewa na Ofisa Uhusiano wa Mahakama Kuu (PRO), Nurdin Ndimbe kuhudhuria kikao hicho bila kukosa.
Waandishi hao zaidi ya saba, walifika ofisi hizo muda waliotakiwa na walipotaka kuingia katika kikao hicho, walikutana nja kikwazo hicho kutoka kwa RAS Beatha akishirikiana na Msaidizi wa Mkuu wa mkoa (DPS), ambaye jina lake halikuweza kujulikana.
Hatua hiyo ni tofauti na taarifa iliyotolewa na Afisa Uhusiano huyo wa Mahakama Kuu, Ndimbe ambaye aliwaeleza waandishi kuwa wanatakiwa kushiriki kikamilifu katika ziara ya Jaji kuanzia ofisi ya Mkuu wa Mkoa na kwingineko.
Vikwazo hivyo vilianzia kwa Msaidizi wa Mkuu wa Mkoa (DPS) ambaye aliwaeleza waandishi kuwa hakuwa na taarifa ya waandishi kutakiwa kuingia katika ofisi hizo na kuwataka watoke nje wakasubiri.
Hata hivyo juhudi za waandishi kujaribu kumuelekeza umuhimu wa wao kuhudhuria mazungumzo baina ya Mkuu wa Mkoa na Jaji Mkuu ziligonga mwamba baada ya Katibu Tawala, Beatha kusimama mlangoni na kuwazuia baadhi ya waandishi kwa kuwasukumia nje ya ofisi.
Baada ya kuwepo kwa kutoelewana baina ya waandishi, msaidizi wa mkuu wa mkoa na Katibu Tawala, Afisa habari wa mahakama, Ndimbe aliwaomba waandishi wasubiri nje huku naye akiwa haelewi kinachoendelea na sababu za waandishi kuzuiwa.
Baadhi ya waandishi walilalamikia kitendo cha Swai kwa madai kuwa yeye pamoja Msaidizi wa Mkuu wa Mkoa wamekuwa na tabia ya kuwazuia waandishi na wakati mwingine kudai hawaruhusu kumuona Mkuu wa Mkoa bila ya kuwa na miadi naye.
Lakini tukio hilo liliwasikitisha waandishi wengi kwani ni tofauti na ushirikiano mkubwa alionao Mwakipesile tangu ateuliwe kushika nafasi hiyo, kwani amekuwa akiwataka waandishi kumuona muda wowote wanapokuwa na jambo la dhalura.
“Hawa wanatushangaza, sisi kumuona Mkuu wa Mkoa lazima tuwe na miadi hata kama kuna jambo la dharura, lakini ofisi ya Mkuu wa Mkoa huwa inaita waandishi bila ya kuweka miadi, hii ni ajabu kabisa” alisema.
Jaji Ramadhani jana alikuwa Mkoani Mbeya kwa ziara ya siku moja ambapo aliwasili Mkoani Mbeya akitokea Mkoani Rukwa.
Tukio hilo lilitokea jana saa 3:00 asubuhi, mara baada ya waandishi wa habari kufika hapo kuitikia wito uliotolewa na Ofisa Uhusiano wa Mahakama Kuu (PRO), Nurdin Ndimbe kuhudhuria kikao hicho bila kukosa.
Waandishi hao zaidi ya saba, walifika ofisi hizo muda waliotakiwa na walipotaka kuingia katika kikao hicho, walikutana nja kikwazo hicho kutoka kwa RAS Beatha akishirikiana na Msaidizi wa Mkuu wa mkoa (DPS), ambaye jina lake halikuweza kujulikana.
Hatua hiyo ni tofauti na taarifa iliyotolewa na Afisa Uhusiano huyo wa Mahakama Kuu, Ndimbe ambaye aliwaeleza waandishi kuwa wanatakiwa kushiriki kikamilifu katika ziara ya Jaji kuanzia ofisi ya Mkuu wa Mkoa na kwingineko.
Vikwazo hivyo vilianzia kwa Msaidizi wa Mkuu wa Mkoa (DPS) ambaye aliwaeleza waandishi kuwa hakuwa na taarifa ya waandishi kutakiwa kuingia katika ofisi hizo na kuwataka watoke nje wakasubiri.
Hata hivyo juhudi za waandishi kujaribu kumuelekeza umuhimu wa wao kuhudhuria mazungumzo baina ya Mkuu wa Mkoa na Jaji Mkuu ziligonga mwamba baada ya Katibu Tawala, Beatha kusimama mlangoni na kuwazuia baadhi ya waandishi kwa kuwasukumia nje ya ofisi.
Baada ya kuwepo kwa kutoelewana baina ya waandishi, msaidizi wa mkuu wa mkoa na Katibu Tawala, Afisa habari wa mahakama, Ndimbe aliwaomba waandishi wasubiri nje huku naye akiwa haelewi kinachoendelea na sababu za waandishi kuzuiwa.
Baadhi ya waandishi walilalamikia kitendo cha Swai kwa madai kuwa yeye pamoja Msaidizi wa Mkuu wa Mkoa wamekuwa na tabia ya kuwazuia waandishi na wakati mwingine kudai hawaruhusu kumuona Mkuu wa Mkoa bila ya kuwa na miadi naye.
Lakini tukio hilo liliwasikitisha waandishi wengi kwani ni tofauti na ushirikiano mkubwa alionao Mwakipesile tangu ateuliwe kushika nafasi hiyo, kwani amekuwa akiwataka waandishi kumuona muda wowote wanapokuwa na jambo la dhalura.
“Hawa wanatushangaza, sisi kumuona Mkuu wa Mkoa lazima tuwe na miadi hata kama kuna jambo la dharura, lakini ofisi ya Mkuu wa Mkoa huwa inaita waandishi bila ya kuweka miadi, hii ni ajabu kabisa” alisema.
Jaji Ramadhani jana alikuwa Mkoani Mbeya kwa ziara ya siku moja ambapo aliwasili Mkoani Mbeya akitokea Mkoani Rukwa.
MAREHEMU JOSEPH HILL WA KUNDI LA CULTURE
MUZIKI wa Reggae umetokea kujipatia mashabiki na wapenzi wengi duniani kutokana na mashairi yake siku zote kugusa maisha halisi ya binadamu.
Kifupi unalenga ukweli halisiNa ndio maana leo hii unapomtaja mwanamuziki mahiri na mfalme wa Reggae, marehemu Robert Nesta Marley maarufu zaidi kwa jina la Bob Marley, hata mtoto mdogo wa miaka mitano hawezi kupata kigugumizi kukueleza kuwa anazipenda nyimbo zake.
Lakini pia kuna waimbaji wengine mahiri wa muziki huu ambao mara nyingi wanamuziki wake hupenda kuziachia nywele zao kichwani kuwa ndefu yaani kufuga Rasta, kama kitambulisho cha muziki huo.Hata hivyo kuna wanamuziki wengine wa muziki huu hawana Rasta.
Mmoja wa waimbaji hao ambao nao wamejipatia sifa na kuutangaza muziki huu wa Reggae na kupelekea kujipatia umaarufu duniani ni marehemu Joseph Hill, kiongozi wa kundi la Culture.
Hill alikuwa ni kiongozi wa kundi hilo la Culture lililokuwa linaundwa na wasanii wakongwe ambalo lilitokea kujipatia sifa kubwa nchini Jamaika na duniani kwa jumla.
Mnamo Agosti 19, mwaka 2006, wapenzi na mashabiki wa reggae walipatwa na mshituko mkubwa kufuatia kifo cha msanii huyu mahiri aliyekuwa na sauti ya kipekee iliyoweza kumtoa nyoka pangani.
Hill alikutwa na mauti mjini Berlin nchi Ujerumani, baada ya kuugua ghafla akiwa katikati ya ziara ya kimuziki barani Ulaya na kundi na kundi lake la Culture.
Kutokana na mchango wake mkubwa Hill alitunukiwa tuzo nyingi ikiwemo ile iliyojulikana kama ‘Jamaika Reggae Walk of Fame and a 2005 Independence Award’ aliyotunukiwa na Waziri Mkuu wa Jamaika.
Kifupi ni kuwa unapokuwa unawaongelea magwiji wa muziki wa Reggae waliowahi kutokea hapa duniani, basi ni wazi lazima utalitaja pia jina la Hill kuwa miongoni mwao na hilo halina ubishi.
Kundi la Culture lililoundwa mnamo mwaka 1976, na kujizolea umaarufu mkubwa huku likijulikana pia kama Mitume ya Afrika, lilikuwa linaundwa na wasanii wakali wakiwemo Joseph Hill, Albert Walker na Kenneth Dayes.
Hill alikuwa ni msanii pekee ndani ya kundi hilo aliyekuwa na uzoefu wa mambo ya Studio, baada ya kuwa amewahi kufanya kazi katika studio ya Coxone Dodd's akiwa mmoja wa waandaaji wa nyimbo za kundi lililoitwa Soul Defenders mwanzoni mwa miaka ya 1970.
Muda mfupi baada ya kuanzishwa kwa kundi la Culture, lilianza kufanya kazi na mtayarishaji wa muziki aitwaye Joe Gibbs akiwa na Injinia wake Errol Thompson. Wakiwa na Gibbs walifanikiwa kurekodi albamu mbili zilizojipatia umaarufu mkubwa.
Mara baada ya kutolewa kwa albamu hizi mbili ambazo zilikuwa na mtazamo mchanganyiko wa historia ya Jamaika, na mtazamo mpya wa mabadiliko ya hali ya hewa. Baada ya kupata mafaniko wakiwa na Gibbs, kundi hilo lilihama na kwenda kufanya kazi na mtayarishaji mwingine aliyejulikana kwa jina la Sonia Pottinger.
Culture pia walianza kufanya kazi na wanamuziki wengine mahiri waliopo kama Robbie Shakespeare, Sly Dunbar, Ansel Collins na Cedric Brooks.Kampuni ya kurekodi ya Virgin ilichukua albamu yao iliyowafanya (Culture) , wazidi kuwa maarufu na kupata mashabiki hadi nje ya Jamaika.
Mwaka 1982 waimbaji watatu wa kundi hilo waliojiondoa na kuanza maisha yao kivyao, ambapo Joseph Hill aliendelea kutumia jina la Culture lakini baadaye mwaka 1986 waliungana tena na kurekodi albamu mbili zilizojizolea umaarufu mkubwa za 'Culture in Culture' na 'Culture at Work'.
Baadaye mwaka 1993 Kenneth Dayes aliondoka katika kundi na kubadiliwa kwa muda na muimbaji kutoka kundi la Dub Mystic, ambaye.
Wakiwa na Dub Mystic, Culture walifikia mafaniko ya juu kimuziki baada ya kuachia albamu za 'One Stone' na ‘Trust Me' na live albamu iliyokwenda kwa jina la 'Cultural Livity'. Baada ya kundi hilo kudumu kwa muda wa miaka 27,Joseph Hill na wenzake hawakuonyesha dalili za kushuka kiwango chao kimuziki.
Kundi la Culture liliendelea kuwa imara likiwa na msimamo wa kudumisha ukweli kuhusu asili ya muziki wa Reggae lakini pia muda mwingine likiingiza milio na sauti mpya katika muziki wao.
Wanamuziki wa kundi la Culture wameonyesha njia kuwa ni moja ya kundi bora la muziki wa Reggae lililoweza kutawala kuanzia katika utunzi wa mashairi ya albamu albamu zao hadi katika kulitawala jukwaa.
Kifupi unalenga ukweli halisiNa ndio maana leo hii unapomtaja mwanamuziki mahiri na mfalme wa Reggae, marehemu Robert Nesta Marley maarufu zaidi kwa jina la Bob Marley, hata mtoto mdogo wa miaka mitano hawezi kupata kigugumizi kukueleza kuwa anazipenda nyimbo zake.
Lakini pia kuna waimbaji wengine mahiri wa muziki huu ambao mara nyingi wanamuziki wake hupenda kuziachia nywele zao kichwani kuwa ndefu yaani kufuga Rasta, kama kitambulisho cha muziki huo.Hata hivyo kuna wanamuziki wengine wa muziki huu hawana Rasta.
Mmoja wa waimbaji hao ambao nao wamejipatia sifa na kuutangaza muziki huu wa Reggae na kupelekea kujipatia umaarufu duniani ni marehemu Joseph Hill, kiongozi wa kundi la Culture.
Hill alikuwa ni kiongozi wa kundi hilo la Culture lililokuwa linaundwa na wasanii wakongwe ambalo lilitokea kujipatia sifa kubwa nchini Jamaika na duniani kwa jumla.
Mnamo Agosti 19, mwaka 2006, wapenzi na mashabiki wa reggae walipatwa na mshituko mkubwa kufuatia kifo cha msanii huyu mahiri aliyekuwa na sauti ya kipekee iliyoweza kumtoa nyoka pangani.
Hill alikutwa na mauti mjini Berlin nchi Ujerumani, baada ya kuugua ghafla akiwa katikati ya ziara ya kimuziki barani Ulaya na kundi na kundi lake la Culture.
Kutokana na mchango wake mkubwa Hill alitunukiwa tuzo nyingi ikiwemo ile iliyojulikana kama ‘Jamaika Reggae Walk of Fame and a 2005 Independence Award’ aliyotunukiwa na Waziri Mkuu wa Jamaika.
Kifupi ni kuwa unapokuwa unawaongelea magwiji wa muziki wa Reggae waliowahi kutokea hapa duniani, basi ni wazi lazima utalitaja pia jina la Hill kuwa miongoni mwao na hilo halina ubishi.
Kundi la Culture lililoundwa mnamo mwaka 1976, na kujizolea umaarufu mkubwa huku likijulikana pia kama Mitume ya Afrika, lilikuwa linaundwa na wasanii wakali wakiwemo Joseph Hill, Albert Walker na Kenneth Dayes.
Hill alikuwa ni msanii pekee ndani ya kundi hilo aliyekuwa na uzoefu wa mambo ya Studio, baada ya kuwa amewahi kufanya kazi katika studio ya Coxone Dodd's akiwa mmoja wa waandaaji wa nyimbo za kundi lililoitwa Soul Defenders mwanzoni mwa miaka ya 1970.
Muda mfupi baada ya kuanzishwa kwa kundi la Culture, lilianza kufanya kazi na mtayarishaji wa muziki aitwaye Joe Gibbs akiwa na Injinia wake Errol Thompson. Wakiwa na Gibbs walifanikiwa kurekodi albamu mbili zilizojipatia umaarufu mkubwa.
Mara baada ya kutolewa kwa albamu hizi mbili ambazo zilikuwa na mtazamo mchanganyiko wa historia ya Jamaika, na mtazamo mpya wa mabadiliko ya hali ya hewa. Baada ya kupata mafaniko wakiwa na Gibbs, kundi hilo lilihama na kwenda kufanya kazi na mtayarishaji mwingine aliyejulikana kwa jina la Sonia Pottinger.
Culture pia walianza kufanya kazi na wanamuziki wengine mahiri waliopo kama Robbie Shakespeare, Sly Dunbar, Ansel Collins na Cedric Brooks.Kampuni ya kurekodi ya Virgin ilichukua albamu yao iliyowafanya (Culture) , wazidi kuwa maarufu na kupata mashabiki hadi nje ya Jamaika.
Mwaka 1982 waimbaji watatu wa kundi hilo waliojiondoa na kuanza maisha yao kivyao, ambapo Joseph Hill aliendelea kutumia jina la Culture lakini baadaye mwaka 1986 waliungana tena na kurekodi albamu mbili zilizojizolea umaarufu mkubwa za 'Culture in Culture' na 'Culture at Work'.
Baadaye mwaka 1993 Kenneth Dayes aliondoka katika kundi na kubadiliwa kwa muda na muimbaji kutoka kundi la Dub Mystic, ambaye.
Wakiwa na Dub Mystic, Culture walifikia mafaniko ya juu kimuziki baada ya kuachia albamu za 'One Stone' na ‘Trust Me' na live albamu iliyokwenda kwa jina la 'Cultural Livity'. Baada ya kundi hilo kudumu kwa muda wa miaka 27,Joseph Hill na wenzake hawakuonyesha dalili za kushuka kiwango chao kimuziki.
Kundi la Culture liliendelea kuwa imara likiwa na msimamo wa kudumisha ukweli kuhusu asili ya muziki wa Reggae lakini pia muda mwingine likiingiza milio na sauti mpya katika muziki wao.
Wanamuziki wa kundi la Culture wameonyesha njia kuwa ni moja ya kundi bora la muziki wa Reggae lililoweza kutawala kuanzia katika utunzi wa mashairi ya albamu albamu zao hadi katika kulitawala jukwaa.
TOENI TAARIFA NA KUORODHESHA VIUATILIFU CHAKAVU
MKAGUZI wa mazao ya kilimo kutoka Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Damian Gasana, amewataka wananchi wa mikoa ya kanda za juu kusini, kutoa taarifa na kuorodhesha viuatilifu chakavu.
Alisema viuatilifu hivyo ambavyo vina athari kwa binadamu na mazingira vitakusanywa na watalaamu maalumu.
Gasana alisema kipindi cha mwaka 1997/1998, Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), lilifanya tathimini na kubaini kuwepo kwa tani 1,000 za viuatilifu na tani nyingine 200 za madawa ya chakavu ya mifugo.Taka hizo zimeonekana katika maeneo yasiyopungua 325 nchini kote.
Hayo aliyasema jana wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelezea mradi wa Africa Stockpiles ambao una mkakati wa kukusanya viuatilifu hivyo kwa mikoa ya kanda hii.
Gasana wananchi wote wanawajibika kutoa taarifa sahihi za uwepo wa viuatilifu chakavu kwa mabwana shamba na ofisi ya kilimo ya wilaya ambapo alisema kuwa wananchi hawatakiwi kushika wala kuhamisha viuatirifu na kwamba kazi hiyo itafanywa na wataalamu maalumu waliofundishwa.
Alisema kuwa shughuli ya kutoa taarifa kuhusu viuatilifuy chakavu ni hiyari na kwamba hakuna hatua zozote za kisheria zitakazochukuliwa kwa wananchi watakaotoa taarifa juu ya uwepo wa viuatilifu, “viuatilifu ni neon linalotumika badala ya neno la dawa za kilimo”.
Alivitaja baada ya viuatilifu chakavu kuwa ni vyote vilivyoisha muda wake, vilivyopigwa marufuku kutumika nchini kisheria, bidhaa za viuatirifu zilizopondeka na kuharibika pamoja na vyombo au vitu vilivyoathirika au kuchafuliwa na viatilifu hivyo.
Aidha, Gasana alisema kuwa hiyo nafasi pekee ya kuisafisha nchi kuondokana na sumu zilizolundikana ambapo alisema kuwa ni jukumu la kila mwananchi kushiriki kutoa taarifa ili viatilifu hivyo viondolewe katika makazi ya wananchi pamoja na kuondokana na vyanzo vya uharibifu wa mazingira.
Alisema viuatilifu hivyo ambavyo vina athari kwa binadamu na mazingira vitakusanywa na watalaamu maalumu.
Gasana alisema kipindi cha mwaka 1997/1998, Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), lilifanya tathimini na kubaini kuwepo kwa tani 1,000 za viuatilifu na tani nyingine 200 za madawa ya chakavu ya mifugo.Taka hizo zimeonekana katika maeneo yasiyopungua 325 nchini kote.
Hayo aliyasema jana wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelezea mradi wa Africa Stockpiles ambao una mkakati wa kukusanya viuatilifu hivyo kwa mikoa ya kanda hii.
Gasana wananchi wote wanawajibika kutoa taarifa sahihi za uwepo wa viuatilifu chakavu kwa mabwana shamba na ofisi ya kilimo ya wilaya ambapo alisema kuwa wananchi hawatakiwi kushika wala kuhamisha viuatirifu na kwamba kazi hiyo itafanywa na wataalamu maalumu waliofundishwa.
Alisema kuwa shughuli ya kutoa taarifa kuhusu viuatilifuy chakavu ni hiyari na kwamba hakuna hatua zozote za kisheria zitakazochukuliwa kwa wananchi watakaotoa taarifa juu ya uwepo wa viuatilifu, “viuatilifu ni neon linalotumika badala ya neno la dawa za kilimo”.
Alivitaja baada ya viuatilifu chakavu kuwa ni vyote vilivyoisha muda wake, vilivyopigwa marufuku kutumika nchini kisheria, bidhaa za viuatirifu zilizopondeka na kuharibika pamoja na vyombo au vitu vilivyoathirika au kuchafuliwa na viatilifu hivyo.
Aidha, Gasana alisema kuwa hiyo nafasi pekee ya kuisafisha nchi kuondokana na sumu zilizolundikana ambapo alisema kuwa ni jukumu la kila mwananchi kushiriki kutoa taarifa ili viatilifu hivyo viondolewe katika makazi ya wananchi pamoja na kuondokana na vyanzo vya uharibifu wa mazingira.
WASICHANA WA NZOVWE JIJINI MBEYA WANAPENDA KUPIGWA 'MTUNGO'
WASICHANA wa eneo la Nzovwe, jijini Mbeya wametuhumiwa kushinda katika klabu za kuuza pombe za kienyeji, hasa nyakati za usiku na kufanya mapenzi na wanaume zaidi ya mmoja kwa siku kwa tamaa ya fedha.
Imedaiwa tabia ya wasichana hao, kupenda kuomba fedha kwa wanaume tofauti wanaokuwa wanakunywa pombe katika klabu hizo, hupelekea mwisho wa siku wakubali kufanya ngono zembe na mwanaume zaidi ya mmoja.
Hayo yalisemwa kwa nyakati tofauti na wakazi wa eneo hilo, katika mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Vijana Mabalozi Watanzania wanaoishi na virusi vinavyosababisha Ukimwi (TAYOPA).
Mkoa wa Mbeya ni wa nne kutembelewa na TAYOPA ambao wapo kuutambulisha mradi wao uitwao 'Vijana Tuzinduke ili kujikinga na Ukimwi'.
Mikoa mingine iliyotembelwa ni Dar es Salaam, Lindi, Mtwara na baadaye wataelekea Ruvuma.
Mradi huo unafadhiriwa kwa pamoja na na shirika la Afya la Kimataifa (FHL) na kituo cha televisheni cha MTV cha nchini Marekani.
Wakizungumza wakazi hao wa Nzovwe walisema kuwa wasichana wa kike wa maeneo hayo, wamekuwa wanaendekeza sana kuombas fedha kwa wanaume katika klabu za pombe nyakati za usiku hali inayopelekea kuwepo kwa ngono zembe na wanaume wengi kwa siku.
Mkazi aliyejitambulisha kwa jina moja la Joyce alisema hali hiyo imefanya wasichana hao ambao bado ni wanafunzi wa shule za msingi, kupenda kufanya ngono na wanaume wengi mtindo ambao ni maarufu zaidi kwa jina la 'Mtungo'.
"Huku unaweza kumuona msichana ukadhani ni mdogo, kumbe anao uwezo wa kufanya mapenzi na zaidi ya mwanaume mmoja kwa siku...kimsingi hali inatisha kwani huwa wanafanya ngono zembe".Joyce alisema
Naye Mwenyekiti wa TAYOPA, John Solanya, alisema yeye alipimwa afya na kugundulika kuwa na maambukizi ya virusi vya Ukimwi tangu mwaka 1995, ambapo alijitangaza.
Solanya alisema kuwa anaishi na mke pamoja na mtoto mmoja ambao hawajaambukizwa Ukimwi, na kuwa tangu mwaka huu hajawahi kuumwa hadi kufikia hatua ya kulazwa hospitalini kwani amekuwa anazingatia ushauri anaopewa.
"Nina mke na mtoto ambao wao hana maambukizi ya Ukimwi... ninapotaka 'chakula cha usiku' kutoka kwa mke wangu huwa tunatumia kondomu" alisema Solanya.
Naye Fitina Mohamed, ambaye pia anaishi na virusi vya Ukimwi, alisema ni wengi wanayo maambukizi ya ugonjwa huo lakini huwezi kuwatambua kwa kuwaangalia kwa macho bali hadi wapime na kujitangaza.
Alihoji kuwa ni nani ambaye angeweza kuwatambua kuwa yeye ama mwenzake Solanya wanaishi na virusi vya Ukimwi iwapo wangeamua kukaa kimya mara baada ya kupima afya zao, na kuendelea kukubali kufanya ngono zembe.
Tukio hilo lilipambwa na burudani kutoka kwa wasanii Fareed Kubanda 'Fid Q. na mshindi wa Bongo Star Search, Jumanne Idd ambao waliweza kutoa burudani kabambe na kuwa kifutio kikubwa katika mkutano huo.
Imedaiwa tabia ya wasichana hao, kupenda kuomba fedha kwa wanaume tofauti wanaokuwa wanakunywa pombe katika klabu hizo, hupelekea mwisho wa siku wakubali kufanya ngono zembe na mwanaume zaidi ya mmoja.
Hayo yalisemwa kwa nyakati tofauti na wakazi wa eneo hilo, katika mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Vijana Mabalozi Watanzania wanaoishi na virusi vinavyosababisha Ukimwi (TAYOPA).
Mkoa wa Mbeya ni wa nne kutembelewa na TAYOPA ambao wapo kuutambulisha mradi wao uitwao 'Vijana Tuzinduke ili kujikinga na Ukimwi'.
Mikoa mingine iliyotembelwa ni Dar es Salaam, Lindi, Mtwara na baadaye wataelekea Ruvuma.
Mradi huo unafadhiriwa kwa pamoja na na shirika la Afya la Kimataifa (FHL) na kituo cha televisheni cha MTV cha nchini Marekani.
Wakizungumza wakazi hao wa Nzovwe walisema kuwa wasichana wa kike wa maeneo hayo, wamekuwa wanaendekeza sana kuombas fedha kwa wanaume katika klabu za pombe nyakati za usiku hali inayopelekea kuwepo kwa ngono zembe na wanaume wengi kwa siku.
Mkazi aliyejitambulisha kwa jina moja la Joyce alisema hali hiyo imefanya wasichana hao ambao bado ni wanafunzi wa shule za msingi, kupenda kufanya ngono na wanaume wengi mtindo ambao ni maarufu zaidi kwa jina la 'Mtungo'.
"Huku unaweza kumuona msichana ukadhani ni mdogo, kumbe anao uwezo wa kufanya mapenzi na zaidi ya mwanaume mmoja kwa siku...kimsingi hali inatisha kwani huwa wanafanya ngono zembe".Joyce alisema
Naye Mwenyekiti wa TAYOPA, John Solanya, alisema yeye alipimwa afya na kugundulika kuwa na maambukizi ya virusi vya Ukimwi tangu mwaka 1995, ambapo alijitangaza.
Solanya alisema kuwa anaishi na mke pamoja na mtoto mmoja ambao hawajaambukizwa Ukimwi, na kuwa tangu mwaka huu hajawahi kuumwa hadi kufikia hatua ya kulazwa hospitalini kwani amekuwa anazingatia ushauri anaopewa.
"Nina mke na mtoto ambao wao hana maambukizi ya Ukimwi... ninapotaka 'chakula cha usiku' kutoka kwa mke wangu huwa tunatumia kondomu" alisema Solanya.
Naye Fitina Mohamed, ambaye pia anaishi na virusi vya Ukimwi, alisema ni wengi wanayo maambukizi ya ugonjwa huo lakini huwezi kuwatambua kwa kuwaangalia kwa macho bali hadi wapime na kujitangaza.
Alihoji kuwa ni nani ambaye angeweza kuwatambua kuwa yeye ama mwenzake Solanya wanaishi na virusi vya Ukimwi iwapo wangeamua kukaa kimya mara baada ya kupima afya zao, na kuendelea kukubali kufanya ngono zembe.
Tukio hilo lilipambwa na burudani kutoka kwa wasanii Fareed Kubanda 'Fid Q. na mshindi wa Bongo Star Search, Jumanne Idd ambao waliweza kutoa burudani kabambe na kuwa kifutio kikubwa katika mkutano huo.
JAJI MKUU WA TANZANIA ALONGA KUHUSU WATUHUMIWA WA UFISADI.
JAJI Mkuu wa Tanzania, Agustino Ramadhan, amesema mahakama haiwatambui watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi kuwa mafisadi hadi pale ushahidi dhidi yao utakapopelekwa na kutiwa hatiani.
Alisema ni vyema wananchi wote wenye ushahidi unaoweza kuwatia hatiani watuhumiwa hao waupeleke mahakamani ili kesi hizo ziweze kukamilishwa lakini siyo kuingilia uhuru wa mahakama kwa kuilazimisha kuwatia hatiani.
“Tuleteeni ushahidi ili tuweze kuufanya kazi lakini hadi sasa hawa sisi mahakama tunawatambua kuwa ni watuhumiwa lakini siyo mafisadi…tukiruhusu kuingiliwa ni wazi uhuru wa mahakama utakuwa unachezewa” alisema Jaji Mkuu Ramadhan.
Jaji Mkuu Ramadhan ambaye ni Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Mahakama, aliyasema hayo wakati akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Mahakama wa wilaya zote na wale wa mkoa wa Mbeya, katika ukumbi wa Dk.Ali Shein.
Alisema umma unatakiwa usiiigilie mahakama katika utendaji wake wa kazi na kutoa mfano kuwa hata Yesu (Nabii Issa), alipopelekwa kwa Pilato ili amtie hatiani, Pilato alinawa mikono baada ya kuona kuwa mtu huyo hana hatia hivyo hawezi kumuhukumu kwa kuwa tu wayahudi wanataka ahukumiwe.
“Mfano huu ni mojawapo ya hofu ya uhuru wa mahakama unavyoweza kuingiliwa…na ndiyo maana Pilato alinawa mikono kuonyesha kuwa mahakama imemuona hana hatia hivyo haiwezi kumuhukumu pasipo kuwa na ushahidi” alisema Ramadhan.
Aliongeza kuwa hisia ya uhuru wa mahakama siyo ndio itamfanya Jaji Mkuu ashindwe kukaa na Rais Jakaya Kikwete, Waziri ama mkuu wa mkoa kwa madai atashindwa kufanya kazi yake ipasavyo.
Alisema:”Jaji Mkuu hawezi kumuingilia na kumuambia Jaji yeyote kuhusu nini cha kufanya kwa kesi iliyopo mbele yake, kwani Jaji ndie mwenye jukumu la kuiendesha kesi hiyo hivyo huwezi kumshika na vivyo hivyo umma nao unatakiwa usiingilie uhuru wa mahakama”.
Aidha, Jaji Mkuu Ramadhan alisema amekuwa anapokea barua nyingi kutoka kwa wabunge na wakuu wa wilaya nchini zikimtaka awahamishe mahakimu kutoka maeneo yao kwa kutuhumiwa kutowajibika katika utendaji wao wa kazi huku wengine wakituhumiwa kwa vitendo vya kupokea rushwa.
Alisema dawa ya tatizo hilo ipo mikononi wa Mtume hizo za Mahakama ambazo kazi yake kubwa ni kuhakikisha kuwa mahakimu wanakuwa na nidhamu na wanafanya kazi zao kwa kufuata misingi ya sheria iliyopo na siyo nje ya hapo.
Aliongeza kuwa kumhamisha hakimu kutoka sehemu moja kwenda nyingine siyo suluhisho, bali kinachotakiwa ni Kamati hizo kukutana mara kwa mara ili kuyafanyia kazi malalamiko wanayokuwa nayo kuhusu mahakimu katika maeneo yao.
Jaji Mkuu alisema:”Juhudi za Tume ni kushughulikia pia maslahi ya watumishi wote wa mahakama…ukiacha nidhamu kwa majaji na mahakimu, lakini pia kuna madhambi mengi yanafanywa na makarani pamoja na wahudumu wa mahakama zetu”.
Alisema ni vyema wananchi wote wenye ushahidi unaoweza kuwatia hatiani watuhumiwa hao waupeleke mahakamani ili kesi hizo ziweze kukamilishwa lakini siyo kuingilia uhuru wa mahakama kwa kuilazimisha kuwatia hatiani.
“Tuleteeni ushahidi ili tuweze kuufanya kazi lakini hadi sasa hawa sisi mahakama tunawatambua kuwa ni watuhumiwa lakini siyo mafisadi…tukiruhusu kuingiliwa ni wazi uhuru wa mahakama utakuwa unachezewa” alisema Jaji Mkuu Ramadhan.
Jaji Mkuu Ramadhan ambaye ni Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Mahakama, aliyasema hayo wakati akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Mahakama wa wilaya zote na wale wa mkoa wa Mbeya, katika ukumbi wa Dk.Ali Shein.
Alisema umma unatakiwa usiiigilie mahakama katika utendaji wake wa kazi na kutoa mfano kuwa hata Yesu (Nabii Issa), alipopelekwa kwa Pilato ili amtie hatiani, Pilato alinawa mikono baada ya kuona kuwa mtu huyo hana hatia hivyo hawezi kumuhukumu kwa kuwa tu wayahudi wanataka ahukumiwe.
“Mfano huu ni mojawapo ya hofu ya uhuru wa mahakama unavyoweza kuingiliwa…na ndiyo maana Pilato alinawa mikono kuonyesha kuwa mahakama imemuona hana hatia hivyo haiwezi kumuhukumu pasipo kuwa na ushahidi” alisema Ramadhan.
Aliongeza kuwa hisia ya uhuru wa mahakama siyo ndio itamfanya Jaji Mkuu ashindwe kukaa na Rais Jakaya Kikwete, Waziri ama mkuu wa mkoa kwa madai atashindwa kufanya kazi yake ipasavyo.
Alisema:”Jaji Mkuu hawezi kumuingilia na kumuambia Jaji yeyote kuhusu nini cha kufanya kwa kesi iliyopo mbele yake, kwani Jaji ndie mwenye jukumu la kuiendesha kesi hiyo hivyo huwezi kumshika na vivyo hivyo umma nao unatakiwa usiingilie uhuru wa mahakama”.
Aidha, Jaji Mkuu Ramadhan alisema amekuwa anapokea barua nyingi kutoka kwa wabunge na wakuu wa wilaya nchini zikimtaka awahamishe mahakimu kutoka maeneo yao kwa kutuhumiwa kutowajibika katika utendaji wao wa kazi huku wengine wakituhumiwa kwa vitendo vya kupokea rushwa.
Alisema dawa ya tatizo hilo ipo mikononi wa Mtume hizo za Mahakama ambazo kazi yake kubwa ni kuhakikisha kuwa mahakimu wanakuwa na nidhamu na wanafanya kazi zao kwa kufuata misingi ya sheria iliyopo na siyo nje ya hapo.
Aliongeza kuwa kumhamisha hakimu kutoka sehemu moja kwenda nyingine siyo suluhisho, bali kinachotakiwa ni Kamati hizo kukutana mara kwa mara ili kuyafanyia kazi malalamiko wanayokuwa nayo kuhusu mahakimu katika maeneo yao.
Jaji Mkuu alisema:”Juhudi za Tume ni kushughulikia pia maslahi ya watumishi wote wa mahakama…ukiacha nidhamu kwa majaji na mahakimu, lakini pia kuna madhambi mengi yanafanywa na makarani pamoja na wahudumu wa mahakama zetu”.
POLISI WATATU WATUPWA LUPANGO KYELA
POLISI watatu wilayani Kyela, wanashikiliwa kwa tuhuma za kuwa chanzo cha vurugu zilizotekea wilayani humo mara baada ya raia Lucas Mwaipopo,mkazi wa Mbugani kuuawa kwa kinachodaiwa ni kipigo kutoka kwa polisi.
Vurugu hizo zilipelekea wananchi zaidi ya 500 kuvamia na kupiga mawe kituo cha polisi, kuchoma moto mahakama ya Mwanzo ya Kyela mjini na pia kufanya uharibu wa mali katika ofisi ya Mkuu wa wilaya hiyo.
Polisi hao watatu wanaoshikiliwa ambao wote wana cheo cha Masajenti kutoka kitengo cha upelelezi wametajwa kuwa ni John mwenye namba D.4067, Joseph mwenye namba F.4849 na Mussa mwenye namba F.5753.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya, Advocate Nyombi alisema jana kuwa polisi hao watatu wanashikiliwa ili kuhojiwa kuweza kupata chanzo cha vurugu hizo zilizotokea wilayani humo na kupelekea polisi kutumia risasi za moto na mabomu ya machozi kuwadhibiti wananchi hao.
Alisema kuwa endapo polisi hao watatu wanaotuhumiwa kuwa chanzo cha kuzuka kwa vurugu hizo, wakibainika kuwa ni kweli watachukuliwa hatua kali za kisheria ili kuwa fundisho kwa wengine.
Nyombi alisema kuwa watu 96 walikamatwa kwa tuhuma za kuchochea vurugu hizo, ambapo walihojiwa na kumi na watano (15), kati yo wamefikishwa mahakamani jana kwa kosa la kufanya vurugu na kuvamia kituo cha polisi.
Aliwataja polisi wanane waliojeruhiwa kwa kupigwa mawe kuwa ni mkuu wa upelelezi wa wilaya ya Kyela Richard Mchomvu, E.9945 PC Julius, G. 54 PC Nyanda, E.7201 PC Timoth, E.1787 Koplo Robert, D.9713 Koplo Sarafini, E.3732 Koplo Travael, na E.8631 Sajent Mwita.
Aidha, magari mawili ya polisi yenye nmba za usajili PT.0798, PT. 0799 yote aina ya Lanlover yaliharibiwa kwa kupigwa mawe huku magari mengine ni T.646 AYL aina ya Landlover mali ya Daniel Mwambulukutu na T. 279 ARJ aina ya Toyota Hiace.
Kamanda Nyombi alisema kuwa katika watu waliojeruhiwa katika vurugu hizo yumo Ofisa Maeneleo ya Jamii wilaya ya Kyela, Nulusigwa Mwakigonja ambaye gari lake lenye namba za usajili T.573 AFA lilipoteza uelekeo na kugonga mti ambapo limeharibika vibaya.
Taarifa nyigine zilizopatikana kutoka hopitali ya Rufani Mbeya, zilidai kuwa majeruhi Jackob Antony (24), ambaye alipigwa risasi iliyoingia tumboni na kutokea kwenye kalio lake la upande wa kulia alikuwa anplekwa chumba cha upasuaji kwa ajili ya kuondolewa risasi.
Kufuatia vurugu hizo polisi juzi walilazimika kutangaza hali ya hatari na kuwataka wananchi kuwepo majumbani mwao ifikapo saa 1:30 usiku hali iliyopelekea mji huo wa mpakani na nchi jirani ya Malawi kupooza huku mitaa yote ikiwa haina watu.
Ni Mtizamo Tu ilishuhudia baadhi ya wateja waliokutwa katika baa ya Half London, iliyopo mjini humo wakipewa misukosuko kwa kukaidi kutii amri hiyo baada ya kukutwa wakiendelea kunywa vinywaji.
Hali hiyo ilipelekea wageni wengi waliochelewa kupta chakula cha jioni kulazimika kulala njaa kwani hakuna hotel ama baa yoyote iliyokuwa inafanya kazi kutokana na amri hiyo ya hatari.
Kituko kingine kilikuwa ni pale msichana aliyetajwa kwa jina la Jenny Chawe, ambaye alikuwa salon iitwayo Mariam iliyopo Kyela mjini akirembwa kujiandaa na sherehe ya kuagwa, naye kupotea kufuatia vurugu hizo hali iliyopelekea ndugu zake kuanza kuhaha kumtafuta mitaani.
Pia baadhi ya wanawake walikutwa barabarani wakiwa wanahaha kuwatafuta watoto wao baada ya kupotezana nao kufuatia vurugu hizo, lakini walifanikiwa kuwapata baadaye hali ilipotulia.
Vurugu hizo zilipelekea wananchi zaidi ya 500 kuvamia na kupiga mawe kituo cha polisi, kuchoma moto mahakama ya Mwanzo ya Kyela mjini na pia kufanya uharibu wa mali katika ofisi ya Mkuu wa wilaya hiyo.
Polisi hao watatu wanaoshikiliwa ambao wote wana cheo cha Masajenti kutoka kitengo cha upelelezi wametajwa kuwa ni John mwenye namba D.4067, Joseph mwenye namba F.4849 na Mussa mwenye namba F.5753.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya, Advocate Nyombi alisema jana kuwa polisi hao watatu wanashikiliwa ili kuhojiwa kuweza kupata chanzo cha vurugu hizo zilizotokea wilayani humo na kupelekea polisi kutumia risasi za moto na mabomu ya machozi kuwadhibiti wananchi hao.
Alisema kuwa endapo polisi hao watatu wanaotuhumiwa kuwa chanzo cha kuzuka kwa vurugu hizo, wakibainika kuwa ni kweli watachukuliwa hatua kali za kisheria ili kuwa fundisho kwa wengine.
Nyombi alisema kuwa watu 96 walikamatwa kwa tuhuma za kuchochea vurugu hizo, ambapo walihojiwa na kumi na watano (15), kati yo wamefikishwa mahakamani jana kwa kosa la kufanya vurugu na kuvamia kituo cha polisi.
Aliwataja polisi wanane waliojeruhiwa kwa kupigwa mawe kuwa ni mkuu wa upelelezi wa wilaya ya Kyela Richard Mchomvu, E.9945 PC Julius, G. 54 PC Nyanda, E.7201 PC Timoth, E.1787 Koplo Robert, D.9713 Koplo Sarafini, E.3732 Koplo Travael, na E.8631 Sajent Mwita.
Aidha, magari mawili ya polisi yenye nmba za usajili PT.0798, PT. 0799 yote aina ya Lanlover yaliharibiwa kwa kupigwa mawe huku magari mengine ni T.646 AYL aina ya Landlover mali ya Daniel Mwambulukutu na T. 279 ARJ aina ya Toyota Hiace.
Kamanda Nyombi alisema kuwa katika watu waliojeruhiwa katika vurugu hizo yumo Ofisa Maeneleo ya Jamii wilaya ya Kyela, Nulusigwa Mwakigonja ambaye gari lake lenye namba za usajili T.573 AFA lilipoteza uelekeo na kugonga mti ambapo limeharibika vibaya.
Taarifa nyigine zilizopatikana kutoka hopitali ya Rufani Mbeya, zilidai kuwa majeruhi Jackob Antony (24), ambaye alipigwa risasi iliyoingia tumboni na kutokea kwenye kalio lake la upande wa kulia alikuwa anplekwa chumba cha upasuaji kwa ajili ya kuondolewa risasi.
Kufuatia vurugu hizo polisi juzi walilazimika kutangaza hali ya hatari na kuwataka wananchi kuwepo majumbani mwao ifikapo saa 1:30 usiku hali iliyopelekea mji huo wa mpakani na nchi jirani ya Malawi kupooza huku mitaa yote ikiwa haina watu.
Ni Mtizamo Tu ilishuhudia baadhi ya wateja waliokutwa katika baa ya Half London, iliyopo mjini humo wakipewa misukosuko kwa kukaidi kutii amri hiyo baada ya kukutwa wakiendelea kunywa vinywaji.
Hali hiyo ilipelekea wageni wengi waliochelewa kupta chakula cha jioni kulazimika kulala njaa kwani hakuna hotel ama baa yoyote iliyokuwa inafanya kazi kutokana na amri hiyo ya hatari.
Kituko kingine kilikuwa ni pale msichana aliyetajwa kwa jina la Jenny Chawe, ambaye alikuwa salon iitwayo Mariam iliyopo Kyela mjini akirembwa kujiandaa na sherehe ya kuagwa, naye kupotea kufuatia vurugu hizo hali iliyopelekea ndugu zake kuanza kuhaha kumtafuta mitaani.
Pia baadhi ya wanawake walikutwa barabarani wakiwa wanahaha kuwatafuta watoto wao baada ya kupotezana nao kufuatia vurugu hizo, lakini walifanikiwa kuwapata baadaye hali ilipotulia.
Friday, July 10, 2009
MKUU WA ST.AGGREY SEKONDARI ABAKA MWANAFUNZI
MKUU wa shule ya sekondari ya St.Aggrey, jijini Mbeya Henry David Chelula, amefikishwa mahakama ya mkoa wa Mbeya, akikabiriwa na kosa la kutaka kumbaka mwanafunzi wa kike wa kidato cha nne shuleni hapo.
Chelula alikamatwa na maofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), mkoani hapa baada ya kuwekewa mtego.
Kesi hiyo ya jinai namba 135 ya mwaka huu ipo chini ya mwendesha mashtaka, Wakili wa serikali Keneth Sekwao na inasikilizwa na Hakimu mkazi Deborah Ndyekura.
Ilidai mahakamani hapo kuwa Julai 2,mwaka huu saa 11:00 jioni katika baa iliyo pia na nyumba ya kulala wageni iitwayo New M. Jokes iliyopo eneo la Maendeleo jijini Mbeya, chumba namba 11, mtuhumiwa Chelula alimdai rushwa ya ngono mwanafunzi huyo (jina linahifadhiwa), mwenye umri wa miaka 18.
Ilielezwa kuwa mtuhumiwa huyo alimdai mwanafunzi huyo wa kike anayesoma shule ya sekondari ya St.Aggrey ambayo yeye ni Mkuu wa shule, rushwa ya ngono kama sharti la kutoa huduma muhimu.
Chelula alikana shtaka hilo na yupo nje kwa dhamana hadi Julai 17,mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena mahakamani hapo.
Wakati huo huo Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Mbeya, Respick Ndowo, alisema kuwa taasisi hiyo inaendelea na uchunguzi kuhusiana na rushwa ya ngono kwa mujibu wa kifungu cha sheria namba 25 cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007.
Ndowo alisema mtuhumiwa Chelula amefikishwa mahakamani ya mkoa Mbeya na ofisi ya mwanasheria wa serikali akikabiriwa na kosa la hilo la kubaka ambalo ni kesi ya jinai iliyopewa namba 135 ya mwaka huu.
Chelula alikamatwa na maofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), mkoani hapa baada ya kuwekewa mtego.
Kesi hiyo ya jinai namba 135 ya mwaka huu ipo chini ya mwendesha mashtaka, Wakili wa serikali Keneth Sekwao na inasikilizwa na Hakimu mkazi Deborah Ndyekura.
Ilidai mahakamani hapo kuwa Julai 2,mwaka huu saa 11:00 jioni katika baa iliyo pia na nyumba ya kulala wageni iitwayo New M. Jokes iliyopo eneo la Maendeleo jijini Mbeya, chumba namba 11, mtuhumiwa Chelula alimdai rushwa ya ngono mwanafunzi huyo (jina linahifadhiwa), mwenye umri wa miaka 18.
Ilielezwa kuwa mtuhumiwa huyo alimdai mwanafunzi huyo wa kike anayesoma shule ya sekondari ya St.Aggrey ambayo yeye ni Mkuu wa shule, rushwa ya ngono kama sharti la kutoa huduma muhimu.
Chelula alikana shtaka hilo na yupo nje kwa dhamana hadi Julai 17,mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena mahakamani hapo.
Wakati huo huo Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Mbeya, Respick Ndowo, alisema kuwa taasisi hiyo inaendelea na uchunguzi kuhusiana na rushwa ya ngono kwa mujibu wa kifungu cha sheria namba 25 cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007.
Ndowo alisema mtuhumiwa Chelula amefikishwa mahakamani ya mkoa Mbeya na ofisi ya mwanasheria wa serikali akikabiriwa na kosa la hilo la kubaka ambalo ni kesi ya jinai iliyopewa namba 135 ya mwaka huu.
JWTZ WAFANYA USAFI KATIKA MASOKO JIJINI MBEYA
WAFANYABIASHARA wa masoko ya Matola na Uhindini, yaliyopo jijini Mbeya, wamelipongeza Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), kwa kufanya usafi mkubwa katika masoko hayo jana.
Walisema kuwa hatua hiyo imezidi kuonyesha jinsi JWTZ linavyothamini na kuisaidia jamii katika mambo mengine ya kijamii mbali ya ulinzi wa mipaka ya nchi yetu.
Akizungumza na Uhuru kwa niaba ya wenzake, Makamu Mwenyekiti wa soko la Matola, Abdallah Shaibu, alisema wanalishukuru jeshi kwa uamuzi wa kwenda kuwafanyia usafi katika soko lao.
“Hii ni changamoto kubwa sana kwetu wafanyabiashara sokoni hapa tuliyopewa na JWTZ ya kuzingatia usafi wa soko hili kwa afya zetu na wananchi wanaokuja kununua mahitaji mbalimbali sokoni hapa” alisema Shaibu.
Aliongeza kuwa hali hiyo itasababisha wafanyabiashara hao waone kuwa usafi wa maeneo yanayolizunguka soko hilo ni muhimu na siyo kusubiria hadi wageni kutoka nje (JWTZ), ndio waende kuwafanyia kazi hiyo.
Shaibu aliwashauri wafanyabiashara wa masoko hayo ya Uhindini na Matola kuiga mfano huo wa kuzingatia usafi na kuyatunza maeneo yao kama walivyoonyeshwa na JWTZ na siyo kubweteka na kujua kazi ya usafi katika masoko hayo haiwahusu wao bali wafanyakazi wa halmashauri ya jiji la Mbeya.
Shaibu alisema:”Tunalishukuru sana JWTZ kwa uamuzi huu wa busara waliouchukua wa kuzijali afya zetu…walifika hapa saa 1:30 asubuhi na baada ya kufanya usafi soko lote waliondoka saa 3:30 asubuhi”.
Walisema kuwa hatua hiyo imezidi kuonyesha jinsi JWTZ linavyothamini na kuisaidia jamii katika mambo mengine ya kijamii mbali ya ulinzi wa mipaka ya nchi yetu.
Akizungumza na Uhuru kwa niaba ya wenzake, Makamu Mwenyekiti wa soko la Matola, Abdallah Shaibu, alisema wanalishukuru jeshi kwa uamuzi wa kwenda kuwafanyia usafi katika soko lao.
“Hii ni changamoto kubwa sana kwetu wafanyabiashara sokoni hapa tuliyopewa na JWTZ ya kuzingatia usafi wa soko hili kwa afya zetu na wananchi wanaokuja kununua mahitaji mbalimbali sokoni hapa” alisema Shaibu.
Aliongeza kuwa hali hiyo itasababisha wafanyabiashara hao waone kuwa usafi wa maeneo yanayolizunguka soko hilo ni muhimu na siyo kusubiria hadi wageni kutoka nje (JWTZ), ndio waende kuwafanyia kazi hiyo.
Shaibu aliwashauri wafanyabiashara wa masoko hayo ya Uhindini na Matola kuiga mfano huo wa kuzingatia usafi na kuyatunza maeneo yao kama walivyoonyeshwa na JWTZ na siyo kubweteka na kujua kazi ya usafi katika masoko hayo haiwahusu wao bali wafanyakazi wa halmashauri ya jiji la Mbeya.
Shaibu alisema:”Tunalishukuru sana JWTZ kwa uamuzi huu wa busara waliouchukua wa kuzijali afya zetu…walifika hapa saa 1:30 asubuhi na baada ya kufanya usafi soko lote waliondoka saa 3:30 asubuhi”.
DAWA ZA KUONGEZA MATITI,HIPS NA MAKALIO ZAKAMATWA IRINGA
MKAGUZI wa Dawa wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), kanda ya nyanda za juu kusini, Paul Sonda, amesema kuwa wamefanya ukaguzi wa ghafla na kulibaini duka moja mkoani Iringa, linalouza dawa za kuongeza matiti, makalio na Hips kwa wanawake.
Imeelezwa kuwa TFDA iliamua kufanya ukaguzi huo wa kawaida baada ya kupewa taarifa na raia wema kuwa duka hilo linauza dawa hizo ambazo zimetengezwa nchini China.
Akizungumza jana Sonda alisema kuwa baada ya kufanya ukaguzi huo walibaini kwamba dawa zote zinazouzwa dukani humo pamoja na jengo lenyewe vyote havijasajiliwa na TFDA.
“Tuliwahoji wauzaji ili kutaka kujua sehemu walikozinunua dawa hizo ambazo zimeandikwa kwa lugha ya Kichina lakini hawakuweza kuweleza kwani hata nyaraka walizonunulia hawakuwa nazo” alisema Sonda.
Alisema TFDA huwa wanasajili dawa zenye maandishi ya Kiingereza, Kiswahili ama zilizoandikwa kwa lugha zote hizo mbili lakini siyo nje ya hapo.
Mkaguzi huyo wa dawa kanda hii aliongeza kuwa dawa inaweza iikawa imeandikwa kwa lugha yoyote ile duniani lakini sharti ni kuwa lazima kuwepo na tafsiri ya maandishi hayo kwa Kiingereza ama Kiswahili.
Sonda alisema kuwa walitoa elimu kwa wauzaji wa duka hilo kuhusu umuhimu wa kusajili jengo hilo pamoja na bidhaa wanazouza ambapo walitoa ushirikiano mzuri.
Alisema:”Baadaye tulizichukua dawa hizo za kuongeza matiti, makalio na Hips na kuondoka nazo kwa kujibu wa taratibu zilizopo na tulikwenda kumkabidhi Mganga Mkuu wa hospitali ya mkoa wa Iringa kwa ajili ya kuziteketeza”.
Aliongeza kuwa hawakuweza kujua thamani halisi ya dawa hizo lakini zilikuwa nyingi na kuwa kwa ukaguzi walioufanya katika mikoa mingine ya Mbeya, Rukwa na Ruvuma hawajaweza kuzibaini dawa za aina hiyo.
Imeelezwa kuwa TFDA iliamua kufanya ukaguzi huo wa kawaida baada ya kupewa taarifa na raia wema kuwa duka hilo linauza dawa hizo ambazo zimetengezwa nchini China.
Akizungumza jana Sonda alisema kuwa baada ya kufanya ukaguzi huo walibaini kwamba dawa zote zinazouzwa dukani humo pamoja na jengo lenyewe vyote havijasajiliwa na TFDA.
“Tuliwahoji wauzaji ili kutaka kujua sehemu walikozinunua dawa hizo ambazo zimeandikwa kwa lugha ya Kichina lakini hawakuweza kuweleza kwani hata nyaraka walizonunulia hawakuwa nazo” alisema Sonda.
Alisema TFDA huwa wanasajili dawa zenye maandishi ya Kiingereza, Kiswahili ama zilizoandikwa kwa lugha zote hizo mbili lakini siyo nje ya hapo.
Mkaguzi huyo wa dawa kanda hii aliongeza kuwa dawa inaweza iikawa imeandikwa kwa lugha yoyote ile duniani lakini sharti ni kuwa lazima kuwepo na tafsiri ya maandishi hayo kwa Kiingereza ama Kiswahili.
Sonda alisema kuwa walitoa elimu kwa wauzaji wa duka hilo kuhusu umuhimu wa kusajili jengo hilo pamoja na bidhaa wanazouza ambapo walitoa ushirikiano mzuri.
Alisema:”Baadaye tulizichukua dawa hizo za kuongeza matiti, makalio na Hips na kuondoka nazo kwa kujibu wa taratibu zilizopo na tulikwenda kumkabidhi Mganga Mkuu wa hospitali ya mkoa wa Iringa kwa ajili ya kuziteketeza”.
Aliongeza kuwa hawakuweza kujua thamani halisi ya dawa hizo lakini zilikuwa nyingi na kuwa kwa ukaguzi walioufanya katika mikoa mingine ya Mbeya, Rukwa na Ruvuma hawajaweza kuzibaini dawa za aina hiyo.
Tuesday, July 7, 2009
MWANAFUNZI WA SEKONDARI YA IYUNGA MBEYA AGONGWA NA KUFARIKI
MWANAFUNZI wa kidato cha nne,shule ya sekondari Iyunga,jijini Mbeya amekufa papo hapo baada ya kugongwa na gari eneo la Nzovwe, akiwa anatembea pembezoni mwa barabara.
Ajali hiyo iliyohusisha gari ambayo ni daladala yenye namba za usajili T.129 AMD aina ya Toyota Hiace,ikiendeshwa na dereva Japhet Mwile, ilitokea jana saa 2:00 asubuhi katika barabara ya Mbeya kwenda Tunduma.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya,Advocate Nyombi, akizungumza jana ofisini kwake, alimtaja mwanafunzi huyo kuwa ni Hery Mlengule.
Nyombi alisema kuwa daladala hiyo ikiwa na abiria ndani yake ilikuwa inaelekea mji mdogo wa Mbalizi na mara baada ya ajalib hiyo, dereva pamoja na gari walipelekwa kituo kikuu cha polisi.
Uchunguzi zaidi juu ya ajali hiyo unaendelea kufanywa ili kujua chanzo cha ajali hiyo.
Katika tukio lingine lililotokea eneo la Forest Mpya, jijini hapa,mtoto mchanga wa kike mwenye umri kati ya wiki moja ama mbili aliokotwa akiwa ametupwa katika mfereji wa maji machafu na mtu asiyefahamika.
Kwa mujibu wa Kamanda Nyombi, tukio hilo lilitokea jana saa 11:00 jioni katika mtaa wa Kilimani uliopo eneo hilo.
Alisema kuwa mtoto huyo aliokotwa akiwa hai na Esther Mwakalebele, ambaye alikuwa anamwagilia bustani yake ya mboga mboga iliyopo jirani na mtaro huo wa maji machafu.
Nyombi alisema kichanga huyo yupo hai na anahifadhiwa hospitali ya Rufani Mbeya, kitengo cha Wazazi Meta na msako wa kumsaka mwanamke aliyefanya kitendo hicho cha kikatili unaendelea kufanywa.
Ajali hiyo iliyohusisha gari ambayo ni daladala yenye namba za usajili T.129 AMD aina ya Toyota Hiace,ikiendeshwa na dereva Japhet Mwile, ilitokea jana saa 2:00 asubuhi katika barabara ya Mbeya kwenda Tunduma.
Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya,Advocate Nyombi, akizungumza jana ofisini kwake, alimtaja mwanafunzi huyo kuwa ni Hery Mlengule.
Nyombi alisema kuwa daladala hiyo ikiwa na abiria ndani yake ilikuwa inaelekea mji mdogo wa Mbalizi na mara baada ya ajalib hiyo, dereva pamoja na gari walipelekwa kituo kikuu cha polisi.
Uchunguzi zaidi juu ya ajali hiyo unaendelea kufanywa ili kujua chanzo cha ajali hiyo.
Katika tukio lingine lililotokea eneo la Forest Mpya, jijini hapa,mtoto mchanga wa kike mwenye umri kati ya wiki moja ama mbili aliokotwa akiwa ametupwa katika mfereji wa maji machafu na mtu asiyefahamika.
Kwa mujibu wa Kamanda Nyombi, tukio hilo lilitokea jana saa 11:00 jioni katika mtaa wa Kilimani uliopo eneo hilo.
Alisema kuwa mtoto huyo aliokotwa akiwa hai na Esther Mwakalebele, ambaye alikuwa anamwagilia bustani yake ya mboga mboga iliyopo jirani na mtaro huo wa maji machafu.
Nyombi alisema kichanga huyo yupo hai na anahifadhiwa hospitali ya Rufani Mbeya, kitengo cha Wazazi Meta na msako wa kumsaka mwanamke aliyefanya kitendo hicho cha kikatili unaendelea kufanywa.
SAMAKI WAPUNGUA ZIWA RUKWA-MBOZI
UVUVI haramu unaondelea kufanyika katika Ziwa Rukwa,upande wa wilaya Mbozi, umepelekea kupunguza kiwango cha uvuvi ziwani humo,imeelezwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa wilaya ya Mbozi,Levisson Chilewa, alisema hilo limebainika baada ya kuona samaki wengi wanaovuliwa kutoka ziwani humo ni wale wadogo (wachanga).
Chilewa alisema kufuatia hali hiyo walitoa ombi kwa Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ili wafunge shughuli za uvuvi kwa miezi minne yaani kuanzia mwezi Januari hadi Aprili mwaka huu ili samaki waweze kuzaliana.
“Tuliona kuwa kipindi hiki ndio ambacho samaki huwa wanazaliana na kukua, hivyo tungeweza kutatua tatizo hili la upungufu wa samaki katika Ziwa hili upande wa Mbozi” alisema Chilewa.
Aliongeza kuwa njia nyingine wanayoitumia katika kukabiriana na hatari ya samaki kutoweka kabisa Ziwani humo, ni kujenga mabwawa 104 ya kufugia samaki ambapo katika viwanja vya ofisi ya halmashauri hiyo wanalo bwawa moja.
Mkurugenzi alisema kuwa bwawa hilo la halmashauri huwa linatumika kwa ajili kuzalisha samaki aina ya Perege ambao huwauza kwa wananchi, taasisi za kiserikali na zile zisizokuwa za kiserikali.
“Nia yetu ni kuhakikisha kuwa wananchi wananchi wanaendelea kutumia Samaki ili kuongeza lishe pia kujioongezea kipato zaidi” alisema Chilewa.
Aliongeza kuwa halmashauri imetengeneza boti ya kufanyia doria yenye thamani shilingi milioni 4.8 huku injini yake ikiwa na thamani ya shilingi milioni 2.8 kwa ajili ya kukabiriana na wavuvi haramu katika Ziwa hilo.
Chilewa alisema kwa kutumia boti hilo wameweza kukamata makokoro 37 na nyavu 110 zenye macho madogo ambazo hutumiwa na wavuvi haramu ambao wamepelekea kupungua kwa samaki Ziwani humo.
Ziwa Rukwa limepitia katika wilaya za Chunya na Mbozi kwa upande wa mkoa wa Mbeya na wilaya za Mpanda pamoja na Sumbawanga Vijijini,kwa mkoa wa Rukwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa wilaya ya Mbozi,Levisson Chilewa, alisema hilo limebainika baada ya kuona samaki wengi wanaovuliwa kutoka ziwani humo ni wale wadogo (wachanga).
Chilewa alisema kufuatia hali hiyo walitoa ombi kwa Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ili wafunge shughuli za uvuvi kwa miezi minne yaani kuanzia mwezi Januari hadi Aprili mwaka huu ili samaki waweze kuzaliana.
“Tuliona kuwa kipindi hiki ndio ambacho samaki huwa wanazaliana na kukua, hivyo tungeweza kutatua tatizo hili la upungufu wa samaki katika Ziwa hili upande wa Mbozi” alisema Chilewa.
Aliongeza kuwa njia nyingine wanayoitumia katika kukabiriana na hatari ya samaki kutoweka kabisa Ziwani humo, ni kujenga mabwawa 104 ya kufugia samaki ambapo katika viwanja vya ofisi ya halmashauri hiyo wanalo bwawa moja.
Mkurugenzi alisema kuwa bwawa hilo la halmashauri huwa linatumika kwa ajili kuzalisha samaki aina ya Perege ambao huwauza kwa wananchi, taasisi za kiserikali na zile zisizokuwa za kiserikali.
“Nia yetu ni kuhakikisha kuwa wananchi wananchi wanaendelea kutumia Samaki ili kuongeza lishe pia kujioongezea kipato zaidi” alisema Chilewa.
Aliongeza kuwa halmashauri imetengeneza boti ya kufanyia doria yenye thamani shilingi milioni 4.8 huku injini yake ikiwa na thamani ya shilingi milioni 2.8 kwa ajili ya kukabiriana na wavuvi haramu katika Ziwa hilo.
Chilewa alisema kwa kutumia boti hilo wameweza kukamata makokoro 37 na nyavu 110 zenye macho madogo ambazo hutumiwa na wavuvi haramu ambao wamepelekea kupungua kwa samaki Ziwani humo.
Ziwa Rukwa limepitia katika wilaya za Chunya na Mbozi kwa upande wa mkoa wa Mbeya na wilaya za Mpanda pamoja na Sumbawanga Vijijini,kwa mkoa wa Rukwa.
Friday, June 19, 2009
MAMBO YA JEANS ZA KIJAPAN HAYA HAPA
Japanese Jeans. Bringing Sexy Back(A)
Japan has come out with yet another sexy, wild, and edgy fashion trend with these Bikini Jeans, that act as both underwear and jeans.
Sandra Tanimura, a Sanna designer, created these jeans after customers mentioned they had a hard time keeping their low cut jeans up.
â€Å“We specialize in making low-rise trousers and our customers wanted them to get even lower.
It was very difficult meeting these demands without the trousers falling down. I came up with the idea of using the bikini strings to let the trousers hang really low without falling,� she added.
Below are some shots of the jeans on a popular Japanese television show:
You can purchase these Bikini Jeans for about $88.
Like all trends, not everyone can pull it off quite the same.
Japan has come out with yet another sexy, wild, and edgy fashion trend with these Bikini Jeans, that act as both underwear and jeans.
Sandra Tanimura, a Sanna designer, created these jeans after customers mentioned they had a hard time keeping their low cut jeans up.
â€Å“We specialize in making low-rise trousers and our customers wanted them to get even lower.
It was very difficult meeting these demands without the trousers falling down. I came up with the idea of using the bikini strings to let the trousers hang really low without falling,� she added.
Below are some shots of the jeans on a popular Japanese television show:
You can purchase these Bikini Jeans for about $88.
Like all trends, not everyone can pull it off quite the same.
WAZIRI WA USALAMA WA NDANI SOMALIA AUAWA
WAZIRI wa usalama wa ndani wa Somalia Omar Hashi Aden ameuwawa kwenye shambulio la kujitoa muhanga la bomu lililotegwa kwenye gari kaskazini mwa mji mkuu wa Mogadishu.
Watu wengine zaidi ya 20 wameuwawa kwenye mlipuko huo katika Hoteli ya Beledweyne, kaskazini mwa mji mkuu wa Mogadishu.
Miongoni mwa waliouwawa ni maafisa kadhaa wa Kidiplomasia wa Somalia.
Rais wa Somalia Sheikh Sharif Sheikh Ahmed amelaumu kundi la wapiganaji wa Kiislamu la Al-Shabaab , ambalo pia baadaye lilikiri kufanya shambulio hilo.
Kundi hilo linaaminika kuwa na uhusiano na mtandao wa kigaidi wa Al -Qaeda.
Siku ya jumaatano watu 10 walikufa wakati kombora liliporushwa kwenye msikiti mjini Mogadishu.
Katika shambulizi la Alhamisi , walioshuhudia walisema mlipuaji wa kujitoa muhanga alilipua gari lililojaa mabomu kwenye hoteli ya Medina , mjini Beledweyne, yapata Kilomita 400 kaskazini mwa Mogadishu.
Abdulkarim Ibrahim Lakanyo, balozi wa zamani wa Somalia nchini Ethiopia pia ameripotiwa kuwa miongoni mwa waliouwawa.
Mwandishi wa BBC Will Ross anasema bwana Aden alihamia mjini Beledweyne hivi majuzi, mji ulioko karibu na mpaka wa Ethiopia, katika jitihada za kukomesha wanamgambo wa Kiislamu wasiendelee kuthibiti maeneo mengi zaidi.
Rais Ahmed ameambia mkutano wa waandishi wa habari mjini Mogadishu kwamba Somalia imevamiwa na magaidi wasiotaka kuona benderea ya nchi hiyo, wala amani .
Amesema kundi hilo la Al- shabaab linajificha kwenye Uislamu kuendesha ukatili wao.
Somalia haijawa na serikali dhabiti tangu mwaka wa 1991 , na zaidi ya watu milioni nne , ambao ni asilimia 75 ya raia wa nchi hiyo wanahitaji msaada wa chakula.
Kundi la Al- Shabaab ni mshirika katika muungano wa wanamgambo wa kiislamu wenye msimamo mkali ambao wamekuwa wakijaribu kuiangusha serikali ya mpito ya Somalia inayoungwa mkono na umoja wa mataifa.
Rais Ahmed , ambaye mwenyewe ni muislamu mwenye msimamo wa wastani alichukua khatamu nchini Somalia mwezi Januari , lakini hata baada ya kuanzisha utawala wa kuzingatia sheria za kiislamu , hatua hiyo bado haijawaridhisha wapiganaji hao.
Jumaatano , kamanda mkuu wa Polisi mjini Mogadishu aliuwawa kwenye mashambulizi dhidi ya ngome za wanamgambo.
Mwakilishi wa shirika la umoja wa mataifa linaloshughulikia wakimbizi UNHCR nchini Somalia amesema umwagikaji damu wa hivi karibuni nchini Somalia ndio mbaya zaidi kuikumba nchi hiyo kwa muda wa karibu miaka 20.
Watu wengine zaidi ya 20 wameuwawa kwenye mlipuko huo katika Hoteli ya Beledweyne, kaskazini mwa mji mkuu wa Mogadishu.
Miongoni mwa waliouwawa ni maafisa kadhaa wa Kidiplomasia wa Somalia.
Rais wa Somalia Sheikh Sharif Sheikh Ahmed amelaumu kundi la wapiganaji wa Kiislamu la Al-Shabaab , ambalo pia baadaye lilikiri kufanya shambulio hilo.
Kundi hilo linaaminika kuwa na uhusiano na mtandao wa kigaidi wa Al -Qaeda.
Siku ya jumaatano watu 10 walikufa wakati kombora liliporushwa kwenye msikiti mjini Mogadishu.
Katika shambulizi la Alhamisi , walioshuhudia walisema mlipuaji wa kujitoa muhanga alilipua gari lililojaa mabomu kwenye hoteli ya Medina , mjini Beledweyne, yapata Kilomita 400 kaskazini mwa Mogadishu.
Abdulkarim Ibrahim Lakanyo, balozi wa zamani wa Somalia nchini Ethiopia pia ameripotiwa kuwa miongoni mwa waliouwawa.
Mwandishi wa BBC Will Ross anasema bwana Aden alihamia mjini Beledweyne hivi majuzi, mji ulioko karibu na mpaka wa Ethiopia, katika jitihada za kukomesha wanamgambo wa Kiislamu wasiendelee kuthibiti maeneo mengi zaidi.
Rais Ahmed ameambia mkutano wa waandishi wa habari mjini Mogadishu kwamba Somalia imevamiwa na magaidi wasiotaka kuona benderea ya nchi hiyo, wala amani .
Amesema kundi hilo la Al- shabaab linajificha kwenye Uislamu kuendesha ukatili wao.
Somalia haijawa na serikali dhabiti tangu mwaka wa 1991 , na zaidi ya watu milioni nne , ambao ni asilimia 75 ya raia wa nchi hiyo wanahitaji msaada wa chakula.
Kundi la Al- Shabaab ni mshirika katika muungano wa wanamgambo wa kiislamu wenye msimamo mkali ambao wamekuwa wakijaribu kuiangusha serikali ya mpito ya Somalia inayoungwa mkono na umoja wa mataifa.
Rais Ahmed , ambaye mwenyewe ni muislamu mwenye msimamo wa wastani alichukua khatamu nchini Somalia mwezi Januari , lakini hata baada ya kuanzisha utawala wa kuzingatia sheria za kiislamu , hatua hiyo bado haijawaridhisha wapiganaji hao.
Jumaatano , kamanda mkuu wa Polisi mjini Mogadishu aliuwawa kwenye mashambulizi dhidi ya ngome za wanamgambo.
Mwakilishi wa shirika la umoja wa mataifa linaloshughulikia wakimbizi UNHCR nchini Somalia amesema umwagikaji damu wa hivi karibuni nchini Somalia ndio mbaya zaidi kuikumba nchi hiyo kwa muda wa karibu miaka 20.
MTIKISIKO WA YUCHUMI DUNIANI
KATIKA hatua muhimu ya kudhibiti huduma za benki nchini Marekani, Rais Barack Obama ametangaza sera mpya zenye lengo la kuhakikisha msukosuko wa kifedha ulioikumba nchi hiyo hautokei tena.
Kufuatia mabadiliko hayo, benki zilizostawi zitahitajika kukuza hazina ambayo itatumiwa kukabiliana na hasara zozote.
Pia kutabuniwa shirika maalum la kutetea haki za wateja ikiwa ni pamoja na kusimamia mfumo wa rehani na mikopo.
Rais Obama aliyataja mabadiliko hayo kuwa ndiyo muhimu zaidi kuwahi kubuniwa katika mfumo wa fedha nchini Marekani tangu miaka ya 1930.
Benki kuu itasimamia utekelezaji wa mabadiliko na imepewa mamlaka ya kuchunguza mienendo ya taasisi za kifedha na benki.
Rais Obama alisema makampuni mengi pamoja na wateja wamepata hasara kubwa kutokana na kutokuwepo na sera mufti za kusimamia benki.
"Tunafanya kila tuwezalo kujenga msingi thabiti wa kukuza uchumi kwa njia endelevu. Hili halitakuwa jambo rahisi" alisema Rais Obama.
Kufuatia mabadiliko hayo, benki zilizostawi zitahitajika kukuza hazina ambayo itatumiwa kukabiliana na hasara zozote.
Pia kutabuniwa shirika maalum la kutetea haki za wateja ikiwa ni pamoja na kusimamia mfumo wa rehani na mikopo.
Rais Obama aliyataja mabadiliko hayo kuwa ndiyo muhimu zaidi kuwahi kubuniwa katika mfumo wa fedha nchini Marekani tangu miaka ya 1930.
Benki kuu itasimamia utekelezaji wa mabadiliko na imepewa mamlaka ya kuchunguza mienendo ya taasisi za kifedha na benki.
Rais Obama alisema makampuni mengi pamoja na wateja wamepata hasara kubwa kutokana na kutokuwepo na sera mufti za kusimamia benki.
"Tunafanya kila tuwezalo kujenga msingi thabiti wa kukuza uchumi kwa njia endelevu. Hili halitakuwa jambo rahisi" alisema Rais Obama.
RUBANI AFA NDEGE IKIWA ANGANI
ABIRIA 247 wameponea chupuchupu katika kisa ambacho wengi watadhani ni muujiza!!!Abiria 247 waliokuwa wakisafiri na ndege ya kampuni ya Continental kutoka Ubelgiji hadi Marekani waliponea chupuchupu wakati nahodha wa ndege yao alipofariki dunia.
Msemaji wa Halmashauri inayosimamia usafiri wa ndege Marekani, Arlene Salac alisema kulikuwa na marubani wengine wawili ambao waliidhibiti ndege hiyo aina ya Boeing 777 hadi uwanja wa ndege wa Newark Liberty ambako ilitua kwa dharura.
Mtaalamu mmoja wa usafiri wa ndege, Jim Ferguson alisema si jambo la kawaida rubani kufariki dunia akiwa angani.
Kwa kawaida ndege hiyo huendeshwa na marubani wawili. Lakini kwa bahati nzuri wakati huu, kulikuwa na mwingine wa ziada.
Bwana Ferguson alisema ingekuwa vigumu kwa rubani mmoja kuidhibiti ndege hiyo kutua.
Abiria hawakuambiwa lolote kuhusu mkasa huo.
Miongoni mwao alikuwa daktari mmoja wa maswala ya moyo, Dr. Julien Struyven ambaye aliitikia tangazo daktari yeyote kwenye ndege hiyo kujitokeza.
Abiria hawakujua kwamba mwito ulitolewa kwa ajili ya kumuokoa rubani wa ndege hiyo.
Dr Struyven alipomfikia rubani huyo alikuta kama tayari ameaga dunia.
“Hakukuwa na uwezekano wowote wa kumwokoa,” alisema Dr Struyven.
Alisema huenda rubani huyo mwenye umri wa miaka 60 na ambaye amehudumia kampuni hiyo kwa zaidi ya miaka 20 alifariki dunia kutokana na matatizo ya moyo
Msemaji wa Halmashauri inayosimamia usafiri wa ndege Marekani, Arlene Salac alisema kulikuwa na marubani wengine wawili ambao waliidhibiti ndege hiyo aina ya Boeing 777 hadi uwanja wa ndege wa Newark Liberty ambako ilitua kwa dharura.
Mtaalamu mmoja wa usafiri wa ndege, Jim Ferguson alisema si jambo la kawaida rubani kufariki dunia akiwa angani.
Kwa kawaida ndege hiyo huendeshwa na marubani wawili. Lakini kwa bahati nzuri wakati huu, kulikuwa na mwingine wa ziada.
Bwana Ferguson alisema ingekuwa vigumu kwa rubani mmoja kuidhibiti ndege hiyo kutua.
Abiria hawakuambiwa lolote kuhusu mkasa huo.
Miongoni mwao alikuwa daktari mmoja wa maswala ya moyo, Dr. Julien Struyven ambaye aliitikia tangazo daktari yeyote kwenye ndege hiyo kujitokeza.
Abiria hawakujua kwamba mwito ulitolewa kwa ajili ya kumuokoa rubani wa ndege hiyo.
Dr Struyven alipomfikia rubani huyo alikuta kama tayari ameaga dunia.
“Hakukuwa na uwezekano wowote wa kumwokoa,” alisema Dr Struyven.
Alisema huenda rubani huyo mwenye umri wa miaka 60 na ambaye amehudumia kampuni hiyo kwa zaidi ya miaka 20 alifariki dunia kutokana na matatizo ya moyo
RUBANI AFA NDEGE IKIWA ANGANI
Rubani afa ndege ikiwa angani Abiria 247 waponea chupuchupu Katika kisa ambacho wengi watadhani ni muujiza, abiria 247 waliokuwa wakisafiri na ndege ya kampuni ya Continental kutoka Ubelgiji hadi Marekani waliponea chupuchupu wakati nahodha wa ndege yao alipofariki dunia.
Msemaji wa Halmashauri inayosimamia usafiri wa ndege Marekani, Arlene Salac alisema kulikuwa na marubani wengine wawili ambao waliidhibiti ndege hiyo aina ya Boeing 777 hadi uwanja wa ndege wa Newark Liberty ambako ilitua kwa dharura.
Mtaalamu mmoja wa usafiri wa ndege, Jim Ferguson alisema si jambo la kawaida rubani kufariki dunia akiwa angani.
Kwa kawaida ndege hiyo huendeshwa na marubani wawili. Lakini kwa bahati nzuri wakati huu, kulikuwa na mwingine wa ziada.
Bwana Ferguson alisema ingekuwa vigumu kwa rubani mmoja kuidhibiti ndege hiyo kutua.
Abiria hawakuambiwa lolote kuhusu mkasa huo.
Miongoni mwao alikuwa daktari mmoja wa maswala ya moyo, Dr. Julien Struyven ambaye aliitikia tangazo daktari yeyote kwenye ndege hiyo kujitokeza.
Abiria hawakujua kwamba mwito ulitolewa kwa ajili ya kumuokoa rubani wa ndege hiyo.
Dr Struyven alipomfikia rubani huyo alikuta kama tayari ameaga dunia.
“Hakukuwa na uwezekano wowote wa kumwokoa,” alisema Dr Struyven.
Alisema huenda rubani huyo mwenye umri wa miaka 60 na ambaye amehudumia kampuni hiyo kwa zaidi ya miaka 20 alifariki dunia kutokana na matatizo ya moyo
Msemaji wa Halmashauri inayosimamia usafiri wa ndege Marekani, Arlene Salac alisema kulikuwa na marubani wengine wawili ambao waliidhibiti ndege hiyo aina ya Boeing 777 hadi uwanja wa ndege wa Newark Liberty ambako ilitua kwa dharura.
Mtaalamu mmoja wa usafiri wa ndege, Jim Ferguson alisema si jambo la kawaida rubani kufariki dunia akiwa angani.
Kwa kawaida ndege hiyo huendeshwa na marubani wawili. Lakini kwa bahati nzuri wakati huu, kulikuwa na mwingine wa ziada.
Bwana Ferguson alisema ingekuwa vigumu kwa rubani mmoja kuidhibiti ndege hiyo kutua.
Abiria hawakuambiwa lolote kuhusu mkasa huo.
Miongoni mwao alikuwa daktari mmoja wa maswala ya moyo, Dr. Julien Struyven ambaye aliitikia tangazo daktari yeyote kwenye ndege hiyo kujitokeza.
Abiria hawakujua kwamba mwito ulitolewa kwa ajili ya kumuokoa rubani wa ndege hiyo.
Dr Struyven alipomfikia rubani huyo alikuta kama tayari ameaga dunia.
“Hakukuwa na uwezekano wowote wa kumwokoa,” alisema Dr Struyven.
Alisema huenda rubani huyo mwenye umri wa miaka 60 na ambaye amehudumia kampuni hiyo kwa zaidi ya miaka 20 alifariki dunia kutokana na matatizo ya moyo
Tuesday, June 16, 2009
WAETHIOPIA 98 WATIWA MBARONI MKOANI MBEYA.
MIST YAPANIA KUONGEZA UDAHILI KWA WANAWAKE
TAASISI ya Sayansi na Teknolojia Mbeya (MIST), imeanza kutekeleza agizo la Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Profesa Peter Msolla, la kuhakikisha kuwa wanaongeza udahili wa wanafunzi wa kike kujiunga chuoni hapo.
Hadi sasa walimu wa taasisi hiyo wamezitembelea shule za sekondari 21 mkoani hapa, ili kutoa elimu kwa wanafunzi wa kike kupenda kusoma masomo ya sayansi,Hisabati na ufundi.
Profesa Msolla alitoa agizo hilo hivi karibuni wakati akizindua shahada katika fani za biashara na uhandisi katika fani za ujenzi, umeme, Mitambo na Usanifu wa Majengo, katika taasisi hiyo.
Mkuu wa MIST Profesa Joseph Msambichaka, aliyasema hayo jana, wakati akielezea kuhusu hatua ya taasisi hiyo kuandaa semina ya siku tatu kwa kushirikiana na asasi ya Peace Corps Tanzania ya nchini Marekani, kwa ajili ya kumuwezesha mtoto wa kike kuyapenda masomo hayo.
Semina hiyo inashirikisha wanafunzi wa kike 80, wa shule za msingi na sekondari kutoka wilaya wilaya zote za mkoa wa Mbeya, na wanafundishwa na wataalam saba wa kujitolea, kutoka Peace Corps Tanzania.
Profesa Msambichaka alisema kuwa tatizo kubwa lililopo ni kuwa wanafunzi wa kike wamekuwa na tabia ya kuyakimbia masomo ya sayansi na kuwaachia watoto wa kikume madai kuwa masomo hayo ni magumu kitu ambacho siyo kweli.
Alisema kuwa hivi sasa MIST inao utaratibu wa kutoa mafunzo maalumu kwa ajili ya somo la Hisabati kwa watoto wa kike wanaokuwa wamemaliza elimu ya sekondari.
"Wale wanaokuwa wamefaulu vizuri huwa serikali inaingia gharama ya kuwasomesha kwa muda wote wanaokuwepo hapa taasisi lengo likiwa ni kuwahamasisha kuyapenda masomo ya sayansi" alisema Msambichaka.
Profesa Msambichaka alisema kuwa mwaka 2008, wanafunzi wa kike 13 walifanya masomo hayo maalumu, ambapo kwa mwaka jana waliojitokeza walikuwa ni zaidi ya 50.
Nao washiriki wa semina hiyo, wakizungumza kwa nyakati tofauti na Uhuru, walisema kuwa wanashukuru kwa kupata semina hiyo kwani ni ukweli kuwa watoto wa kike wapo nyuma.
Walisema kuwa wazazi wengi huwa wanawaona watoto wa kiume kuwa ndio wanaopaswa kusoma na wao kupenda kufanyishwa kazi za nyumbani hivyo huwa na muda kidogo wa kujisomea tofauti na wenzao wanaume.
"Tunataka kuiambia jamii kuwa tulikuwa nyuma kutokana na mfumo dume uliojenga kwa muda mrefu...watoto wa kike tulikuwa tunaonekana kwamba hatuwezi kusoma kwani mzazi aliyekuwa anamsomsemesha mtoto wa kike alikuwa akionekana anapoteza muda" walisema.
Hadi sasa walimu wa taasisi hiyo wamezitembelea shule za sekondari 21 mkoani hapa, ili kutoa elimu kwa wanafunzi wa kike kupenda kusoma masomo ya sayansi,Hisabati na ufundi.
Profesa Msolla alitoa agizo hilo hivi karibuni wakati akizindua shahada katika fani za biashara na uhandisi katika fani za ujenzi, umeme, Mitambo na Usanifu wa Majengo, katika taasisi hiyo.
Mkuu wa MIST Profesa Joseph Msambichaka, aliyasema hayo jana, wakati akielezea kuhusu hatua ya taasisi hiyo kuandaa semina ya siku tatu kwa kushirikiana na asasi ya Peace Corps Tanzania ya nchini Marekani, kwa ajili ya kumuwezesha mtoto wa kike kuyapenda masomo hayo.
Semina hiyo inashirikisha wanafunzi wa kike 80, wa shule za msingi na sekondari kutoka wilaya wilaya zote za mkoa wa Mbeya, na wanafundishwa na wataalam saba wa kujitolea, kutoka Peace Corps Tanzania.
Profesa Msambichaka alisema kuwa tatizo kubwa lililopo ni kuwa wanafunzi wa kike wamekuwa na tabia ya kuyakimbia masomo ya sayansi na kuwaachia watoto wa kikume madai kuwa masomo hayo ni magumu kitu ambacho siyo kweli.
Alisema kuwa hivi sasa MIST inao utaratibu wa kutoa mafunzo maalumu kwa ajili ya somo la Hisabati kwa watoto wa kike wanaokuwa wamemaliza elimu ya sekondari.
"Wale wanaokuwa wamefaulu vizuri huwa serikali inaingia gharama ya kuwasomesha kwa muda wote wanaokuwepo hapa taasisi lengo likiwa ni kuwahamasisha kuyapenda masomo ya sayansi" alisema Msambichaka.
Profesa Msambichaka alisema kuwa mwaka 2008, wanafunzi wa kike 13 walifanya masomo hayo maalumu, ambapo kwa mwaka jana waliojitokeza walikuwa ni zaidi ya 50.
Nao washiriki wa semina hiyo, wakizungumza kwa nyakati tofauti na Uhuru, walisema kuwa wanashukuru kwa kupata semina hiyo kwani ni ukweli kuwa watoto wa kike wapo nyuma.
Walisema kuwa wazazi wengi huwa wanawaona watoto wa kiume kuwa ndio wanaopaswa kusoma na wao kupenda kufanyishwa kazi za nyumbani hivyo huwa na muda kidogo wa kujisomea tofauti na wenzao wanaume.
"Tunataka kuiambia jamii kuwa tulikuwa nyuma kutokana na mfumo dume uliojenga kwa muda mrefu...watoto wa kike tulikuwa tunaonekana kwamba hatuwezi kusoma kwani mzazi aliyekuwa anamsomsemesha mtoto wa kike alikuwa akionekana anapoteza muda" walisema.
WHO YAISAIDIA TANZANIA FRIJI KUMI ZA KUHIFADHIA DAMU SALAMA
SHIRIKA la Afya Duniani (WHO),limetoa msaada wa friji kumi za kuhifadhia damu kwa Tanzania, kutokana na mafanikio makubwa yaliyoyafikiwa kwa muda mfupi tangu mpango wa damu salama uanzishwe mwaka 2005.
Imeelezwa kuwa hatua hiyo ya WHO ni kuichangia mpango wa damu salama nchini.
Hayo yamo katika salamu za Mkurugenzi wa shirika hilo,barani Afrika Dk.Luis Gomes Sambo, zilizotolewa katika kilele cha maadhimisho ya siku ya kuchangia damu duniani, ambapo kitaifa ilifanyika katika viwanja vya Ruanda Nzovwe jijini mbeya.
Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo yaliyotanguliwa na maandamano kutoka kituo cha mafuta Oil Com kilichopo Soweto hadi katika viwanja hivyo, alikuwa ni Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Profesa David Mwakyusa.
Sambo alisema kuwa tunaposherehekea na kuwatambua wachangia damu kwa hiyari, kwa ‘zawadi ya uhai’ ni muhimu kukumbuka kuwa ongezeko la wachangiaji damu hao mara kwa mara ndio njia pekee ya kuhakikisha upatikanaji wa damu salama kwa kila mgonjwa.Mkurugenzi huyo wa WHO barani afrika alisema:
”Mahitaji ya damu barani Afrika yanaongozwa na tatizo la vifo vya kina mama hadi kufikia elfu moja ambapo kwa watoto laki moja wanaozaliwa hai, zaidi ya asilimia 40 ya vifo vyao husababishwa na kutokwa damu”.
Aliongeza kuwa inakadiriwa kuwa asilimia 90 ya vifo milioni moja kila mwaka duniani kote, kutokana na ugonjwa wa maralia hutokea katika bara la afrika wakati kwa sehemu nyingine vifo hivyo vinavyotokana na maralia kali na ukosefu wa damu hufikia hadi asilimia saba na nusu.Dk.
Sambo alisema WHO limeunda mkakati wa damu salama mnamo mwaka 2001 nia ikiwa ni kulenga utoshelevu pamoja na usalama wa damu na tangu wakati huo kumekuwa na maendeleo mazuri katika kukusanya na kupima damu pia kuzuia magonjwa yanayoenea kwa damu.
“Lengo mojawapo katika mkakati huu ni kila nchi iweze kuchangia kwa hiari sio chini ya asilimia 80 ya mahitaji yake ya damu ifikapo mwaka 2012” alisema Dk.Sambo.
Aliongeza kuwa zaidi ya asilimia 50 ya nchi wanachama wamefikia lengo hilo ambapo nchi kumi na mbili kati ya 46 hukusanya damu yote inayohitajika kutoka kwa wachangia damu kwa hiari.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo, zaidi ya lita milioni 3.2 ya damu inakusanywa barani humu ila hata hivyo kuna upungufu kutokana na mahitaji ya lita milioni nane kwa mwaka hivyo juhudi zaidi zinahitajika ili kufikia lengo hilo.
Naye Meneja wa Mpango wa Damu salama nchini, Efespar Nkya,alisema hapo awali kulikuwa hakuna mfumo uliokuwa ukisimamia na kuratibu huduma za upatikanaji na upimaji damu uliokuwa ukizingatia ubora wa viwango.
Nkya alisema mfumo huu unategemea wachangiaji ndugu,marafiki na wakati mwingine watu wanaolipwa na kuwa mfumo huo una kiwango kiwango kikubwa cha maambukizi ya magonjwa kupitia kwenye damu, upungufu wa damu mara kwa mara na kukosekana.
Imeelezwa kuwa hatua hiyo ya WHO ni kuichangia mpango wa damu salama nchini.
Hayo yamo katika salamu za Mkurugenzi wa shirika hilo,barani Afrika Dk.Luis Gomes Sambo, zilizotolewa katika kilele cha maadhimisho ya siku ya kuchangia damu duniani, ambapo kitaifa ilifanyika katika viwanja vya Ruanda Nzovwe jijini mbeya.
Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo yaliyotanguliwa na maandamano kutoka kituo cha mafuta Oil Com kilichopo Soweto hadi katika viwanja hivyo, alikuwa ni Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Profesa David Mwakyusa.
Sambo alisema kuwa tunaposherehekea na kuwatambua wachangia damu kwa hiyari, kwa ‘zawadi ya uhai’ ni muhimu kukumbuka kuwa ongezeko la wachangiaji damu hao mara kwa mara ndio njia pekee ya kuhakikisha upatikanaji wa damu salama kwa kila mgonjwa.Mkurugenzi huyo wa WHO barani afrika alisema:
”Mahitaji ya damu barani Afrika yanaongozwa na tatizo la vifo vya kina mama hadi kufikia elfu moja ambapo kwa watoto laki moja wanaozaliwa hai, zaidi ya asilimia 40 ya vifo vyao husababishwa na kutokwa damu”.
Aliongeza kuwa inakadiriwa kuwa asilimia 90 ya vifo milioni moja kila mwaka duniani kote, kutokana na ugonjwa wa maralia hutokea katika bara la afrika wakati kwa sehemu nyingine vifo hivyo vinavyotokana na maralia kali na ukosefu wa damu hufikia hadi asilimia saba na nusu.Dk.
Sambo alisema WHO limeunda mkakati wa damu salama mnamo mwaka 2001 nia ikiwa ni kulenga utoshelevu pamoja na usalama wa damu na tangu wakati huo kumekuwa na maendeleo mazuri katika kukusanya na kupima damu pia kuzuia magonjwa yanayoenea kwa damu.
“Lengo mojawapo katika mkakati huu ni kila nchi iweze kuchangia kwa hiari sio chini ya asilimia 80 ya mahitaji yake ya damu ifikapo mwaka 2012” alisema Dk.Sambo.
Aliongeza kuwa zaidi ya asilimia 50 ya nchi wanachama wamefikia lengo hilo ambapo nchi kumi na mbili kati ya 46 hukusanya damu yote inayohitajika kutoka kwa wachangia damu kwa hiari.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo, zaidi ya lita milioni 3.2 ya damu inakusanywa barani humu ila hata hivyo kuna upungufu kutokana na mahitaji ya lita milioni nane kwa mwaka hivyo juhudi zaidi zinahitajika ili kufikia lengo hilo.
Naye Meneja wa Mpango wa Damu salama nchini, Efespar Nkya,alisema hapo awali kulikuwa hakuna mfumo uliokuwa ukisimamia na kuratibu huduma za upatikanaji na upimaji damu uliokuwa ukizingatia ubora wa viwango.
Nkya alisema mfumo huu unategemea wachangiaji ndugu,marafiki na wakati mwingine watu wanaolipwa na kuwa mfumo huo una kiwango kiwango kikubwa cha maambukizi ya magonjwa kupitia kwenye damu, upungufu wa damu mara kwa mara na kukosekana.
MBEYA YATAWALIWA NA MAUJI MFULULIZO.
>WENGINE WAWILI WAUAWA NDANI YA NYUMBA KISHA KUCHOMWA MOTO.
MWANAMKE mmoja wa kijiji cha Mwaoga-Makongorosi, amekufa papo hapo baada ya kukatwa katwa mapanga na mwanaume ambaye naye alikamatwa na wananchi wenye hasira kali na kuuawa.
Tukio hilo la aina yake linalodaiwa chanzo ni wivu wa kimapenzi, limetokea jana saa 7:40 mchana, katika kijiji hicho kilichopo wilayani Chunya mkoani Mbeya.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kaimu Kamanda wa polisi mkoani hapa, Monica Madembwe, alisema kuwa marehemu wote wawili hawajaweza kufahamika majina ya.
Monica alisema kuwa mwanamke huyo mwenye umri kati ya miaka 30-35, akiwa katika barabara ya Mkwajuni kwenda Makongorosi, alishambuliwa na mwanaume huyo mwenye umri kati ya miaka 20-25 kwa kukatwa katwa mapanga na kufariki papo hapo.
Kaimu Kamanda Monica alisema baada ya kufanya mauaji hayo, wananchi wenye hasira kali walimkamata na kumshambulia kwa mawe, fimbo na marungu hadi na yeye kufariki.
Aliongeza kuwa hakuna mtu ama watu waliokamatwa kuhusiana na tukio hilo, ambalo chake chake inasadikiwa ni wivu wa kimapenzi.Uchunguzi zaidi unaendelea.
Katika tukio lingine lilitokea kijiji cha Itimba-Utengule wilaya ya Mbeya vijijini, watu wawili wameuawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani wakiwa ndani ya nyumba yao.
Monica aliwataja marehemu hao kuwa ni Merry Mpenzu (50) na William Mpenzu (30).
Akielezea zaidi tukio hilo, alisema marehemu hao wawili wakiwa ndani ya nyumba walivamiwa na watu wasiofahamika na kupigwa na kitu kizito vichwani, kufungiwa mlango na baadaye nyumba hiyo kuwashwa moto.
"Nyumba yao ilikuwa imeeezekwa kwa nyasi, hivyo baada ya marehemu hao kuuawa, wauaji hao waliezua paa la nyumba hiyo na kulitumia kuchoma moto nyumba hiyo huku marehemu hao wakiwa ndani" alisema Monica.
Uchunguzi zaidi kujua chanzo cha mauaji hayo pamoja na kuwasaka watuhumiwa unaendelea kufanywa.Wakati huo huo mkazi wa kijiji cha Hatelele, wilayani Mbozi ameuawa kwa kukatwa na kitu chenye ncha kikali kichwani.
Marehemu ametajwa kuwa ni Evance Halele (29), ambaye mwili wake ulikutwa umetupwa kwenye mtaro wa barabara.
Imedaiwa kuwa marehemu alikuwa anajishughulisha na matukio ya wizi na hakuna mtu aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo.
MWANAMKE mmoja wa kijiji cha Mwaoga-Makongorosi, amekufa papo hapo baada ya kukatwa katwa mapanga na mwanaume ambaye naye alikamatwa na wananchi wenye hasira kali na kuuawa.
Tukio hilo la aina yake linalodaiwa chanzo ni wivu wa kimapenzi, limetokea jana saa 7:40 mchana, katika kijiji hicho kilichopo wilayani Chunya mkoani Mbeya.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kaimu Kamanda wa polisi mkoani hapa, Monica Madembwe, alisema kuwa marehemu wote wawili hawajaweza kufahamika majina ya.
Monica alisema kuwa mwanamke huyo mwenye umri kati ya miaka 30-35, akiwa katika barabara ya Mkwajuni kwenda Makongorosi, alishambuliwa na mwanaume huyo mwenye umri kati ya miaka 20-25 kwa kukatwa katwa mapanga na kufariki papo hapo.
Kaimu Kamanda Monica alisema baada ya kufanya mauaji hayo, wananchi wenye hasira kali walimkamata na kumshambulia kwa mawe, fimbo na marungu hadi na yeye kufariki.
Aliongeza kuwa hakuna mtu ama watu waliokamatwa kuhusiana na tukio hilo, ambalo chake chake inasadikiwa ni wivu wa kimapenzi.Uchunguzi zaidi unaendelea.
Katika tukio lingine lilitokea kijiji cha Itimba-Utengule wilaya ya Mbeya vijijini, watu wawili wameuawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani wakiwa ndani ya nyumba yao.
Monica aliwataja marehemu hao kuwa ni Merry Mpenzu (50) na William Mpenzu (30).
Akielezea zaidi tukio hilo, alisema marehemu hao wawili wakiwa ndani ya nyumba walivamiwa na watu wasiofahamika na kupigwa na kitu kizito vichwani, kufungiwa mlango na baadaye nyumba hiyo kuwashwa moto.
"Nyumba yao ilikuwa imeeezekwa kwa nyasi, hivyo baada ya marehemu hao kuuawa, wauaji hao waliezua paa la nyumba hiyo na kulitumia kuchoma moto nyumba hiyo huku marehemu hao wakiwa ndani" alisema Monica.
Uchunguzi zaidi kujua chanzo cha mauaji hayo pamoja na kuwasaka watuhumiwa unaendelea kufanywa.Wakati huo huo mkazi wa kijiji cha Hatelele, wilayani Mbozi ameuawa kwa kukatwa na kitu chenye ncha kikali kichwani.
Marehemu ametajwa kuwa ni Evance Halele (29), ambaye mwili wake ulikutwa umetupwa kwenye mtaro wa barabara.
Imedaiwa kuwa marehemu alikuwa anajishughulisha na matukio ya wizi na hakuna mtu aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo.
Wednesday, June 3, 2009
WAPATA HATI SAFI YA UKAGUZI WA HESABU
HALMASHAURI ya wilaya ya Chunya mkoani Mbeya, ni miongoni mwa halmashauri 54 nchini, zilizofanikiwa kupata hati safi ya ukaguzi wa hesabu kwa mwaka wa fedha 2007/2008.
Hilo limetokana na halmashauri kuwa na watumishi wenye uwezo na pia kitengo cha ukaguzi wa ndani kufanya ukaguzi wa mara kwa mara katika idara za halmashauri hiyo.
Mkaguzi wa ndani wa halmashauri hiyo, Saimon Minja, aliyasema hayo jana alipokuwa akizungumzia kuhusu jitihada zinazofanywa na kitengo hicho muhimu katika kuhakikisha halmashauri hiyo inasonga mbele.
Minja alisema kwa kitengo hicho kufanya ukaguzi wa mara kwa mara, huwa inasaidia wahusika kurekebisha makosa yao na hivyo anapokuja mkaguzi wa nje, huwa anakuta matatizo yote yameisharekebishwa.
"Pia kitu kingine kilichotusaidia kupata hati safi ni ushirikiano mkubwa uliopo kati ya kitengo cha ukaguzi wa ukaguzi wa ndani na Mkurugenzi Maurice Sapanjo, hali ambayo inafanya mazingira ya kazi kuwa rahisi" alisema Minja.
Aliongeza kuwa Mkurugenzi Sapanjo amekuwa anatumia taarifa za kitengo hicho kuwakemea na pia kuwashauri wakuu wa idara kutokana na taarifa anazokuwa amefikishwa mezani pake.
Alisema Changamoto waliyonayo hivi sasa ni ukubwa wa wilaya hiyo hivyo kuwa kikwazo kwao kuweza kufika maeneo yote ya wilaya hiyo kwa ajili ya kufanya ukaguzi wa ndani wa hesabu.
Ofisa huyo wa wilaya alisema vile vile kitengo hicho cha ukaguzi wa ndani hakina usafiri hali inayowalazimu kuomba magari kutoka idara nyigine, na inapotokea magari hayo kuwa na kazi hulazimika kusubiri ili kwenda kutekeleza majukumu yao.
Minja alisema:"Kuna dhana potofu iliyopo wilayani hapa kwa baadhi ya watu wakiwemo wana-siasa kuwa Mkaguzi wa ndani anatakiwa kuwakamata watu wanaobainika kufuja fedha za halmashauri, kitu ambacho siyo sahihi".
Alifafanua zaidi kauli yake hiyo kuwa wao wanachokifanya mara baada ya kubaini ubadhirifu wa fedha ndani ya idara yoyote huwa wanazifikishga taarifa kwa Mkurugenzi kwa hatua zaidi na wao huwa hawana uwezo wa kuwa polisi wa kuwakamata wabadhirifu hao.
Minja aliongeza kuwa pia kitengo hicho kinakabiriwa na upungufu wa watumishi kwani kinao wawili tu na mmoja hivi sasa yupo masomoni, hali inayofanya utendaji wa kazi kuwa mgumu hasa ukizingatia kuwa wilaya ina eneo kubwa kuliko wilaya nyigine zote mkoani hapa.
Hilo limetokana na halmashauri kuwa na watumishi wenye uwezo na pia kitengo cha ukaguzi wa ndani kufanya ukaguzi wa mara kwa mara katika idara za halmashauri hiyo.
Mkaguzi wa ndani wa halmashauri hiyo, Saimon Minja, aliyasema hayo jana alipokuwa akizungumzia kuhusu jitihada zinazofanywa na kitengo hicho muhimu katika kuhakikisha halmashauri hiyo inasonga mbele.
Minja alisema kwa kitengo hicho kufanya ukaguzi wa mara kwa mara, huwa inasaidia wahusika kurekebisha makosa yao na hivyo anapokuja mkaguzi wa nje, huwa anakuta matatizo yote yameisharekebishwa.
"Pia kitu kingine kilichotusaidia kupata hati safi ni ushirikiano mkubwa uliopo kati ya kitengo cha ukaguzi wa ukaguzi wa ndani na Mkurugenzi Maurice Sapanjo, hali ambayo inafanya mazingira ya kazi kuwa rahisi" alisema Minja.
Aliongeza kuwa Mkurugenzi Sapanjo amekuwa anatumia taarifa za kitengo hicho kuwakemea na pia kuwashauri wakuu wa idara kutokana na taarifa anazokuwa amefikishwa mezani pake.
Alisema Changamoto waliyonayo hivi sasa ni ukubwa wa wilaya hiyo hivyo kuwa kikwazo kwao kuweza kufika maeneo yote ya wilaya hiyo kwa ajili ya kufanya ukaguzi wa ndani wa hesabu.
Ofisa huyo wa wilaya alisema vile vile kitengo hicho cha ukaguzi wa ndani hakina usafiri hali inayowalazimu kuomba magari kutoka idara nyigine, na inapotokea magari hayo kuwa na kazi hulazimika kusubiri ili kwenda kutekeleza majukumu yao.
Minja alisema:"Kuna dhana potofu iliyopo wilayani hapa kwa baadhi ya watu wakiwemo wana-siasa kuwa Mkaguzi wa ndani anatakiwa kuwakamata watu wanaobainika kufuja fedha za halmashauri, kitu ambacho siyo sahihi".
Alifafanua zaidi kauli yake hiyo kuwa wao wanachokifanya mara baada ya kubaini ubadhirifu wa fedha ndani ya idara yoyote huwa wanazifikishga taarifa kwa Mkurugenzi kwa hatua zaidi na wao huwa hawana uwezo wa kuwa polisi wa kuwakamata wabadhirifu hao.
Minja aliongeza kuwa pia kitengo hicho kinakabiriwa na upungufu wa watumishi kwani kinao wawili tu na mmoja hivi sasa yupo masomoni, hali inayofanya utendaji wa kazi kuwa mgumu hasa ukizingatia kuwa wilaya ina eneo kubwa kuliko wilaya nyigine zote mkoani hapa.
CHUNYA WAKAMATA MAKOKORO YENYE THAMANI YA ZAIDI YA SH.MILIONI 20
MAKOKORO 103 yenye thamani ya zaidi ya shilingi 20,600,000, yamekamatwa katika maeneo ya Isanzu na Udinde yaliyopo pembezoni mwa Ziwa Rukwa, wilayani Chunya.
Imeelezwa kuwa wamiliki wa makokoro hayo hawakuweza kutiwa mbaroni baada ya kuwahi kukimbia na kuyatelekeza makokoro hayo.
Akizungumza Ofisa Uvuvi wa wilaya hiyo, Christina Potta, alisema kuwa operesheni ya kuyakamata makokoro hayo ilifanyika kati ya Mei 3, na hadi 14, mwaka huu katika maeneo hayo yaliyopo Ziwa Rukwa, upande wa wilaya ya Chunya.
Christina alisema kuwa matumizi ya makokoro huwa yanapelekea upungufu wa samaki kwani nyavu za aina hiyo (makokoro), kutokana na kuwa na macho madogo zinapovutwa huharibu viota, mayai, vifaranga vya samaki na hivyo kuua vizazi vya samaki.
Aliongeza kuwa katika zoezi hilo, wilaya hiyo ilishirikiana na kikosi cha doria cha uvuvi cha Kanda ya Kasanga, kilichopo mkoani Rukwa.
"Kazi ya kutupa makokoro ziwa Rukwa huwa inafanywa nyakati za usiku, hivyo hutuwia vigumu kuwatia mbaroni watuhumiwa na huwa tukienda mchana huwa ntunafanikiwa kuyakukuta makokoro lakini wamiliki wake huwa wanafanikiwa kukimbia" alisema Christina.
Ofisa Uvuvi huyo wa wilaya alisema ili kukabiriana na wavuvi ambao wamekuwa watumiaji wakubwa wa makokoro, wilaya imekuwa inajitahidi kutoa elimu kwa wananchi juu athari za makokoro.Christina alisema:
"Tunaendelea kushirikiana na viongozi wa vijiji katika utoaji elimu hali iliyopelekea baadhi ya wavuvi kwa hiyari yao wenyewe, kuamua kuanza kusalimisha makokoro waliyokuwa wanayatumia".
Aliongeza kuwa changamoto kubwa wanayokutana nayo ni kuwa watumiaji wa makokoro hayo kwa kutumia simu za kiganjani, wamekuwa wanapeana taarifa kila unapofanyika msako hali inayowawia vigumu kuwatia mbaroni watuhumiwa ili kuwafikisha mbele ya sheria.
Alisema wilaya katika kukabiriana na tatizo hilo, imefanikiwa kukamilisha matengenzo ya Boti ya doria ambayo tayari imetumbukizwa kwenye Ziwa Rukwa, ambayo itasaidia sana kukabiriana na wavuvi wanaotumia makokoro katika shughuli zao za uvuvi.
Imeelezwa kuwa wamiliki wa makokoro hayo hawakuweza kutiwa mbaroni baada ya kuwahi kukimbia na kuyatelekeza makokoro hayo.
Akizungumza Ofisa Uvuvi wa wilaya hiyo, Christina Potta, alisema kuwa operesheni ya kuyakamata makokoro hayo ilifanyika kati ya Mei 3, na hadi 14, mwaka huu katika maeneo hayo yaliyopo Ziwa Rukwa, upande wa wilaya ya Chunya.
Christina alisema kuwa matumizi ya makokoro huwa yanapelekea upungufu wa samaki kwani nyavu za aina hiyo (makokoro), kutokana na kuwa na macho madogo zinapovutwa huharibu viota, mayai, vifaranga vya samaki na hivyo kuua vizazi vya samaki.
Aliongeza kuwa katika zoezi hilo, wilaya hiyo ilishirikiana na kikosi cha doria cha uvuvi cha Kanda ya Kasanga, kilichopo mkoani Rukwa.
"Kazi ya kutupa makokoro ziwa Rukwa huwa inafanywa nyakati za usiku, hivyo hutuwia vigumu kuwatia mbaroni watuhumiwa na huwa tukienda mchana huwa ntunafanikiwa kuyakukuta makokoro lakini wamiliki wake huwa wanafanikiwa kukimbia" alisema Christina.
Ofisa Uvuvi huyo wa wilaya alisema ili kukabiriana na wavuvi ambao wamekuwa watumiaji wakubwa wa makokoro, wilaya imekuwa inajitahidi kutoa elimu kwa wananchi juu athari za makokoro.Christina alisema:
"Tunaendelea kushirikiana na viongozi wa vijiji katika utoaji elimu hali iliyopelekea baadhi ya wavuvi kwa hiyari yao wenyewe, kuamua kuanza kusalimisha makokoro waliyokuwa wanayatumia".
Aliongeza kuwa changamoto kubwa wanayokutana nayo ni kuwa watumiaji wa makokoro hayo kwa kutumia simu za kiganjani, wamekuwa wanapeana taarifa kila unapofanyika msako hali inayowawia vigumu kuwatia mbaroni watuhumiwa ili kuwafikisha mbele ya sheria.
Alisema wilaya katika kukabiriana na tatizo hilo, imefanikiwa kukamilisha matengenzo ya Boti ya doria ambayo tayari imetumbukizwa kwenye Ziwa Rukwa, ambayo itasaidia sana kukabiriana na wavuvi wanaotumia makokoro katika shughuli zao za uvuvi.
TAMISEMI WAPOKEA MALUMBANO KATI YA KAPUNGA NA ELIZABETH
WAZIRI wa Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI),Selina Kombani, amesema kuwa ofisi yake imepokea taarifa za kuwepo malumbano kati ya watendaji na viongozi wa siasa jijini Mbeya.
Alisema lakini serikali haiwezi kuzifanyia kazi hizo za malalamiko bila ya kuzifanyia utafiti, hivyo kuwataka waliopeleka taarifa hizo kuvuta subira.
“Nawaomba wale walioniletea taarifa hizi ofisini kwangu kuwa na subira ili niweze kuniwezesha kufanya utafiti kwa nia ya kutoa majibu yaliyo sahihi” alisema Selina.
Hayo aliyasema jana mjini hapa, mara baada ya kufungua semina ya madiwani wanawake mkoani hapa,katika ukumbi wa Benjamini Mkapa yenye nia ya kuwawezesha kuwa na ujasiri katika kugombea nafasi za uongozi.
Waziri wa TAMISEMI alisema ofisi yake ilishapokea taarifa za kuwepo malumbano kati ya watendaji na viongozi wa kisiasa wa halmashauri ya jiji la Mbeya.
Aliongeza kuwa hatua za awali zilizochukuliwa ni kufanya utafiti wa chanzo cha malumbano hayo, ambapo baada ya kubainika chanzo cha tatizo hilo ndipo utatolewa uamuzi utakaokuwa na nia ya kuutendea haki kila upande.Selina alisema:
”Lengo la TAMISEMI kukaa kimya muda mrefu bila ya kutoa maamuzi ya malalamiko hayo (hakutaja kundi lililopeleka kwakwe), ni kuhakikisha uamuzi unaotolewa hauumizi upande mmoja au kuwagawa wahusika”.
Waziri huyo alikiri kuwa ni kweli ofisi ama sehemu yoyote inayokuwa na malumbano, shughuli za utendaji hushuka lakini hilo haliwezi kuifanya serikali ikatoa maamuzi yasiyofanyiwa utafiti wa kina hivyo kuwataka wananchi kuwa wavumilivu.
“Nakubaliana nanyi kuwa sehemu kunapokuwa na malumbano ya namna hii kazi nyingi zinafanyika kwa kiwango cha chini…lakini kwa kuwa hazijasimama kabisa,niwaombe wananchi wa Mbeya na taifa kwa ujumla kuvuta subira ili uamuzi utakaotolewa uwe na manufaa kwa wote” alisema Selina.
Alisema utaratibu uliopo TAMISEMI ni kuwa wanafanyia kazi maelezo yaliyotolewa na pande zote mbili kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na maofisa wake na kwamba vikao vitaketi na kupitia taarifa hiyo ili kufikia uamuzi.
Malumbano yaliyofikishwa TAMISEMI ni kati ya mkurugenzi wa jiji la Mbeya, Elibeth Munuo na Meya wake Athanas Kapunga, ambapo kwa nyakati tofauti kila mmoja amekuwa akimlaumu mwenzake kuwa ni chanzo cha matatizo mbalimbali katika halmashauri hiyo.
Alisema lakini serikali haiwezi kuzifanyia kazi hizo za malalamiko bila ya kuzifanyia utafiti, hivyo kuwataka waliopeleka taarifa hizo kuvuta subira.
“Nawaomba wale walioniletea taarifa hizi ofisini kwangu kuwa na subira ili niweze kuniwezesha kufanya utafiti kwa nia ya kutoa majibu yaliyo sahihi” alisema Selina.
Hayo aliyasema jana mjini hapa, mara baada ya kufungua semina ya madiwani wanawake mkoani hapa,katika ukumbi wa Benjamini Mkapa yenye nia ya kuwawezesha kuwa na ujasiri katika kugombea nafasi za uongozi.
Waziri wa TAMISEMI alisema ofisi yake ilishapokea taarifa za kuwepo malumbano kati ya watendaji na viongozi wa kisiasa wa halmashauri ya jiji la Mbeya.
Aliongeza kuwa hatua za awali zilizochukuliwa ni kufanya utafiti wa chanzo cha malumbano hayo, ambapo baada ya kubainika chanzo cha tatizo hilo ndipo utatolewa uamuzi utakaokuwa na nia ya kuutendea haki kila upande.Selina alisema:
”Lengo la TAMISEMI kukaa kimya muda mrefu bila ya kutoa maamuzi ya malalamiko hayo (hakutaja kundi lililopeleka kwakwe), ni kuhakikisha uamuzi unaotolewa hauumizi upande mmoja au kuwagawa wahusika”.
Waziri huyo alikiri kuwa ni kweli ofisi ama sehemu yoyote inayokuwa na malumbano, shughuli za utendaji hushuka lakini hilo haliwezi kuifanya serikali ikatoa maamuzi yasiyofanyiwa utafiti wa kina hivyo kuwataka wananchi kuwa wavumilivu.
“Nakubaliana nanyi kuwa sehemu kunapokuwa na malumbano ya namna hii kazi nyingi zinafanyika kwa kiwango cha chini…lakini kwa kuwa hazijasimama kabisa,niwaombe wananchi wa Mbeya na taifa kwa ujumla kuvuta subira ili uamuzi utakaotolewa uwe na manufaa kwa wote” alisema Selina.
Alisema utaratibu uliopo TAMISEMI ni kuwa wanafanyia kazi maelezo yaliyotolewa na pande zote mbili kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na maofisa wake na kwamba vikao vitaketi na kupitia taarifa hiyo ili kufikia uamuzi.
Malumbano yaliyofikishwa TAMISEMI ni kati ya mkurugenzi wa jiji la Mbeya, Elibeth Munuo na Meya wake Athanas Kapunga, ambapo kwa nyakati tofauti kila mmoja amekuwa akimlaumu mwenzake kuwa ni chanzo cha matatizo mbalimbali katika halmashauri hiyo.
Saturday, May 30, 2009
WASAHINDI WATATU WA MISS MBEYA 2009
MARY KAGALI MISS MBEYA 2009
MARY Kagali (19), ameshinda taji la Miss Mbeya 2009, baada ya kuwashinda warembo wengine kumi na mmoja waliojitokeza kuwania taji hilo na kujinyakulia zawadi ya sh.800,000.
Shindano hilo, liliingia dosari baada ya kiongozi wa majaji,Tasha Jim kumtangaza mrembo, Raulensia Laurency kuwa mshindi namba mbili, hali iliyopelekea ukumbi mzima kuzomea kupinga matokeo hayo.
Mamia ya mashabiki lukuki waliohudhuria shindano hilo, lililofanyikia katika ukumbi wa Benjamin Mkapa, walifikia hatua hiyo baada ya Raulensia kushindwa kuonyesha uwezo katika kutembea pia kwenye kujibu swali ili kumpima ufahamu wake.
Kwa kushinda nafasi hiyo, mrembo huyo alijinyakulia zawadi ya shilingi 400,000 huku nafasi ya tatu ikitwalia na Agnes Mpona, aliyezawadiwa shilingi 200,000.
Warembo hao watatu wataungana na mrembo aliyeshika ya nne, Jacqueline Magayane kuingia katika shindano la kumsaka mrembo wa kanda ya nyanda za juu kusini.
Awali warembo hao kumi na wawili walipita jukwaani na kuonyesha mavazi ya ubunifu, ufukweni na baadaye kumaliza na vazi la kutokea jioni, ambapo walichujwa na kupatikana tano bora.
Waliofanikiwa kuingia tano ni Jacqueline Magayane, Neema Mushi, Agnes Sasawata, Raulensia Laurency na Mary Kagali ambaye kila alipokuwa akipita jukwaani ukumbi mzima ulikuwa unalipuka kwa kofi na mayowe kumshangilia.
Mashabiki wa shindano hilo, walimtupia lawama jaji mkuu, Tasha Jim, kwa kuharibu shindano hilo kufuatia kumtangaza Raulensia kuwa mshindi wa pili ambaye wengi waliona kuwa hakustahili kutwaa nafasi hiyo.
Shindano hilo, lilipambwa na burudani kutoka kikundi cha muziki wa taarabu cha Victoria Modern kutoka Dar es Salaam lenye wasani wa kike watupu pamoja na kundi la muziki kutoka jijini Mbeya lililo chini ya msanii Robby Matunda.
Shindano hilo, liliingia dosari baada ya kiongozi wa majaji,Tasha Jim kumtangaza mrembo, Raulensia Laurency kuwa mshindi namba mbili, hali iliyopelekea ukumbi mzima kuzomea kupinga matokeo hayo.
Mamia ya mashabiki lukuki waliohudhuria shindano hilo, lililofanyikia katika ukumbi wa Benjamin Mkapa, walifikia hatua hiyo baada ya Raulensia kushindwa kuonyesha uwezo katika kutembea pia kwenye kujibu swali ili kumpima ufahamu wake.
Kwa kushinda nafasi hiyo, mrembo huyo alijinyakulia zawadi ya shilingi 400,000 huku nafasi ya tatu ikitwalia na Agnes Mpona, aliyezawadiwa shilingi 200,000.
Warembo hao watatu wataungana na mrembo aliyeshika ya nne, Jacqueline Magayane kuingia katika shindano la kumsaka mrembo wa kanda ya nyanda za juu kusini.
Awali warembo hao kumi na wawili walipita jukwaani na kuonyesha mavazi ya ubunifu, ufukweni na baadaye kumaliza na vazi la kutokea jioni, ambapo walichujwa na kupatikana tano bora.
Waliofanikiwa kuingia tano ni Jacqueline Magayane, Neema Mushi, Agnes Sasawata, Raulensia Laurency na Mary Kagali ambaye kila alipokuwa akipita jukwaani ukumbi mzima ulikuwa unalipuka kwa kofi na mayowe kumshangilia.
Mashabiki wa shindano hilo, walimtupia lawama jaji mkuu, Tasha Jim, kwa kuharibu shindano hilo kufuatia kumtangaza Raulensia kuwa mshindi wa pili ambaye wengi waliona kuwa hakustahili kutwaa nafasi hiyo.
Shindano hilo, lilipambwa na burudani kutoka kikundi cha muziki wa taarabu cha Victoria Modern kutoka Dar es Salaam lenye wasani wa kike watupu pamoja na kundi la muziki kutoka jijini Mbeya lililo chini ya msanii Robby Matunda.
MHANDISI MSHAURI WA MAJENGO MKOA WA MBEYA AMCHEFUA RC.
MKUU wa mkoa wa Mbeya, John Mwakipesile, amemuagiza Katibu Tawala, Beatha Swai, kumuondoa Mhandisi mshauri wa majengo, Aidan Ngwada, kufuatia kuboronga katika utendaji wake wa kazi.
Hatua hiyo imefikiwa kufuatia malalamiko mengi kutolewa kuhusu idara ya Uhandisi mkoani hapa, hali inayopelekea miradi mingi inayofanyika kuwa chini ya kiwango cha ubora.
Mwakipesile alifikia hatua hiyo jana katika kikao cha Kamati ya Ushauri ya mkoa (RCC), kilichofanyika jana katika ukumbi wa Dk.Ali Shein, baada ya wakuu wa wilaya watatu, kumnyoshea kidole Ngwada, kuwa kazi anazosimamia hazina kiwango.
Alisema kuwa idara hiyo ni mbovu ambapo fedha nyingi zinazotolewa na serikali kuu kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali zimekuwa zinatumika isivyo huku miradi hiyo ikiwa haina ubora wowote.
"Tumechoka na kazi mbovu za Uandisi katika serikali ya mkoa wa Mbeya na hatuwezi kuendelea kukaa kimya wakatri fedha za serikali zinatumika vibaya huku miradi ikiwa haina ubora unaotakiwa" alisema Mwakipesile.
Aliongeza kuwa hataki kuwa sehemu ya wizi huo unaofanyika katika idara hiyo na awali alishawahi kumtaka aliyekuwa Katibu Tawala mkoani hapa Assumpta Ndimbo, kumuondoa Mhandisi huyo lakini haelewi ni vipi anaendelea kushikilia wadhifa huo hadi leo.
Mkuu wa mkoa alisema:"Sitaki kuwa sehemu ya wizi huu, inawezekana wewe ni injinia mbovu, huna cheti na iwapo hivi vyote unavyo basi ni wazi unashirikiana na wengine katika wizi".
Alisema kuwa serikali imeajiri wahandisi kwa kila wilaya, lakini wamekuwa wanalipwa tu mishahara bila ya kufanya kazi zozote kutokana na ukiritimba unaofanywa na Ngwada wa kwenda kufanya kazi hizo badala ya kuziachia wilaya husika.
Akizungumza kwa hasira, Mwakipesile alisema hawezi kukubali yeye aonekane ni sehemu ya ubovu katika mkoa wa Mbeya, kwani kila siku amekuwa akipokea malamiko ya ujenzi mbovu wa barabara hasi nyumba za wakuu wa wilaya na makatibu Tawala wa wilaya.
"Hivyo nawaomba wajumbe tusiendelee kuchangia katika hili, kwani kwa kuwa Katibu Tawala Beatha yupo, amesikia na atalifanyia kazi...tumuachie hili mikononi mwake" alisema Mwakipesile.
Kufuatia hali ya hewa kuchafuka, mara baada ya Mkuu wa mkoa kumaliza kuitolea ufafabnuzi hoja hiyo iliyokuwa imeibuliwa na Wakuu wa wilaya za Chunya, Kyela na Mbeya, mnamo saa 7:20 mchana Ngwada alisimama na kutoka nje ya ukumbi na hakurejea tena hadi kikao hicho kinafungwa saa 9:00 alasiri.
Waandishi walipotoka nje ili kumuomba Ngwada atoe ufafanuzi kuhusu kilichotokea, aliwaomba wamuache kwani hajisikii vizuri na kuwa mapigo ya moyo (BP), hayapo salama.
Hatua hiyo imefikiwa kufuatia malalamiko mengi kutolewa kuhusu idara ya Uhandisi mkoani hapa, hali inayopelekea miradi mingi inayofanyika kuwa chini ya kiwango cha ubora.
Mwakipesile alifikia hatua hiyo jana katika kikao cha Kamati ya Ushauri ya mkoa (RCC), kilichofanyika jana katika ukumbi wa Dk.Ali Shein, baada ya wakuu wa wilaya watatu, kumnyoshea kidole Ngwada, kuwa kazi anazosimamia hazina kiwango.
Alisema kuwa idara hiyo ni mbovu ambapo fedha nyingi zinazotolewa na serikali kuu kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali zimekuwa zinatumika isivyo huku miradi hiyo ikiwa haina ubora wowote.
"Tumechoka na kazi mbovu za Uandisi katika serikali ya mkoa wa Mbeya na hatuwezi kuendelea kukaa kimya wakatri fedha za serikali zinatumika vibaya huku miradi ikiwa haina ubora unaotakiwa" alisema Mwakipesile.
Aliongeza kuwa hataki kuwa sehemu ya wizi huo unaofanyika katika idara hiyo na awali alishawahi kumtaka aliyekuwa Katibu Tawala mkoani hapa Assumpta Ndimbo, kumuondoa Mhandisi huyo lakini haelewi ni vipi anaendelea kushikilia wadhifa huo hadi leo.
Mkuu wa mkoa alisema:"Sitaki kuwa sehemu ya wizi huu, inawezekana wewe ni injinia mbovu, huna cheti na iwapo hivi vyote unavyo basi ni wazi unashirikiana na wengine katika wizi".
Alisema kuwa serikali imeajiri wahandisi kwa kila wilaya, lakini wamekuwa wanalipwa tu mishahara bila ya kufanya kazi zozote kutokana na ukiritimba unaofanywa na Ngwada wa kwenda kufanya kazi hizo badala ya kuziachia wilaya husika.
Akizungumza kwa hasira, Mwakipesile alisema hawezi kukubali yeye aonekane ni sehemu ya ubovu katika mkoa wa Mbeya, kwani kila siku amekuwa akipokea malamiko ya ujenzi mbovu wa barabara hasi nyumba za wakuu wa wilaya na makatibu Tawala wa wilaya.
"Hivyo nawaomba wajumbe tusiendelee kuchangia katika hili, kwani kwa kuwa Katibu Tawala Beatha yupo, amesikia na atalifanyia kazi...tumuachie hili mikononi mwake" alisema Mwakipesile.
Kufuatia hali ya hewa kuchafuka, mara baada ya Mkuu wa mkoa kumaliza kuitolea ufafabnuzi hoja hiyo iliyokuwa imeibuliwa na Wakuu wa wilaya za Chunya, Kyela na Mbeya, mnamo saa 7:20 mchana Ngwada alisimama na kutoka nje ya ukumbi na hakurejea tena hadi kikao hicho kinafungwa saa 9:00 alasiri.
Waandishi walipotoka nje ili kumuomba Ngwada atoe ufafanuzi kuhusu kilichotokea, aliwaomba wamuache kwani hajisikii vizuri na kuwa mapigo ya moyo (BP), hayapo salama.
Friday, May 29, 2009
TANROADS MBEYA WATAKIWA KUWASILISHA BAJETI
WAJUMBE wa kikao cha Bodi ya barabara mkoa wa Mbeya, wamemuagiza Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), mkoa kuhakikisha kuwa bajeti ya barabara inayotakiwa kupitishwa inapitiwa kwanza na kikao hicho.
Imeelezwa kuwa TANROADS wamekuwa wanapitisha bajeti hiyo na kuamua wao barabara za kuzitengeneza badala ya zile zinazotakiwa na wananchi wa wilaya husika.
Wakichangia katika kikao cha Bodi ya Barabara kilichofanyika jana.chini ya Uenyekiti wa Mkuu wa mkoa wa Mbeya,wajumbe hao walisema kuwa barabara zinazotengenezwa na TANROADS zinatakiwa kujibu kero za wananchi na siyo nje ya hapo.
Walisema kuwa hivyo kuanzia bajeti ijayo ni lazima kabla ya kupitishwa iwe inaletwa kwenye kikao hicho kujadiriwa ili barabara zitakazotengenezwa ziwe ni zile zinazopewa kipaumbele na wananchi na siyo wakala huyo wa barabara.
“Ni vyema hili lifanyiwe kazi ili barabara zile zinazotakiwa na wananchi kutokana na umuhimu wake ndizo zipewe kipaumbele cha kwanza na siyo zile ambazo TANROADS mmekuwa mnaziamua na kuzipangia bajeti bila ya kutushirikisha” walisema.
Imeelezwa kuwa TANROADS wamekuwa wanapitisha bajeti hiyo na kuamua wao barabara za kuzitengeneza badala ya zile zinazotakiwa na wananchi wa wilaya husika.
Wakichangia katika kikao cha Bodi ya Barabara kilichofanyika jana.chini ya Uenyekiti wa Mkuu wa mkoa wa Mbeya,wajumbe hao walisema kuwa barabara zinazotengenezwa na TANROADS zinatakiwa kujibu kero za wananchi na siyo nje ya hapo.
Walisema kuwa hivyo kuanzia bajeti ijayo ni lazima kabla ya kupitishwa iwe inaletwa kwenye kikao hicho kujadiriwa ili barabara zitakazotengenezwa ziwe ni zile zinazopewa kipaumbele na wananchi na siyo wakala huyo wa barabara.
“Ni vyema hili lifanyiwe kazi ili barabara zile zinazotakiwa na wananchi kutokana na umuhimu wake ndizo zipewe kipaumbele cha kwanza na siyo zile ambazo TANROADS mmekuwa mnaziamua na kuzipangia bajeti bila ya kutushirikisha” walisema.
MKANDARASI ABORONGA UJENZI WA BARABARA JIJINI MBEYA
SERIKALI mkoa wa Mbeya, imeuagiza uongozi wa halmashauri ya jiji la Mbeya, kutomkamilisha malipo mkandarasi aliyejenga barabara inayoanzia benki ya Stanbic, kuelekea Ikulu ndogo kwani imejengwa chini ya kiwango.Imeelezwa kuwa hadi sasa halmashauri tayari imemlipa Mkandarasi huyo shilingi milioni 43 kati ya milioni 132 anazotakiwa kulipwa kwa kazi hiyo.
Agizo hilo limetolewa jana na Mkuu wa mkoa wa Mbeya,John Mwakipesile, kufuatia malalamiko yaliyofikishwa ofisini kwake na wananchi wa eneo la Uzunguni,inapopita barabara hiyo kufuatia adha ya vumbi wanayoipata wakati barabara hiyo inajengwa kwa kiwango cha lami.
Mwakipesile alisema kuwa hata yeye kiwango cha utengenezaji wa barabara hiyo kilimtia mashaka,hali iliyopelekea kumuagiza mtaalamu kutoka Wakala wa barabara nchini (TANROADS), mkoa wa Mbeya kwenda kuifanyia ukaguzi ili kuona kama imejengwa kwa kiwango.
"Mtaalam niliyemtuma kutoka TANROADS aliikagua barabara hiyo na kubaini kuwa imejengwa chini ya kiwango kinachotakiwa...hivyo naagiza kuwa mkandarasi huyo asilipwe fedha zilizobaki hadi tujiridhishe na kazi iliyofanyika" alisema Mwakipesile.
Aliongeza kuwa wakazi wa eneo la Uzunguni wamekuwa wanampelelekea malalamiko kutokana na adha ya vumbi linalotimka katika barabara hiyo ambayo ilitakiwa kujengwa kwa kiwango cha lami.
Agizo hilo limetolewa jana na Mkuu wa mkoa wa Mbeya,John Mwakipesile, kufuatia malalamiko yaliyofikishwa ofisini kwake na wananchi wa eneo la Uzunguni,inapopita barabara hiyo kufuatia adha ya vumbi wanayoipata wakati barabara hiyo inajengwa kwa kiwango cha lami.
Mwakipesile alisema kuwa hata yeye kiwango cha utengenezaji wa barabara hiyo kilimtia mashaka,hali iliyopelekea kumuagiza mtaalamu kutoka Wakala wa barabara nchini (TANROADS), mkoa wa Mbeya kwenda kuifanyia ukaguzi ili kuona kama imejengwa kwa kiwango.
"Mtaalam niliyemtuma kutoka TANROADS aliikagua barabara hiyo na kubaini kuwa imejengwa chini ya kiwango kinachotakiwa...hivyo naagiza kuwa mkandarasi huyo asilipwe fedha zilizobaki hadi tujiridhishe na kazi iliyofanyika" alisema Mwakipesile.
Aliongeza kuwa wakazi wa eneo la Uzunguni wamekuwa wanampelelekea malalamiko kutokana na adha ya vumbi linalotimka katika barabara hiyo ambayo ilitakiwa kujengwa kwa kiwango cha lami.
TANROADS MBEYA WAWEKWA KITI MOTO.
WAJUMBE wa kikao cha Bodi ya barabara mkoa wa Mbeya, wamemuagiza Wakala wa Barabara nchini (TANROADS),mkoa kuhakikisha kuwa bajeti ya barabara inayotakiwa kupitishwa inapitiwa kwanza na kikao hicho.
Imeelezwa kuwa TANROADS wamekuwa wanapitisha bajeti hiyo na kuamua wao barabara za kuzitengeneza badala ya zile zinazotakiwa na wananchi wa wilaya husika.
Wakichangia katika kikao cha Bodi ya Barabara kilichofanyika jana.chini ya Uenyekiti wa Mkuu wa mkoa wa Mbeya,wajumbe hao walisema kuwa barabara zinazotengenezwa na TANROADS zinatakiwa kujibu kero za wananchi na siyo nje ya hapo.
Walisema kuwa hivyo kuanzia bajeti ijayo ni lazima kabla ya kupitishwa iwe inaletwa kwenye kikao hicho kujadiriwa ili barabara zitakazotengenezwa ziwe ni zile zinazopewa kipaumbele na wananchi na siyo wakala huyo wa barabara.
“Ni vyema hili lifanyiwe kazi ili barabara zile zinazotakiwa na wananchi kutokana na umuhimu wake ndizo zipewe kipaumbele cha kwanza na siyo zile ambazo TANROADS mmekuwa mnaziamua na kuzipangia bajeti bila ya kutushirikisha” walisema.
Waliongeza kuwa mabadiliko hayo yasipofanyika ni wazi hadi tunaingia kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2010,barabara nyingi zitakuwa zimetengenezwa lakini zitakuwa hazijibu utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2005-2010.
Walisema haiwezekani TANROADS wawe wanaamua barabara zipi za kutengenezwa, kupanga bajeti na kisha kuileta kwenye kikao cha Bodi ya Barabara kwa ajili ya kuwasomea tu wajumbe,hali ambayo inakuwa haisadii.
“Tuachane na utaratibu huu uliopo hivi sasa kwani barabara hizi ni zetu na nyie TANROADS ni wakala tu wa kuzisimamia….kwani wananchi ndio wanaoamua barabara ipi itengenezwe kutokana na umuhimu wake na siyo nyie ndio muwe mnawaamulia” walisema.
Kufuatia hali hiyo,Mkuu wa mkoa Mwakipesile alikubaliana na hoja hizo za wajumbe na kuwa kuanzia sasa bajeti hiyo iwe inaletwa kwenye kikao hicho,kujadiriwa kabla ya kuanza kutekelezwa ili barabara zenye umuhimu kwa wananchi ndizo zipewe kipaumbele kikubwa cha kutengenezwa.
Imeelezwa kuwa TANROADS wamekuwa wanapitisha bajeti hiyo na kuamua wao barabara za kuzitengeneza badala ya zile zinazotakiwa na wananchi wa wilaya husika.
Wakichangia katika kikao cha Bodi ya Barabara kilichofanyika jana.chini ya Uenyekiti wa Mkuu wa mkoa wa Mbeya,wajumbe hao walisema kuwa barabara zinazotengenezwa na TANROADS zinatakiwa kujibu kero za wananchi na siyo nje ya hapo.
Walisema kuwa hivyo kuanzia bajeti ijayo ni lazima kabla ya kupitishwa iwe inaletwa kwenye kikao hicho kujadiriwa ili barabara zitakazotengenezwa ziwe ni zile zinazopewa kipaumbele na wananchi na siyo wakala huyo wa barabara.
“Ni vyema hili lifanyiwe kazi ili barabara zile zinazotakiwa na wananchi kutokana na umuhimu wake ndizo zipewe kipaumbele cha kwanza na siyo zile ambazo TANROADS mmekuwa mnaziamua na kuzipangia bajeti bila ya kutushirikisha” walisema.
Waliongeza kuwa mabadiliko hayo yasipofanyika ni wazi hadi tunaingia kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2010,barabara nyingi zitakuwa zimetengenezwa lakini zitakuwa hazijibu utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2005-2010.
Walisema haiwezekani TANROADS wawe wanaamua barabara zipi za kutengenezwa, kupanga bajeti na kisha kuileta kwenye kikao cha Bodi ya Barabara kwa ajili ya kuwasomea tu wajumbe,hali ambayo inakuwa haisadii.
“Tuachane na utaratibu huu uliopo hivi sasa kwani barabara hizi ni zetu na nyie TANROADS ni wakala tu wa kuzisimamia….kwani wananchi ndio wanaoamua barabara ipi itengenezwe kutokana na umuhimu wake na siyo nyie ndio muwe mnawaamulia” walisema.
Kufuatia hali hiyo,Mkuu wa mkoa Mwakipesile alikubaliana na hoja hizo za wajumbe na kuwa kuanzia sasa bajeti hiyo iwe inaletwa kwenye kikao hicho,kujadiriwa kabla ya kuanza kutekelezwa ili barabara zenye umuhimu kwa wananchi ndizo zipewe kipaumbele kikubwa cha kutengenezwa.
Thursday, May 28, 2009
ASKARI WA TANAPA AUAWA NA MWILI WAKE KUTUPWA MFEREJINI.
ASKARI wa Hifadhi ya Taifa (TANAPA), kambi ya Nyota wilayani Mbarali, mwenye cheo cha Staff Sajenti, Brighton Ng’umbi (57), ameuawa na watu wasiojulikana na maiti yake kutupwa katika mfereji wa maji.
Mwili wa marehemu Ng’umbi ambaye alipotea tangu Mei 23,mwaka huu saa 5:00 usiku, akitokea katika baa ya Oasis iliyopo Rujewa, ulikutwa katika mfereji huo unaosafirisha maji kwenye mashamba ya mpunga ya kampuni ya Highland Estate Ltd.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya, Zelothe Stephen, alisema mwili huo uliokotwa jana saa 2:00 asuubuhi ukiwa umetupwa katika mfereji huo.
Stephen alisema uchunguzi uliofanywa kwenye mwili wa marehemu Ng’umbi umeonyesha majeraha kwenye paji lake la uso na mdomoni.
“Polisi inamshikilia Rebecca Emmanuel (39), maarufu zaidi kwa jina la Mwakyami, mkazi wa kijiji cha Ihango, kwa tuhuma za kuhusika na kifo hicho” alisema Stephen.
Alifafanua kuwa mtuhumiwa Rebecca ametiwa mbaroni kwani ndiye alikuwa na marehemu siku ya mwisho kabla ya kutoweka wakiwa wanakunywa vinywaji katika baa hiyo ya Oasis, hivyo anaisadia polisi.
Alisema uchunguzi zaidi ili kuwabaini watuhumiwa waliohusika na mauaji ya askari huyo wa doria wa TANAPA (Park Ranger), unaendelea kufanywa na polisi.
Mwili wa marehemu Ng’umbi ambaye alipotea tangu Mei 23,mwaka huu saa 5:00 usiku, akitokea katika baa ya Oasis iliyopo Rujewa, ulikutwa katika mfereji huo unaosafirisha maji kwenye mashamba ya mpunga ya kampuni ya Highland Estate Ltd.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya, Zelothe Stephen, alisema mwili huo uliokotwa jana saa 2:00 asuubuhi ukiwa umetupwa katika mfereji huo.
Stephen alisema uchunguzi uliofanywa kwenye mwili wa marehemu Ng’umbi umeonyesha majeraha kwenye paji lake la uso na mdomoni.
“Polisi inamshikilia Rebecca Emmanuel (39), maarufu zaidi kwa jina la Mwakyami, mkazi wa kijiji cha Ihango, kwa tuhuma za kuhusika na kifo hicho” alisema Stephen.
Alifafanua kuwa mtuhumiwa Rebecca ametiwa mbaroni kwani ndiye alikuwa na marehemu siku ya mwisho kabla ya kutoweka wakiwa wanakunywa vinywaji katika baa hiyo ya Oasis, hivyo anaisadia polisi.
Alisema uchunguzi zaidi ili kuwabaini watuhumiwa waliohusika na mauaji ya askari huyo wa doria wa TANAPA (Park Ranger), unaendelea kufanywa na polisi.
Wednesday, May 27, 2009
MAUAJI MFYULULIZO YA WANAWAKE YATINGISHA MJI WA MABATINI, JIJINI MBEYA
WIMBI la mauaji ya kinyama ya wanawake, katika eneo la Mabatini jijini Mbeya, linaelekea kuota mizizi, kufuatia mwanamke mwingine kuuawa kikatili kwa kupigwa na kitu kizito kichwani.
Katika tukio hilo, wanawake wengine wawili ambao ni ndugu wa marehemu walijeruhiwa vibaya maeneo ya kichwani na wanaendelea kupata matibabu hospitali ya Rufani Mbeya.
Marehemu ametajwa kuwa ni Vena Kasokela (25), wakati waliojeruhiwa wakitajwa kuwa Emmy (46) na Lydia John (58).
Hivi karibuni mwanamke mjamzito, Jacquliene Mwasunga (18), aliuawa kikatili eneo hilo hilo huku mtoto wa dada ake, ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha pili sekondari ya Legico, Upendo Mwasunga (16), akijeruhiwa kichwani na kukatwa sikio lake kushoto.
Akithibitisha kutokea kwa tukio la kinyama, Kamanda wa polisi mkoani Mbeya, Zelothe Stephen, alisema lilitokea juzi saa 12:00 asubuhi, baada ya watu wasiofahamika kuivamia nyumba hiyo.
Akifafanua, Stephen alisema kuwa marehemu Vena na majeruhi Emmy, walikuwa ni wageni waliokuwa wamefikia kwa mwenyeji wao Lydia ambaye ni mfanyabiashara wa pombe za kienyeji katika klabu moja iliyopo eneo hilo.
"Mara baada ya kuvamiwa, wanawake wote watatu walianza kupigwa maeneo ya kichwani na kitu kizito, na kusababisha majeraha ambapo wote walikimbizwa hospitali ya Rufani Mbeya kwa matibabu" alisema Stephen.
Aliongeza kuwa ilipofika saa 4:00 asubuhi, zilipatikana taarifa kuwa mmoja wa majeruhi, Vena Kasokela, amefariki dunia wakati akiendelea kupatiwa matibabu ili kuokoa maisha yake.
Stephen alisema:"Taarifa za awali kuhusu chanzo cha mauaji haya, zinaonyesha kuwa huenda tukio hili ni la ulipizaji kisasi, kwani majeruhi Emmy alikuwa ameolewa na ameachika hivi karibuni".
Alisema kuwa polisi wanachukulia mauaji hayo kama ni ya kulipiza kisasi, kwani watuhumiwa wa mauaji hao hawakuchukua kitu chochote kutoka nyumba hiyo, hali ambayo ingeashiria kuwa walikuwa ni majambazi wa kawaida.
Aliongeza kuwa kikosi cha upelelezi cha jeshi hilo, kimepelekwa eneo la Mabatini kwa ajili ya kuendelea na uchunguzi zaidi kuhusu tukio hilo la kinyama.
Alisema hivyo polisi wanaendelea na uchunguzi wa matukio yote mawili,aliyoyata kuwa ni kujeruhi na mauaji kwani wana uhakika kuwa wakifanikiwa kuwakamata watuhumiwa basi ni wazi ndio watakuwa wameshiriki katika matukio yote mawili.
Lakini wananchi wa eneo la Mabatini waliozungumza na gazeti hili, kwa nyakati tofauti, wamelitupia lawama jeshi la polisi mkoa kwani hadi leo halijafanikiwa kuwatia mbaroni watuhumiwa wa mauaji ya mwanamke mjamzito, Jacquliene.
Waliongeza kuwa hali ya usalama iliyopo hivi sasa maeneo hayo, hasa kwa wanawake inawatia hofu kwani matukio yote mawili ya mauaji hayo ya mfululizo, yamekuwa yakitokea saa za asubuhi.
"Tunaomba jeshi la polisi lifanye kazi zake kwa ufanisi ili kuweza kuwatia mbaroni watuhumiwa hawa wa mauaji yanayotokea mfululizo... kwa kweli hivi sasa tunaishi kwa maashaka hatujui kesho itakuwa zamu ya nani" walisema.
Katika tukio hilo, wanawake wengine wawili ambao ni ndugu wa marehemu walijeruhiwa vibaya maeneo ya kichwani na wanaendelea kupata matibabu hospitali ya Rufani Mbeya.
Marehemu ametajwa kuwa ni Vena Kasokela (25), wakati waliojeruhiwa wakitajwa kuwa Emmy (46) na Lydia John (58).
Hivi karibuni mwanamke mjamzito, Jacquliene Mwasunga (18), aliuawa kikatili eneo hilo hilo huku mtoto wa dada ake, ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha pili sekondari ya Legico, Upendo Mwasunga (16), akijeruhiwa kichwani na kukatwa sikio lake kushoto.
Akithibitisha kutokea kwa tukio la kinyama, Kamanda wa polisi mkoani Mbeya, Zelothe Stephen, alisema lilitokea juzi saa 12:00 asubuhi, baada ya watu wasiofahamika kuivamia nyumba hiyo.
Akifafanua, Stephen alisema kuwa marehemu Vena na majeruhi Emmy, walikuwa ni wageni waliokuwa wamefikia kwa mwenyeji wao Lydia ambaye ni mfanyabiashara wa pombe za kienyeji katika klabu moja iliyopo eneo hilo.
"Mara baada ya kuvamiwa, wanawake wote watatu walianza kupigwa maeneo ya kichwani na kitu kizito, na kusababisha majeraha ambapo wote walikimbizwa hospitali ya Rufani Mbeya kwa matibabu" alisema Stephen.
Aliongeza kuwa ilipofika saa 4:00 asubuhi, zilipatikana taarifa kuwa mmoja wa majeruhi, Vena Kasokela, amefariki dunia wakati akiendelea kupatiwa matibabu ili kuokoa maisha yake.
Stephen alisema:"Taarifa za awali kuhusu chanzo cha mauaji haya, zinaonyesha kuwa huenda tukio hili ni la ulipizaji kisasi, kwani majeruhi Emmy alikuwa ameolewa na ameachika hivi karibuni".
Alisema kuwa polisi wanachukulia mauaji hayo kama ni ya kulipiza kisasi, kwani watuhumiwa wa mauaji hao hawakuchukua kitu chochote kutoka nyumba hiyo, hali ambayo ingeashiria kuwa walikuwa ni majambazi wa kawaida.
Aliongeza kuwa kikosi cha upelelezi cha jeshi hilo, kimepelekwa eneo la Mabatini kwa ajili ya kuendelea na uchunguzi zaidi kuhusu tukio hilo la kinyama.
Alisema hivyo polisi wanaendelea na uchunguzi wa matukio yote mawili,aliyoyata kuwa ni kujeruhi na mauaji kwani wana uhakika kuwa wakifanikiwa kuwakamata watuhumiwa basi ni wazi ndio watakuwa wameshiriki katika matukio yote mawili.
Lakini wananchi wa eneo la Mabatini waliozungumza na gazeti hili, kwa nyakati tofauti, wamelitupia lawama jeshi la polisi mkoa kwani hadi leo halijafanikiwa kuwatia mbaroni watuhumiwa wa mauaji ya mwanamke mjamzito, Jacquliene.
Waliongeza kuwa hali ya usalama iliyopo hivi sasa maeneo hayo, hasa kwa wanawake inawatia hofu kwani matukio yote mawili ya mauaji hayo ya mfululizo, yamekuwa yakitokea saa za asubuhi.
"Tunaomba jeshi la polisi lifanye kazi zake kwa ufanisi ili kuweza kuwatia mbaroni watuhumiwa hawa wa mauaji yanayotokea mfululizo... kwa kweli hivi sasa tunaishi kwa maashaka hatujui kesho itakuwa zamu ya nani" walisema.
Tuesday, May 26, 2009
VIMBWANGA MICHEZONI
Subscribe to:
Posts (Atom)